Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,621
- 8,411
Mfanyabiashara maarufu nchini ambaye anashika nafasi ya 21 ya utajiri Afrika, Mohamed Dewji ameanza kulipa mishahara ya wachezaji wa klabu hiyo kutokana na klabu kutokuwa na mdhamini.
Taarifa kutoka ndani ya klabu ya Simba zinasema kuwa pamoja na kulipa mishahara ya wachezaji Dewji amekubali pia kuendelea kuisaidia klabu hiyo kwa kutoa gharama za uendeshaji mpaka pale kipindi cha mpito cha miezi sita kitakapomalizika.
Sambamba na msaada huo anaoutoa kwa klabu yake ya samba Dewji aliyeomba kununua asilimia 51 ya hisa za Simba kwa shilingi bilioni 20 ameanza pia kutekeleza ahadi zake alizoahidi wakati ambapo Simba inaelekea katika mfumo wa mabadiliko ya kiuendeshaji.
Wakati mchakato wa kuiondoa samba kutoka katika mfumo wa sasa na kuiingiza katika mfumo wa hisa tayari Dewji amekubali kulipia nyasi za bandia zitakazoletwa nchini kwa aya ujenzi wa uwanja wa mazoezi wa simba.
Itakumbukwa klabu hii imekuwa ikijiendesha yenyewe kupitia wanachama wake na sasa inatarajia kuhamia katika mfumo wa uendeshaji kupitia uuzaji wa hisa ambapo mwenyekiti wake huyo tayari ameomba kununua asilimia 51 ya hisa za klabu hiyo.
Taarifa kutoka ndani ya klabu ya Simba zinasema kuwa pamoja na kulipa mishahara ya wachezaji Dewji amekubali pia kuendelea kuisaidia klabu hiyo kwa kutoa gharama za uendeshaji mpaka pale kipindi cha mpito cha miezi sita kitakapomalizika.
Sambamba na msaada huo anaoutoa kwa klabu yake ya samba Dewji aliyeomba kununua asilimia 51 ya hisa za Simba kwa shilingi bilioni 20 ameanza pia kutekeleza ahadi zake alizoahidi wakati ambapo Simba inaelekea katika mfumo wa mabadiliko ya kiuendeshaji.
Wakati mchakato wa kuiondoa samba kutoka katika mfumo wa sasa na kuiingiza katika mfumo wa hisa tayari Dewji amekubali kulipia nyasi za bandia zitakazoletwa nchini kwa aya ujenzi wa uwanja wa mazoezi wa simba.
Itakumbukwa klabu hii imekuwa ikijiendesha yenyewe kupitia wanachama wake na sasa inatarajia kuhamia katika mfumo wa uendeshaji kupitia uuzaji wa hisa ambapo mwenyekiti wake huyo tayari ameomba kununua asilimia 51 ya hisa za klabu hiyo.