Dereva Mtanzania anayeshikiliwa Sudani Kusini kwa kugonga mtu aendelea kusota gerezani, familia ya aliyegonjwa yataka fidia

Dereva Mtanzania anayeshikiliwa Sudani Kusini kwa kugonga mtu aendelea kusota gerezani, familia ya aliyegonjwa yataka fidia

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2025-02-21 at 06.22.21_45162f04.jpg
Dereva Mtanzania Juma Ally Maganga (45) anayeshikiliwa na Jeshi la Polisi katika Mji wa Juba tangu Februari 14, 2025 kwa tuhuma za kugonga na kusababisha kifo cha Mtu, imeelezwa familia ya aliyefariki imetoa maelekezo ya kudai fidia ili Juma aachiwe.

JamiiForums imewasiliana na Mmiliki wa Kampuni ya Kiliki, Gabriel Kiliki ambaye gari lake ndilo lilihusika, amesema “Nimeelezwa Baba wa marehemu anataka fidia Dola 3,200 (Tsh. Milioni 8.2) kisha Juma ataachiwa, baada ya hapo kwa kuwa marehemu alikuwa na Wake watatu, kila mmoja wao aelezee mahitaji yao ya fidia, yakitimizwa wataachia gari pamoja na Juma atarusiwa kuondoka Sudani.”

Ameongeza “Hatujataka kufanya malipo hayo kwa kuwa awali kuna malipo tuliambiwa yanahitajika ili wamuachie, yalifanyika na haikujulikana yalipoteaje, Wakala wa Bima ya gari kule Sudani Kusini tunayemtumia anaitwa Alex, naye hatoi ushirikiano kwetu na hatujui nini kinaendelea.”

JamiiForums imewasiliana na Mkurugenzi wa Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje, Mindi Kasiga ambaye awali alisema Idara ya Afrika inafuatilia suala hilo, ambapo pia alisema Tanzania haina Ubalozi Sudani Kusini, amesema “Nitakurudia kukupa mrejesho.”

Ilivyokuwa awali, soma hapa ~ Dereva Mtanzania anashikiliwa Sudan Kusini baada ya kugonga mtu, inadaiwa Polisi wagoma kumuachia wanataka hela
WhatsApp Image 2025-02-23 at 12.51.03_bb2cdcde.jpg
 
. Du shughuli zingine ni ngumu sana kuzifanya..

. Kwa hiyo hapo Sudan hakuna muajiriwa na sa100?? 🤔 🤔
 
Poleni wanaume wote mnaopambana kwa ajili ya familia zenu

Nyie mnaopambania michepuko lolote liwakute
 
Back
Top Bottom