Dereva wa basi azuiwa kuendelea na safari baada kukutwa yupo tungi, vipimo hivi vianze kutumika rasmi kupunguza ajali

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760


Na inaonekana ana jicho limeiva kama nyanya si ajabu kavuta misokoto kadhaa

JESHI la Polisi Kikosi cha Usalama barabarani limeshikilia dreva wa kampuni ya Ahmed Trans lenye namba za Usajili T586 AJH linalofanya safari ya kusafirisha abiria kati ya Mbeya na Tanga Rajab Omari baada ya kumkuta amelewa chakali huku akiwa amebeba abiria tayari ya kwa safari ya kutoka Mbeya kwenda Tanga.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Mbeya Mkuu wa Oparesheni ya Trafic kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi ACP Nassor Sisiwah amesema wakiwa katika zoezi la ukaguzi wamemkamata Dereva huyo na baada ya kumpima wamemkuta na kileva 450 .3 ml/gm kinyume cha sheria.



Your browser is not able to display this video.
 
Naamini watachukua na leseni yake angalau hata kwa mwaka mmoja Kisha wamrejeshee hii itapunguza ajali na kuleta SoMo kwa wengine
 
Zamani raha sana.....
Kuna dereva aliitwa sudi.....anakula maji mpaka baadae...
tunambeba mpaka kwenye gari akisha Kalia kiti utamkubali anavyotandika chuma....ngoma mpera mpera dar arusha masaa 6
 
UZuri mtuhumiwa anahojiwa anakuambia nilikua napumzisha mwili kidogo. Tz raha sana😀
 
Kazi sana ....atapata raha yake anayostahiliii
 
Zamani raha sana.....
Kuna dereva aliitwa sudi.....anakula maji mpaka baadae...
tunambeba mpaka kwenye gari akisha Kalia kiti utamkubali anavyotandika chuma....ngoma mpera mpera dar arusha masaa 6
Mngeingizwa mtaroni au korongoni haki yenu kabisa

Ova
 
Mngeingizwa mtaroni au korongoni haki yenu kabisa

Ova
I normally drink when I do long trip.... Na nakua salama kabsa but I don't advice.

Last time I was with my mother ila nilishukuru kufika. Sio safe kabsa.
 
Yes don't drink n drive,ila wamempima kutumia kipimo gani?blood test ndicho kipimo sahihi ambacho kinaweza kusimama mahakamani kwenye ushahidi,kipimo cha kupuliza kina mapungufu mengi na tatizo la nchi yetu mahakama sio huru na hatuna wanasheria wa kupeleka kesi mahakamani ili kutest kukubalika kwa kipimo cha kupuliza
 
Kutumia kilevi na kuendesha chombo cha moto ni HATARI mno kwa usalama wa watu wote
 
Siamini kama vilevi vinasababisha ajali...ni mtazamo tu
 
Kwenye malori kuna watu tulitembea na magaloni ya gongo na hatukumvunja mtu hata kidole.. 👍
 
Eti isitoshe ni wiki ya usalama
Mpumbavu huyo afungwe tu maana ni muuwaji mtarajiwa
Kwa kama sio wiki ya usalama kulewa ni rukhsa?
. Kuna dereva alikutwa na traffic kalewa halafu badala ya kumkamata akamuita konda aendeshe gari na yeye apumzike kisa ni mshkaji wake au kala hongo sana kwake
Ilikuwa Mwanza hiyo
 
Safi sana, hizi Ajali zinazoangamiza Wananchi zitapungua haswa zile ajali ambazo mpaka huwa unajiuliza huyu Dereva huyu Dereva alikuwa timamu kweli?
 
Amekutwa na alcohol 450 kinyume na sheria. Sheria ni alcohol ngapi ??? Ingekuwa Ulaya polisi au media ingesema 450 ni mara mbili au mara kumi ya kiwango kinachokubalika.




Halafu siku hizi breathalizer ni kidude kinatosha mfukoni, wao la kwao linaishi juu ya meza la chuma limechongwa SIDO, lina miwaya mirefuuu, linawekwa katikati ya barabara puuuuu! No wonder linaletwa barabarani nyakati za sikukuu tu kama alivyosema Kamanda hapo... Nyakati zingine watu hawanywi na ajali hakuna nadhani. Failed states of the third world.




na wamemlazimisha ku plead guilty hapo hapo barabarani, tena aviambie vyombo vya habari, na wakamsainisha guilty plea right there and then!.... halafu mnasema tuunde tume kwa nini wanafunzi wote wa law school wamefeli, wamefeli sheria zipi zinazofuatwa za kufelisha wanafunzi ??? hahahaaaa...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…