Depression inaniathiri, nakaribia kujiua

Depression inaniathiri, nakaribia kujiua

Pole sana ndugu hizo ni changamoto za dunia jipe Moyo.

Mods tumewahi kuomba mara kadhaa kwamba wakati umefika tupate Jukwaa la "Mental therapy" na "Ushauri nasaha/Counselling"


Matatizo ya afya ya akili yanashika kasi sana nyakati hizi na mpaka kuja kugundua viashiria inakuwa too late na tunapoteza wapendwa wetu wengi.


Kama tumeweza kuwa na Jukwaa la Jokes ama Mizaha sidhani kama tutashindwa kuwa na Jukwaa muhimu linalohusiana na Afya Ya Akili. Naomba kuwasilisha.


CC Maxence Melo

JamiiForums
 
Najitahidi mkuu ila kwa kiasi fulani inakera sana ..
hiyo inayoitwa "kukera" itupe kwenye dust bin...enyoy maisha yako, focus kinachotakiwa kufanywa sasa kwenye maisha yako vs umri wako...... work hard man, earn big....hilo ndio la msingi mengine unapoteza muda wako na kujikabidhi kwa shetani kirahisi..
 
Nikupongeze mkuu, HONGERA sana.

Ujue kwanini? Kwanza uandishi wako murua (at 19 years) inaonesha wewe ni AKILI kubwa.

Na hizo emoji za kucheka ukiwa unaandika ushuhuda uliouita wa kuumiza, hadi hapo ni kwamba unao ujasiri na umeweza kupuuza na kusonga mbele.

Ushauri wangu, jikubali ulivyo na umshukuru Mungu… kisha TAFUTA PESA.

Utakuja kuelewa mbeleni.
Asante mkuu
 
Mkuu we nyiuweee....maana maisha mbele Ni magumu Sanaa,nimesoma baadhi ya sababu zako nimeona unautoto mwingi.kuna watu wanavichwa Kama ngumi wanafurahia maisha,Kuna watu wafupi Kama themothi na wanafuraia maisha we jiuweee bwasheeee
Kuna utoto ndio sababu bado ni mtoto 19 yrs
Mshauri kama mtoto au mdogo ako basi!
Ni kweli hata mie nataka atambue kila mtu ana kasoro.shida ni jinsi ya kuhandle maneno ya watu na kufocus kwenye mambo yake.
Mtoa mada mi nakushauri uwe unavaa kofia kama hauko comfortable na hujajikubali.kinyume na hapo ujikubali tu na watu watakuzoea.
Mbona diamond alisemwa sana hadi Leo haters wanamwita domo ila hajali.
Acha na maneno ya watu,achana na ndugu zako.jikubali weka bidii kwenye malengo yako.ukifanikiwa watabadili maneno yaol
 
Pole sana ndugu hizo ni changamoto za dunia jipe Moyo.

Mods tumewahi kuomba mara kadhaa kwamba wakati umefika tupate Jukwaa la "Mental therapy" na "Ushauri nasaha/Counselling"


Matatizo ya afya ya akili yanashika kasi sana nyakati hizi na mpaka kuja kugundua viashiria inakuwa too late na tunapoteza wapendwa wetu wengi.


Kama tumeweza kuwa na Jukwaa la Jokes ama Mizaha sidhani kama tutashindwa kuwa na Jukwaa muhimu linalohusiana na Afya Ya Akili. Naomba kuwasilisha.


CC Maxence Melo

JamiiForums
Asante mkuu
 
hiyo inayoitwa "kukera" itupe kwenye dust bin...enyoy maisha yako, focus kinachotakiwa kufanywa sasa kwenye maisha yako vs umri wako...... work hard man, earn big....hilo ndio la msingi mengine unapoteza muda wako na kujikabidhi kwa shetani kirahisi..
Asante mkuu kwa ushauri
 
Kuna utoto ndio sababu bado ni mtoto 19 yrs
Mshauri kama mtoto au mdogo ako basi!
Ni kweli hata mie nataka atambue kila mtu ana kasoro.shida ni jinsi ya kuhandle maneno ya watu na kufocus kwenye mambo yake.
Mtoa mada mi nakushauri uwe unavaa kofia kama hauko comfortable na hujajikubali.kinyume na hapo ujikubali tu na watu watakuzoea.
Mbona diamond alisemwa sana hadi Leo haters wanamwita domo ila hajali.
Acha na maneno ya watu,achana na ndugu zako.jikubali weka bidii kwenye malengo yako.ukifanikiwa watabadili maneno yaol
Asante mkuu
 
Pole sana kijana,
Kwanza nikupongeze kwa hatua ya kwanza kabisa(kulisema tatizo) kwenye kupambana na mental problem ambayo inakusumbua.

Sjui hiyo mitaa unayotokea kama wamefikia hatua ya kufanya "bulling" mpaka muhusika ukajua kuwa kuna jambo wananionesha.
Kwa upande wangu ningekushauri njia kama tatu;

Moja, husisha familia na ndugu zako juu ya hili linalokukuta na madhara ambayo unayapata (ukieleza mpaka ishu ya suicidal ideation). Wazazi au ndugu yawezkana wamechkulia poa kwa sababu tu wao wanajua "hujafa, hujaumbika" hivyo hawaoni tatizo kwako ila ukiwaeleza kwa undani wao ndio msaada wa kwanza.

Mbili, waalimu shuleni, sio kila mwalimu aliyeshuleni atakuwa na uwezo wa kukusaidia ila naamini wapo walimu wenye uelewa wa maisha pamoja na dunia kwa ujumla hasa wale wenye umri mkubwa na busara. Mueleze kila kitu juu ya tatizo linalokusumbua atakusaidia hasa mazingira ya shule though yote hayo hayatabadili ukweli wa muonekano wako sababu tatizo ni kitu gani wanasema juu yako.

Tatu; nenda hospital kwenye kutengo cha ushauri nasaha au hata kwa magonjwa ya akili kwa sababu depression ni moja ya magonjwa ya akili yanayopelekea watu kujiua.

Lastly, tafuta hela mzee.
 
unazingua wewe..
Mimi mpaka leo sikio langu moja la kulia haliskii vizuri halafu unaskia vizuri, una akili, mikono, miguu.. Unajali nani akiongea? Cha msingi mambo yako yanaenda

Sikufichi mpaka sasa sikio langu moja haliskii vizuri.. Toka shule nimetaniwa majina ya kila aina lakini mpka leo nimekaza mambo yanaenda
 
Kwanza jikubali kwasababu wenye napungufu ni wengi duniani na wanaishi sababu wamejikubali.

Usikubali binadamu akuondolee furaha nafsini mwako kwa maneno yao kwasababu wewe haujajiumba bali umeumbwa hivyo na Mungu.
Asante mkuu
 
Pole sana kijana,
Kwanza nikupongeze kwa hatua ya kwanza kabisa(kulisema tatizo) kwenye kupambana na mental problem ambayo inakusumbua.

Sjui hiyo mitaa unayotokea kama wamefikia hatua ya kufanya "bulling" mpaka muhusika ukajua kuwa kuna jambo wananionesha.
Kwa upande wangu ningekushauri njia kama tatu;

Moja, husisha familia na ndugu zako juu ya hili linalokukuta na madhara ambayo unayapata (ukieleza mpaka ishu ya suicidal ideation). Wazazi au ndugu yawezkana wamechkulia poa kwa sababu tu wao wanajua "hujafa, hujaumbika" hivyo hawaoni tatizo kwako ila ukiwaeleza kwa undani wao ndio msaada wa kwanza.

Mbili, waalimu shuleni, sio kila mwalimu aliyeshuleni atakuwa na uwezo wa kukusaidia ila naamini wapo walimu wenye uelewa wa maisha pamoja na dunia kwa ujumla hasa wale wenye umri mkubwa na busara. Mueleze kila kitu juu ya tatizo linalokusumbua atakusaidia hasa mazingira ya shule though yote hayo hayatabadili ukweli wa muonekano wako sababu tatizo ni kitu gani wanasema juu yako.

Tatu; nenda hospital kwenye kutengo cha ushauri nasaha au hata kwa magonjwa ya akili kwa sababu depression ni moja ya magonjwa ya akili yanayopelekea watu kujiua.

Lastly, tafuta hela mzee.
Asante sana mkuu
 
Habari za muda huu wakuu,

Niende moja kwa moja kwenye mada, mimi ni kijana wa kiume miaka 19 kwa muda mrefu sana nimekua nikisimbuliwa na depression "great depression" inayonifanya kutoyafurahia maisha na kujiona kama mtu anayeishi kwa bahati mbaya au labda sikustahili kuwepo duniani maana nimekua ni mtu wa kuchukiwa na watu mbali mbali either ninaowafahamu au hata wale ambao siwafahamu kwa sababu tu ya muonekano wangu hali iliyopelekea hata kujichukia mwenyewe.

Binafsi muonekano wa masikio yangu sio wa kawaida, kwani yametokeza sana kutokea usawa wa kichwa yani ni dizaini kama popo hivi (bat ears) hali inayopelekea kuwa bullied kila ninapokwenda, kuitwa majina yasiyofaa hata na watu nisiowafahamu, na wengine kwenda mbali zaidi kuukashifu uumbaji wa mwenyezi mungu.

Yafuatayo hapo chini ni baadhi tu ya matukio mengi niliyoyapitia so far ambayo sio siri yananila sana ndani kwa ndani;

✓ Ilikua siku ya jmosi asubuhi nimejiandaa nikasepa skonga Ile kufika nikazuiliwa kuingia simply because kulikua na rule kwamba mwanafunzi yeyoye ambaye ni day scholar siku za jmosi alitakiwa avae casual wear ambayo ni red and black ambavyo Ilikua tofauti kwangu mimi. Basi ikanibidi nivunge tu pale nje, baada ya muda kidogo akaja dem flani hivi wa form 2 (mimi nilikua form 4) basi katika kupiga stori mbili tatu na washkaji zangu wengine wawili tukaamua tutimbe maeneo flani (kupoteza muda of course,Ilikua bado asubuhi kurudi home Ilikua jau).

Kwenye mida ya kama saa nane hivi mchana wale washkaji zangu wawili wakaaga wakasepa nikabaki na yule demu ambapo pia aliniambia nimsindikize kwenye kituo cha daladala asepe na hapo ndipo msala ulipotokea, Ilikua hivi wakati tunatembea kando ya barabara alitokea jamaa flani kwa nyuma yetu akiwa kwenye bodaboda iliyokua ikitembea kwa mwendo wa taratibu, kimuonekano ni mtu mzima ambaye hakosi kuwa na mke na at least watoto wawili.

Kusema ukweli yule jamaa alinidhalilisha sana mbele za watu yani sijui hata nilimkosea nini au kosa langu nini mpaka afikie hatua ya kunifanyia kitendo cha kinyama namna Ile. Alianza kwa kucheka kwa nguvu sana kisha aliongea maneno ambayo yaliniumiza sana na nukuu .. " [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] hivi hujaona wengine, na ex wako amesemaje kuhusu hili" hayo ni baadhi tu ya mengi aliyoyasema akimwambia yule dem. Kusema ukweli nilifedheheka sana mbele za watu, nilirudi home nikajifungia chumbani nikalia sana, sikuwa hata na hamu ya kukutana tena na yule dem jtatu skonga.

✓ siku hiyo baada ya kumaliza michosho ya home hapa nikawa sina chengine cha kufanya nikaamua ninyooshe miguu kitaa, sikufika ata hatua 20 nikakutana na kidem flani kikiwa na boyfriend wake.. aisee maneno yaliyomtoka yule dem kusema ukweli yaliniuma sana, alianza kwa kunishangaa kisha akasema " eeh Mungu anisaidie nisizae mtoto anayefanana kama huyu" . Kusema ukweli niliishiwa nguvu miguu ikanyong'onyea nikaamua tu nirudi home nikalale ..

✓ siku hiyo nikiwa town naelekea kituo cha daladala nisepe home kuna jamaa wawili nikawasikia wanaongea .. mmoja akimuuliza mwenzie " hivi mtu kama huyo unaweza kumuozesha binti yako ?" Nikageuka ghafla nikakuta ameninyooshea kidole . Dah nilicheka tu ila nikachukulia easy tu [emoji23][emoji23]

NB: hii imenitokea mara nyingi sana ndo maana nilichukulia kawaida yani hayo maneno nilisha yazoea ..

✓ kuna mwalimu aliwahi kuniambia mbele ya darasa zima kuwa sifanani na binadamu .. walinicheka sana wanafunzi wenzangu siku Ile [emoji1787][emoji1787]

✓Hayo ni baadhi tu ukiachana na yale madogo madogo kwa mfano unaweza ukawa unaongea na mtu ukimwangalia usoni utagundua ni dizaini kama anakucheka hivi ( japo sina uhakika kama ni kweli au najishtukia ), kingine pia sijui kama kuna jina baya au la kudhalilisha ambalo sijawahi kuitwa ..

Katika pitapita zangu mtandaoni nilikutana na hospitali moja Nairobi ambayo inajihusisha na cosmetic surgery mbali mbali ikiwemo Otoplasty ( ear shaping surgery). Basi nikaamua niwashirikishe wazazi wangu nione kama labda naweza kupata msaada wowote ukizingatia kwamba bei yake ni affordable ( japokua nikiri kwamba hii Ilikua last option kwangu), kwa jinsi nilivyo teseka sikua na jinsi.

Wazazi walikuja na response ambayo sikuitarajia kwani walinigomea katakata kwa hoja zisizo na mashiko sijui Michael Jackson and the like .. kilichoniuma zaidi bi mkubwa asubuhi na mapema akampigia kaka yangu mkubwa kunishtakia, bro nayeye alivyo mweupe kichwani bila ya kuuliza akanipandia hewani akawasha moto vilivyo [emoji23][emoji23].. tena kwa msisitizo akapayuka "SIO KWA HELA YANGU!, SIO KWA HELA YANGU!!"

Kusema ukweli nilivunjika sana moyo yani hapa saivi nnavyoandika nina zaidi ya miezi sita sijamtafuta mzee wala bimkubwa yani itokee sana wakipiga wao kwenye simu ya sister angu mkubwa wakiomba kuongea na mimi ndo huwa naongea nao tu hivo hivo kinafki lakini moyoni najikuta nawachukia sana wazazi wangu (Mungu anisamehe sijapenda ila depression inapelekea yote hayo)

Yani ukweli ni kwamba nimeathirika sana kisaikolojia nimekua mtu wa kujifungia tu chumbani siku nzima, hata darasani nashindwa kusimama mbele za watu nikazungumza yani itokee hata ka birthday party home nitajitungia tu kasafari ilimradi tu nisiwepo kwenye mkusanyiko wa watu.

Jambo linaloniumiza sana ni kwamba hakuna anayejali hali ninayopitia hata sister angu ninayeishi nae hapa ata akuone ni mwenye mawazo kiasi gani atakupita kama hakuoni jambo ambalo linazidi kuniongezea depression na kujiona sifai yani kwa kifupi sina mtu wa kumueleza hali ninayopitia. Ila yote kwa yote, shetani nae hachezi mbali maana wazo la kujiua limekua likinijia mara kwa mara lakini nashukuru Mungu amenisimamia mpaka leo sijachukua maamuzi magumu ..

Yote kwa yote naamini JF the home of great thinkers nitapata mawazo chanya yatakayo nisaidia kujua jinsi gani napambana na hali hii ya depression.

NB: Najua kuna wanaopitia magumu zaidi yangu ila amini usiamini mambo madogo madogo kama haya psychologically ni very draining yanaumiza.

#NAWASILISHA
Hongera
 
unazingua wewe..
Mimi mpaka leo sikio langu moja la kulia haliskii vizuri halafu unaskia vizuri, una akili, mikono, miguu.. Unajali nani akiongea? Cha msingi mambo yako yanaenda

Sikufichi mpaka sasa sikio langu moja haliskii vizuri.. Toka shule nimetaniwa majina ya kila aina lakini mpka leo nimekaza mambo yanaenda
Pole mkuu
 
Watu watakubeza ila naelewa Mkuu

Wengi wanaokupa ushauri hawajawahi kupitia hii bullying

Inaumiza unaweza jihisi una laana na kukosoa uumbaji wa Mungu

But keeping moving focus sna Kwa yanakuhusu (yaani wew mwenyewe)

Jifunze tabia ya kuwapuuza hii itakusaidia pandikiza +ve energy ya kujikubali
 
Aise, pole sana aise, usijinyonge, utakuwa mbinafsi nambari moja ukifanya hivyo. Wazazi usione hawana time. Ni vile wazazi wanaile nature ya kuwa protective kwa watoto wao hata awe mtu mzima. Hapo wameona hoja yako haina msingi na wanahofu badala ya kurekebisha ndio utajiharibu zaidi. Uamuzi wa kujinyonga ndio utawapa majonzi makubwa.

Cha kukushauri, puuzi mitazamo hasi yote juu yako, jikite kujenga maisha. Who knows?! Ukipata pesa yako hakuna atakayekuuliza, utaenda kufanya hizo plastic surgery vile utakavyo.
 
Back
Top Bottom