Depression inaniathiri, nakaribia kujiua

Depression inaniathiri, nakaribia kujiua

Poleh sana mdogo wangu
Nashauri uende kwa wanaotoa ushauri/wanasaikolojia

Mueleze hio shida
Mwambie akupe mbinu za kujipenda na kujikubali jinsi ulivyo
Utasogeza muda
Ukiwa na hela yako mwenyewe utaamu ujikubali ama ubadili mwonekano.,
Asante mkuu
 
Kuna wakati fulani nilipanda mlima Kilimanjaro sasa katika group tulilokuwa mimi kidogo ndio nilikuwa mdogo kiumri na kiumbo pia wakati ndio tumeanza safari nilikutana na kijana kama mimi kiumbo na umri pia unaonekana ulikuwa kama wangu sasa, chakushangaza yeye katika mguu wake wa kulia alikuwa amekatwa mguu yani huu unyayo wa kukanyagia chini au eneo linalovishwa kiatu hakuwa nalo, na just imagine kwamba alipanda kama poster ( mbeba mzigo with 20 KG mgongoni ) alafu anapandisha mlima. Nilipomwona nilimuonea huruma na kabla ya safari niliingiwa na hofu ya kutoweza kupanda mlima. Toka nilipomwona nilipata ujasiri kuwa mimi ni mzima na ninaweza

Toka nilipomwona huyo jamaa sikuwahi kata tamaa katika jambo nalolifanya, nikimkumbuka ananipa ujasiri mkubwa wakufanya maajabu.
 
Hakuna watu wenye stress kama wenye vibamia mkuu, na wanaishi! Mimi nna madikio pengine yanazidi yako, nishaitwa ponjoro, masikio popo, majina ya kishenzi kama yoote kipindi nipo mdogo, lakini leo hii masikio yangu yapo vile vile na sisikii hizo habari na kama wapo wanaonisema basi si mbele yangu, sijali na mi mwenyewe najiona wa kawaida tu na maisha yanaenda fresh! Usijitie msongo wa mawazo mkuu, unaonekana una akili, itumie ndugu utafika mbali, acha kifo kikutafute chenuewe sio wewe ukitafute! Kuanzia sasa achana na fikra hizo kabisa, wengi wamekushauri mambo ya msingi na nnaamini huko uliko ushhapata nguvu ya kitosha sana kusonga na kuachana na nawazo ya kutaka kuwaachia dunia wapuuzi ambao woote wana vilema vyao.
Asante kwa ushauri mkuu
 
Wewe mtoto naomba kwanza amini Mungu anakupenda na ndio maana alikuumba!! Mtu asiyeweza hata kujiongezea unywele mmoja asikutishe!! Uzuri au ubaya wa sura waachie wanadamu!! Jikubali na mtu akikuoneshea dharau ukiweza mwambie nashukuru sana kwa kuwa wewe unaweza kuumba walio wazuri!!! Amini Mungu anakupenda saanaa!!
Asante mkuu
 
Tumia changamoto kuwa furusa! Fungua banda la masikio!
Andiko masikio adimu yanaonekana hapa!
Weka picha ya sungura halafu kwa pembeni weka njoo ujionee masikio yanayogeuka, ongezea na chumvi kwamba masikio yako yanasikia hadi usiku ukiwa umelala hivyo kampuni za ulinzi zitakugombania kwa dau!
Hukupewa masikio hayo bila kusudi la Mungu, huenda huo ndiyo mgodi wako wa kupiga hela, wengine wanapewa kipaji wewe umepewa masikio!

Ebu njoo inbobo tuyajenge nikupe mtaji
😁😁😁😁😁😁😁
 
Kuna wakati fulani nilipanda mlima Kilimanjaro sasa katika group tulilokuwa mimi kidogo ndio nilikuwa mdogo kiumri na kiumbo pia wakati ndio tumeanza safari nilikutana na kijana kama mimi kiumbo na umri pia unaonekana ulikuwa kama wangu sasa, chakushangaza yeye katika mguu wake wa kulia alikuwa amekatwa mguu yani huu unyayo wa kukanyagia chini au eneo linalovishwa kiatu hakuwa nalo, na just imagine kwamba alipanda kama poster ( mbeba mzigo with 20 KG mgongoni ) alafu anapandisha mlima. Nilipomwona nilimuonea huruma na kabla ya safari niliingiwa na hofu ya kutoweza kupanda mlima. Toka nilipomwona nilipata ujasiri kuwa mimi ni mzima na ninaweza

Toka nilipomwona huyo jamaa sikuwahi kata tamaa katika jambo nalolifanya, nikimkumbuka ananipa ujasiri mkubwa wakufanya maajabu.
Asante kwa inspiration mkuu
 
Ignoring na kuchukulia kawaida sana kutakuokoa pia jione you are the best above anyone
 
Mkuu pole sana kikubwa ni kujikubali jinsi ulivyo , Ni watu wengi sana wana matatizo kama yako tena la kwako dogo. Jikubali wewe ni mtoto wa kiume usiyumbishwe na maneno ya watu tena wapumbavu. Fight umezaliwa wa kiume pambana, Mtangulize Mungu kwa kila jambo usiogope chochote.

UKITAKA MSAADA NI PM ANY TIME NITAKUSAIDIA
 
Mkuu pole sana kikubwa ni kujikubali jinsi ulivyo , Ni watu wengi sana wana matatizo kama yako tena la kwako dogo. Jikubali wewe ni mtoto wa kiume usiyumbishwe na maneno ya watu tena wapumbavu. Fight umezaliwa wa kiume pambana, Mtangulize Mungu kwa kila jambo usiogope chochote.

UKITAKA MSAADA NI PM ANY TIME NITAKUSAIDIA
Nashukuru sana mkuu
 
Nakumbuka wakati niko mtoto, katika vurugu za utoto kuna mtoto aliwahi kusema eti nina pua kubwa🤣

Kweli nikawa nikijiangalia kwenye kioo, najiona kweli nina pua kubwa kweli, wakati kawaida tu 🤣
😂😂😂 tuma picha hapa tuone kubwa au ndogo kweli
 
Nashukuru sana mkuu
Mleta mada pole kwa changamoto unayopitia lakini nakushauri usikate tamaa na wala usifikirie kujiua mimi pia katika makuzi yangu nilipitia changamoto kama yako mimi ilikuwa ni muonekano wa mdomo kuwa mkubwa like diamond hii ishu ilinitesa sana kwenye makuzi mpaka nilifikiria nikikua nitafute hospital yoyote ya upasuaji yaani hata nikiwa uwanjani maana nilikuwa na kipaji futball mashabiki pinzani walikuwa wananitania kinoma age ya kuanzia miaka 6,7,8,9 mpaka 16 nimepata shida but nikaamua kukubali hali yangu from now nachukulia normal wewe mcheki Manara jinsi alivyo lakini anaenjoy life so minakushauri jikubali na pambana kwenye life ili uje uwe kioo cha jamii
 
😂😂😂 tuma picha hapa tuone kubwa au ndogo kweli
Ni ya kawaida tu maana sijawahi kuwa bullied wala kuambiwa na mtu mwingine tena...Kitu kingine ni mimi ni mweusi ila siyo kama Baraka the prince🤣 ila wakati wa utoto mtu anakushambulia wewe mweusi, kweli ukijiona kwenye kioo unajisikia vibaya wakati ni issue ya kijinga tu.
 
Dogo usikate tamaa na vitu ambavyo huwezi kuvi control. Relax
Then litafute kusudi la kuumbwa kwetu na uendelee kuishi.zingatia tumeumbwa ili
1. Tumjue Mungu
2. Tumtumikie Mungu
3.Tumpende
4 na tuishi nae milele.

Ishu ukizingatia haya mambo manne.
Usiruhusu hata siku.moja Hali yako ikakupelekea kushindwa kutimiza haya.
Na ukitaniwa husionyeshe kukasirika kwa kuwa utazidisha utani na watu wapuuzi. Ila naimani hujakutana na mitoto mitukutu ya uswazi, wakikutania ukionyesha tu hasira UMEISHaa.
 
Habari za muda huu wakuu,

Niende moja kwa moja kwenye mada, mimi ni kijana wa kiume miaka 19 kwa muda mrefu sana nimekua nikisimbuliwa na depression "great depression" inayonifanya kutoyafurahia maisha na kujiona kama mtu anayeishi kwa bahati mbaya au labda sikustahili kuwepo duniani maana nimekua ni mtu wa kuchukiwa na watu mbali mbali either ninaowafahamu au hata wale ambao siwafahamu kwa sababu tu ya muonekano wangu hali iliyopelekea hata kujichukia mwenyewe.

Binafsi muonekano wa masikio yangu sio wa kawaida, kwani yametokeza sana kutokea usawa wa kichwa yani ni dizaini kama popo hivi (bat ears) hali inayopelekea kuwa bullied kila ninapokwenda, kuitwa majina yasiyofaa hata na watu nisiowafahamu, na wengine kwenda mbali zaidi kuukashifu uumbaji wa mwenyezi mungu.

Yafuatayo hapo chini ni baadhi tu ya matukio mengi niliyoyapitia so far ambayo sio siri yananila sana ndani kwa ndani;

✓ Ilikua siku ya jmosi asubuhi nimejiandaa nikasepa skonga Ile kufika nikazuiliwa kuingia simply because kulikua na rule kwamba mwanafunzi yeyoye ambaye ni day scholar siku za jmosi alitakiwa avae casual wear ambayo ni red and black ambavyo Ilikua tofauti kwangu mimi. Basi ikanibidi nivunge tu pale nje, baada ya muda kidogo akaja dem flani hivi wa form 2 (mimi nilikua form 4) basi katika kupiga stori mbili tatu na washkaji zangu wengine wawili tukaamua tutimbe maeneo flani (kupoteza muda of course,Ilikua bado asubuhi kurudi home Ilikua jau).

Kwenye mida ya kama saa nane hivi mchana wale washkaji zangu wawili wakaaga wakasepa nikabaki na yule demu ambapo pia aliniambia nimsindikize kwenye kituo cha daladala asepe na hapo ndipo msala ulipotokea, Ilikua hivi wakati tunatembea kando ya barabara alitokea jamaa flani kwa nyuma yetu akiwa kwenye bodaboda iliyokua ikitembea kwa mwendo wa taratibu, kimuonekano ni mtu mzima ambaye hakosi kuwa na mke na at least watoto wawili.

Kusema ukweli yule jamaa alinidhalilisha sana mbele za watu yani sijui hata nilimkosea nini au kosa langu nini mpaka afikie hatua ya kunifanyia kitendo cha kinyama namna Ile. Alianza kwa kucheka kwa nguvu sana kisha aliongea maneno ambayo yaliniumiza sana na nukuu .. " [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] hivi hujaona wengine, na ex wako amesemaje kuhusu hili" hayo ni baadhi tu ya mengi aliyoyasema akimwambia yule dem. Kusema ukweli nilifedheheka sana mbele za watu, nilirudi home nikajifungia chumbani nikalia sana, sikuwa hata na hamu ya kukutana tena na yule dem jtatu skonga.

✓ siku hiyo baada ya kumaliza michosho ya home hapa nikawa sina chengine cha kufanya nikaamua ninyooshe miguu kitaa, sikufika ata hatua 20 nikakutana na kidem flani kikiwa na boyfriend wake.. aisee maneno yaliyomtoka yule dem kusema ukweli yaliniuma sana, alianza kwa kunishangaa kisha akasema " eeh Mungu anisaidie nisizae mtoto anayefanana kama huyu" . Kusema ukweli niliishiwa nguvu miguu ikanyong'onyea nikaamua tu nirudi home nikalale ..

✓ siku hiyo nikiwa town naelekea kituo cha daladala nisepe home kuna jamaa wawili nikawasikia wanaongea .. mmoja akimuuliza mwenzie " hivi mtu kama huyo unaweza kumuozesha binti yako ?" Nikageuka ghafla nikakuta ameninyooshea kidole . Dah nilicheka tu ila nikachukulia easy tu [emoji23][emoji23]

NB: hii imenitokea mara nyingi sana ndo maana nilichukulia kawaida yani hayo maneno nilisha yazoea ..

✓ kuna mwalimu aliwahi kuniambia mbele ya darasa zima kuwa sifanani na binadamu .. walinicheka sana wanafunzi wenzangu siku Ile [emoji1787][emoji1787]

✓Hayo ni baadhi tu ukiachana na yale madogo madogo kwa mfano unaweza ukawa unaongea na mtu ukimwangalia usoni utagundua ni dizaini kama anakucheka hivi ( japo sina uhakika kama ni kweli au najishtukia ), kingine pia sijui kama kuna jina baya au la kudhalilisha ambalo sijawahi kuitwa ..

Katika pitapita zangu mtandaoni nilikutana na hospitali moja Nairobi ambayo inajihusisha na cosmetic surgery mbali mbali ikiwemo Otoplasty ( ear shaping surgery). Basi nikaamua niwashirikishe wazazi wangu nione kama labda naweza kupata msaada wowote ukizingatia kwamba bei yake ni affordable ( japokua nikiri kwamba hii Ilikua last option kwangu), kwa jinsi nilivyo teseka sikua na jinsi.

Wazazi walikuja na response ambayo sikuitarajia kwani walinigomea katakata kwa hoja zisizo na mashiko sijui Michael Jackson and the like .. kilichoniuma zaidi bi mkubwa asubuhi na mapema akampigia kaka yangu mkubwa kunishtakia, bro nayeye alivyo mweupe kichwani bila ya kuuliza akanipandia hewani akawasha moto vilivyo [emoji23][emoji23].. tena kwa msisitizo akapayuka "SIO KWA HELA YANGU!, SIO KWA HELA YANGU!!"

Kusema ukweli nilivunjika sana moyo yani hapa saivi nnavyoandika nina zaidi ya miezi sita sijamtafuta mzee wala bimkubwa yani itokee sana wakipiga wao kwenye simu ya sister angu mkubwa wakiomba kuongea na mimi ndo huwa naongea nao tu hivo hivo kinafki lakini moyoni najikuta nawachukia sana wazazi wangu (Mungu anisamehe sijapenda ila depression inapelekea yote hayo)

Yani ukweli ni kwamba nimeathirika sana kisaikolojia nimekua mtu wa kujifungia tu chumbani siku nzima, hata darasani nashindwa kusimama mbele za watu nikazungumza yani itokee hata ka birthday party home nitajitungia tu kasafari ilimradi tu nisiwepo kwenye mkusanyiko wa watu.

Jambo linaloniumiza sana ni kwamba hakuna anayejali hali ninayopitia hata sister angu ninayeishi nae hapa ata akuone ni mwenye mawazo kiasi gani atakupita kama hakuoni jambo ambalo linazidi kuniongezea depression na kujiona sifai yani kwa kifupi sina mtu wa kumueleza hali ninayopitia. Ila yote kwa yote, shetani nae hachezi mbali maana wazo la kujiua limekua likinijia mara kwa mara lakini nashukuru Mungu amenisimamia mpaka leo sijachukua maamuzi magumu ..

Yote kwa yote naamini JF the home of great thinkers nitapata mawazo chanya yatakayo nisaidia kujua jinsi gani napambana na hali hii ya depression.

NB: Najua kuna wanaopitia magumu zaidi yangu ila amini usiamini mambo madogo madogo kama haya psychologically ni very draining yanaumiza.

#NAWASILISHA
Dogo, dawa siyo kujiua! Dawa nzuri ni kutafuta tu hela kwa bidii! Halafu utashangaa utakavyo sifiwa ya kwamba wewe ni handsome! Na una masikio mazuri kama Jay Z!! 🥵

Hujamuona hata yule msanii wetu aliyekuwa akidharauliwa enzi akiwa hana kitu? Eti alikuwa na mdomo mkubwa! 😃 Leo hii anakula tu na kuwazalisha watoto wazuri! Wanamuona ni bonge la handsome! Tafuta hela Dogo, halafu utakuja kunishukuru baadae kwa huu ushauri.
 
Habari za muda huu wakuu,

Niende moja kwa moja kwenye mada, mimi ni kijana wa kiume miaka 19 kwa muda mrefu sana nimekua nikisimbuliwa na depression "great depression" inayonifanya kutoyafurahia maisha na kujiona kama mtu anayeishi kwa bahati mbaya au labda sikustahili kuwepo duniani maana nimekua ni mtu wa kuchukiwa na watu mbali mbali either ninaowafahamu au hata wale ambao siwafahamu kwa sababu tu ya muonekano wangu hali iliyopelekea hata kujichukia mwenyewe.

Binafsi muonekano wa masikio yangu sio wa kawaida, kwani yametokeza sana kutokea usawa wa kichwa yani ni dizaini kama popo hivi (bat ears) hali inayopelekea kuwa bullied kila ninapokwenda, kuitwa majina yasiyofaa hata na watu nisiowafahamu, na wengine kwenda mbali zaidi kuukashifu uumbaji wa mwenyezi mungu.

Yafuatayo hapo chini ni baadhi tu ya matukio mengi niliyoyapitia so far ambayo sio siri yananila sana ndani kwa ndani;

✓ Ilikua siku ya jmosi asubuhi nimejiandaa nikasepa skonga Ile kufika nikazuiliwa kuingia simply because kulikua na rule kwamba mwanafunzi yeyoye ambaye ni day scholar siku za jmosi alitakiwa avae casual wear ambayo ni red and black ambavyo Ilikua tofauti kwangu mimi. Basi ikanibidi nivunge tu pale nje, baada ya muda kidogo akaja dem flani hivi wa form 2 (mimi nilikua form 4) basi katika kupiga stori mbili tatu na washkaji zangu wengine wawili tukaamua tutimbe maeneo flani (kupoteza muda of course,Ilikua bado asubuhi kurudi home Ilikua jau).

Kwenye mida ya kama saa nane hivi mchana wale washkaji zangu wawili wakaaga wakasepa nikabaki na yule demu ambapo pia aliniambia nimsindikize kwenye kituo cha daladala asepe na hapo ndipo msala ulipotokea, Ilikua hivi wakati tunatembea kando ya barabara alitokea jamaa flani kwa nyuma yetu akiwa kwenye bodaboda iliyokua ikitembea kwa mwendo wa taratibu, kimuonekano ni mtu mzima ambaye hakosi kuwa na mke na at least watoto wawili.

Kusema ukweli yule jamaa alinidhalilisha sana mbele za watu yani sijui hata nilimkosea nini au kosa langu nini mpaka afikie hatua ya kunifanyia kitendo cha kinyama namna Ile. Alianza kwa kucheka kwa nguvu sana kisha aliongea maneno ambayo yaliniumiza sana na nukuu .. " [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] hivi hujaona wengine, na ex wako amesemaje kuhusu hili" hayo ni baadhi tu ya mengi aliyoyasema akimwambia yule dem. Kusema ukweli nilifedheheka sana mbele za watu, nilirudi home nikajifungia chumbani nikalia sana, sikuwa hata na hamu ya kukutana tena na yule dem jtatu skonga.

✓ siku hiyo baada ya kumaliza michosho ya home hapa nikawa sina chengine cha kufanya nikaamua ninyooshe miguu kitaa, sikufika ata hatua 20 nikakutana na kidem flani kikiwa na boyfriend wake.. aisee maneno yaliyomtoka yule dem kusema ukweli yaliniuma sana, alianza kwa kunishangaa kisha akasema " eeh Mungu anisaidie nisizae mtoto anayefanana kama huyu" . Kusema ukweli niliishiwa nguvu miguu ikanyong'onyea nikaamua tu nirudi home nikalale ..

✓ siku hiyo nikiwa town naelekea kituo cha daladala nisepe home kuna jamaa wawili nikawasikia wanaongea .. mmoja akimuuliza mwenzie " hivi mtu kama huyo unaweza kumuozesha binti yako ?" Nikageuka ghafla nikakuta ameninyooshea kidole . Dah nilicheka tu ila nikachukulia easy tu [emoji23][emoji23]

NB: hii imenitokea mara nyingi sana ndo maana nilichukulia kawaida yani hayo maneno nilisha yazoea ..

✓ kuna mwalimu aliwahi kuniambia mbele ya darasa zima kuwa sifanani na binadamu .. walinicheka sana wanafunzi wenzangu siku Ile [emoji1787][emoji1787]

✓Hayo ni baadhi tu ukiachana na yale madogo madogo kwa mfano unaweza ukawa unaongea na mtu ukimwangalia usoni utagundua ni dizaini kama anakucheka hivi ( japo sina uhakika kama ni kweli au najishtukia ), kingine pia sijui kama kuna jina baya au la kudhalilisha ambalo sijawahi kuitwa ..

Katika pitapita zangu mtandaoni nilikutana na hospitali moja Nairobi ambayo inajihusisha na cosmetic surgery mbali mbali ikiwemo Otoplasty ( ear shaping surgery). Basi nikaamua niwashirikishe wazazi wangu nione kama labda naweza kupata msaada wowote ukizingatia kwamba bei yake ni affordable ( japokua nikiri kwamba hii Ilikua last option kwangu), kwa jinsi nilivyo teseka sikua na jinsi.

Wazazi walikuja na response ambayo sikuitarajia kwani walinigomea katakata kwa hoja zisizo na mashiko sijui Michael Jackson and the like .. kilichoniuma zaidi bi mkubwa asubuhi na mapema akampigia kaka yangu mkubwa kunishtakia, bro nayeye alivyo mweupe kichwani bila ya kuuliza akanipandia hewani akawasha moto vilivyo [emoji23][emoji23].. tena kwa msisitizo akapayuka "SIO KWA HELA YANGU!, SIO KWA HELA YANGU!!"

Kusema ukweli nilivunjika sana moyo yani hapa saivi nnavyoandika nina zaidi ya miezi sita sijamtafuta mzee wala bimkubwa yani itokee sana wakipiga wao kwenye simu ya sister angu mkubwa wakiomba kuongea na mimi ndo huwa naongea nao tu hivo hivo kinafki lakini moyoni najikuta nawachukia sana wazazi wangu (Mungu anisamehe sijapenda ila depression inapelekea yote hayo)

Yani ukweli ni kwamba nimeathirika sana kisaikolojia nimekua mtu wa kujifungia tu chumbani siku nzima, hata darasani nashindwa kusimama mbele za watu nikazungumza yani itokee hata ka birthday party home nitajitungia tu kasafari ilimradi tu nisiwepo kwenye mkusanyiko wa watu.

Jambo linaloniumiza sana ni kwamba hakuna anayejali hali ninayopitia hata sister angu ninayeishi nae hapa ata akuone ni mwenye mawazo kiasi gani atakupita kama hakuoni jambo ambalo linazidi kuniongezea depression na kujiona sifai yani kwa kifupi sina mtu wa kumueleza hali ninayopitia. Ila yote kwa yote, shetani nae hachezi mbali maana wazo la kujiua limekua likinijia mara kwa mara lakini nashukuru Mungu amenisimamia mpaka leo sijachukua maamuzi magumu ..

Yote kwa yote naamini JF the home of great thinkers nitapata mawazo chanya yatakayo nisaidia kujua jinsi gani napambana na hali hii ya depression.

NB: Najua kuna wanaopitia magumu zaidi yangu ila amini usiamini mambo madogo madogo kama haya psychologically ni very draining yanaumiza.

#NAWASILISHA
Kwanza hongera kwa uandishi bora kabisa.Hakika na class utakuwa vizuri ila hio ni inferior complex.Wote tumeubwa kwa mfano wake hakuna aliye mbaya ila kikubwa mkuu.Tutafute pesa uone kama kuna mtu atakudharau..Jikubali your the best mbona mi na kibyongo ila am still the best.
 
Back
Top Bottom