Dhahabu kilo 53 yakamatwa uwanja wa ndege wa Mumbai kutoka kwa wasafiri waliotoka Tanzania

Dhahabu kilo 53 yakamatwa uwanja wa ndege wa Mumbai kutoka kwa wasafiri waliotoka Tanzania

In the first case, customs department seized 53 kg of gold valued at Rs 28.17 crore from four passengers of Indian nationality. The passenger landed at Mumbai airport in a flight from Tanzania. They were smuggling gold in the form of one Kg bars ingeniously concealed in specially designed waist belts with multiple pockets.

Read more at:
Mumbai Airport Customs seize 61 kg gold worth Rs 32 crore in a day. FM Niramala Sitharaman lauds the alertness
Huyo jamaa anafahamika vizuri sana kwa upumbavu wake juu ya maswala kama haya. Ni mmoja wa watu wanaofurahia sana kuona Tanzania ikihujumiwa. Sijui huyu ni mtu wa wapi hasa.
 
Kiongozi yeyote anayejifanya kukumbatia demokrasia katika nchi za Afika hukalibisha wizi, rushwa, ubadhirifu, uonevu na uharifu uliokithiri bila kukemewa kwa kuwa wanufaika wanapata cha kwao ndivyo ilivyo kwa sasa Tanzania hamna kitu na wewe ni mmojawapo mlikokuwa mnashadadia sana utawala huu usiokuwa na huruma na rasilimali za nchi wala kujali wananchi wananufaika moja kwa moja.
akili zikae sawa
Wacha uovu uendelee kwa kuwa aliyekuwa anajitoa mlimchukia na kumfanyia njma ovu na mtakoma sana ili akili zikae sawa.
Acha uongo, kwani kipindi Cha JPM Dhahabu haikukamatwa Nairobi? Ikarudishwa na Kenyatta? Wizi haujawahi kuisha chini ya CCM.

Hata ukaguzi wa Mererani ulionyesha watu walipitisha madini chini ya ukuta!!

Whether JPM au Samia au Kikwete wizi wa madini haukuwahi kuisha msitake kujifanya kama vile CCM iliwahi kuwa safi kipindi Cha JPM.
 
Utetezi wa kipumbavu ulio kubuhu[emoji2959][emoji2959] kabisa! Kama wamefuata utaratibu wange kamatwaje
Anachosema jamaa mfano Kila nchi Ina Sheria zake mathalani unaweza kutoa Hela zako kwenye benki kihalali kabisa ila kusafiri na cash kupo limited kwenye nchi na nchi so ukisafiri na cash labda Dollar laki 5 hawaruhusu so mtu ukikamatwa Nazo ni kosa licha ya kwamba Sio za wizi.

So mtu hata kama angechukua Dhahabu kihalali Bongo ila anaogopa Kodi hizo kwa nchi husika so anaona Bora afiche kwenye begi kuepuka tozo so ukidakwa ni kosa hata kama ulinunua kihalali.

Jamaa ndio alijengea hoja hapo.
 
"In the first case, customs department seized 53 kg of gold valued at Rs 28.17 crore from four passengers of Indian nationality. The passenger landed at Mumbai airport in a flight from Tanzania. They were smuggling gold in the form of one Kg bars ingeniously concealed in specially designed waist belts with multiple pockets.

The specially designed belts with UAE-made gold bars concealed inside were reportedly handed over to the passengers by a person of Sudanese nationality at Doha airport .."

Dhahabu imetoka Tanzania wazi kabisa, kufika Doha ikabidi ifichwe kwenye hizo special belts during Transit.
Huyu mama kawafanya muwe wehu, kila kitu mnatetea, ati tu kwa sababu hamkumpenda JPM, -------- cretinous stupidity
Nakubaliana na hoja zako ila hapo umetranslate kimakosa, hao waliotoka TZ walikua hawana Dhahabu wamepewa na MSUDANI aliyekua DOHA ndio wao wakaipeleka MUMBAI!! So Dhahabu haikusafirishwa from Tanzania according the article ila WAMEIKUTA "njiani".
 
Watanzania hasara tuliyoipata kumpoteza
Magufuli,haipimiki.

Patriots know what I mean.!
 
Whether JPM au Samia au Kikwete wizi wa madini haukuwahi kuisha msitake kujifanya kama vile CCM iliwahi kuwa safi kipindi Cha JPM.
Utaniona mtu wa ajabu sana leo nikipingana nawe katika hili, hasa kumhusu huyo Magufuli, ambaye msimamo wangu unajulikana vizuri juu yake.
Magufuli alipiga kelele, na sote tukazisikia hizo kelele, hata kama zilikuwa ni kama kelele za 'scare crow', lakini watu walizisikia.

Na kwa kweli, asingekuwa ni mtu mwenye papara na kutaka misifa mingi, Magufuli angefahamika kuwa na dhamira ya kuyadhibiti haya madudu. Tatizo, njia zake zilikuwa ni njia za pupa, zisizo na matokeo mazuri.

Umeizungumzia CCM hapo, jambo ambalo ninakubaliana nalo, lakini elewa kwamba CCM kama chama ni kasha tu kwa sasa hivi. Kiongozi yeyote mkuu anayekuwepo sasa hivi analijaza kasha hilo na uchafu wowote anaopenda yeye bila ya kuhojiwa na yeyote.

Hili ndilo tatizo kubwa sana kwa nchi yetu kwa sasa hivi.
 
Nakubaliana na hoja zako ila hapo umetranslate kimakosa, hao waliotoka TZ walikua hawana Dhahabu wamepewa na MSUDANI aliyekua DOHA ndio wao wakaipeleka MUMBAI!! So Dhahabu haikusafirishwa from Tanzania according the article ila WAMEIKUTA "njiani".
LOooo! Aiiiseeeee!

Hivi ninakusoma wewe, au ninamsoma mtu mwingine hapa!

Kwa hiyo 'stori' ndiyo hiyo, hawa wahindi wasafiri walitoka Tanzania safi kabisa, hadi walipofika huko njiani, wakakutana na msudan aliyewatwisha mzigo! Hili ndilo linalopaswa kutupa matumaini makubwa kwamba tupo vizuri sana kwa upande wetu, au siyo?
 
LOooo! Aiiiseeeee!

Hivi ninakusoma wewe, au ninamsoma mtu mwingine hapa!

Kwa hiyo 'stori' ndiyo hiyo, hawa wahindi wasafiri walitoka Tanzania safi kabisa, hadi walipofika huko njiani, wakakutana na msudan aliyewatwisha mzigo! Hili ndilo linalopaswa kutupa matumaini makubwa kwamba tupo vizuri sana kwa upande wetu, au siyo?
Wapi nimetetea? Tunaongelea hiyo article ndio imesema Dhahabu ilikua UAE made (meaning it could've been smuggled from anywhere) ila wasafiri from TZ ndio wakapewa huo mzigo na huyo Msudani kwenda kuuza huko India.

Sasa article au Mimi nani ndio anapinga kuwa Dhahabu haijatoka Tz?
 
Utaniona mtu wa ajabu sana leo nikipingana nawe katika hili, hasa kumhusu huyo Magufuli, ambaye msimamo wangu unajulikana vizuri juu yake.
Magufuli alipiga kelele, na sote tukazisikia hizo kelele, hata kama zilikuwa ni kama kelele za 'scare crow', lakini watu walizisikia.

Na kwa kweli, asingekuwa ni mtu mwenye papara na kutaka misifa mingi, Magufuli angefahamika kuwa na dhamira ya kuyadhibiti haya madudu. Tatizo, njia zake zilikuwa ni njia za pupa, zisizo na matokeo mazuri.

Umeizungumzia CCM hapo, jambo ambalo ninakubaliana nalo, lakini elewa kwamba CCM kama chama ni kasha tu kwa sasa hivi. Kiongozi yeyote mkuu anayekuwepo sasa hivi analijaza kasha hilo na uchafu wowote anaopenda yeye bila ya kuhojiwa na yeyote.

Hili ndilo tatizo kubwa sana kwa nchi yetu kwa sasa hivi.
Dhahabu ya Bongo ilipokamatwa Nairobi kwa msaada wa intelijensia ya Kenyatta nani alikua Rais wa Tanzania? Si JPM, Tena alipiga Hadi simu kumshukuru Kenyatta

Wizi haukuwahi kuisha chini ya CCM...
Kwani Ile audit kwamba Tanzanite ilipitishwa chini ya ukuta ilikua imetokea awamu Gani? Je watu kuchimba kwenye vitalu vya serikali (Reserve) ilitokea awamu Gani?

Acha kutetea wahalifu mkuu, CCM haijawahi kuwa safi tukiendelea kudhani chini ya JPM hakukua na wizi wa madini tutabaki kubadili Marais huku ufisadi hauishi!!
 
Wapi nimetetea? Tunaongelea hiyo article ndio imesema Dhahabu ilikua UAE made (meaning it could've been smuggled from anywhere) ila wasafiri from TZ ndio wakapewa huo mzigo na huyo Msudani kwenda kuuza huko India.

Sasa article au Mimi nani ndio anapinga kuwa Dhahabu haijatoka Tz?
Mbona hueleweki.
Kwa hiyo hiyo makala inapinga kuwa mali haikutoka Tanzania?
 
Yeah Article inasema smugglers wameichukia Dhahabu Doha na Dhahabu iliuzwa huko UAE so MSUDANI ndio akawauzia hao WAHINDI wa MUMBAI ndio wakadakwa huko Airport!!

Sasa wapi article imesema Dhahabu imetokea Tz?? Based on the article sitaki maoni Wala hisia
 
Dhahabu ya Bongo ilipokamatwa Nairobi kwa msaada wa intelijensia ya Kenyatta nani alikua Rais wa Tanzania? Si JPM, Tena alipiga Hadi simu kumshukuru Kenyatta

Wizi haukuwahi kuisha chini ya CCM...
Kwani Ile audit kwamba Tanzanite ilipitishwa chini ya ukuta ilikua imetokea awamu Gani? Je watu kuchimba kwenye vitalu vya serikali (Reserve) ilitokea awamu Gani?

Acha kutetea wahalifu mkuu, CCM haijawahi kuwa safi tukiendelea kudhani chini ya JPM hakukua na wizi wa madini tutabaki kubadili Marais huku ufisadi hauishi!!
Tusibishane hapa kwa jambo ambalo liko wazi.
Magufuli pamoja na ukichaa wake huwezi kumfananisha na Kikwete au huyu Samia katika eneo hili, na hata wewe hilo unalijuwa.
Sijui ni wapi umenisoma katika mistari hiyo hapo juu nikiitetea CCM.
Ila ninachokiona hapa kwa upande wako ni juhudi za kumtetea Samia katika madhaifu yake makubwa sana katika eneo hili na mengineyo.
Tutapata hasara sana chini ya utawala wake huu.
 
Yeah Article inasema smugglers wameichukia Dhahabu Doha na Dhahabu iliuzwa huko UAE so MSUDANI ndio akawauzia hao WAHINDI wa MUMBAI ndio wakadakwa huko Airport!!

Sasa wapi article imesema Dhahabu imetokea Tz?? Based on the article sitaki maoni Wala hisia
Naomba uisome vizuri tena hii habari yako hapa juu ya usahihi wake.
Si jambo jema tuendelee kuzungushana hapa kwa kutafuta njia za kupotosha kilichoandikwa.

Hao wahindi "waliinunua hiyo dhahabu Doha"?
Sasa kama ilikuwa ni mali imenunuliwa kihalali, hao kwenye uwanja wa Mumbai walikuwa na taizo gani na mali halali?
 
Utaniona mtu wa ajabu sana leo nikipingana nawe katika hili, hasa kumhusu huyo Magufuli, ambaye msimamo wangu unajulikana vizuri juu yake.
Magufuli alipiga kelele, na sote tukazisikia hizo kelele, hata kama zilikuwa ni kama kelele za 'scare crow', lakini watu walizisikia.

Na kwa kweli, asingekuwa ni mtu mwenye papara na kutaka misifa mingi, Magufuli angefahamika kuwa na dhamira ya kuyadhibiti haya madudu. Tatizo, njia zake zilikuwa ni njia za pupa, zisizo na matokeo mazuri.

Umeizungumzia CCM hapo, jambo ambalo ninakubaliana nalo, lakini elewa kwamba CCM kama chama ni kasha tu kwa sasa hivi. Kiongozi yeyote mkuu anayekuwepo sasa hivi analijaza kasha hilo na uchafu wowote anaopenda yeye bila ya kuhojiwa na yeyote.

Hili ndilo tatizo kubwa sana kwa nchi yetu kwa sasa hivi.
Kupiga kelele kwenye TV Kuna impact Gani?

1. Nani aliyekamatwa kwa Wizi wa Makinikia Hadi Leo?

2. Mpaka anafariki mbona hakuwa amedai Trillion 450 zetu?

3. Mwanyika tuliyeambiwa ame facilitate wizi wa Makinikia alimpigia kampeni na pia kampa Ubunge wa Makambako.

4. Mpaka anafariki Makinikia yalikua Bado yanasafirishwa nje.

5. Mpaka anafariki Sheria yake ya permanent sovereignty ilishakua imefanyiwa ammendments kibao ikiwemo kuondoa kipengele Cha mashauri ya madai kusikilizwa na mahakama za humu ndani.

6. Licha ya kujenga ukuta tuliambiwa na ripoti ya ukaguzi huko Mererani kuwa madini yaliibwa chini ya ukuta JPM akiwa Rais.

7. Tunaambiwa kitalu Cha serikali kilivamiwa na watu binafsi kuchimba Tanzanite wakati ni reserve for future govt repository!!

Sasa Kama haya yote yamefanyika Kuna faida Gani ya kutoa mapovu kwenye TV huku reality ni tofauti? Au unaona Raha Mama Samia apinge ufisadi kwenye screen huku madini yanatoroshwa kwako wwe inakua enough?
 
Back
Top Bottom