Dhana ya kutenganisha mamlaka (mihimili) ie Separation of powers, je inafanya kazi kwa kiasi gani hapa kwetu?

Dhana ya kutenganisha mamlaka (mihimili) ie Separation of powers, je inafanya kazi kwa kiasi gani hapa kwetu?

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Duniani kote kuna hii dhana ya mihimili ya mahakama, bunge na serikali kutokuingiliana (separation of powers) na kugawana madaraka bila kuathili mawasiliano kwa maana ya coordination baina yao kwa uendeshaji mzuri wa nchi. Ni kwa kiasi gani dhana hii inafanya kazi hapa kwetu?

Je, kiuhalisia/in practice inawezekana kutenganisha mihimili hii isiingiliane kabisa na mambo yakaenda vizuri? Je kuna mifano ya Taifa lolote duniani lililofanikiwa kufanyia kazi dhana hii kwa mafanikio? Karibuni wataalam tujadili.
 
Haijawahi kuwa Applied pahala popote pale katika nchi hii ni maandiko tu na inaudhi kwani ni ubadhirifu wa fedha za waTanzania bora hata bunge, mahakama viondoshwe tu ili tubaki na Serikali tu
 
Kujipendekeza kwa Rais👇😁😁😁
Taifa haliwezi kuendelea kwa mihimili kujipendekeza kwa Rais.She is hopeless fool.
 
Duniani kote kuna hii dhana ya mihimili ya mahakama, bunge na serikali kutokuingiliana (separation of powers) na kugawana madaraka bila kuathili mawasiliano kwa maana...
Haifayi Kazi hapa nchini, kwa kuwa Mwendazake, alishajitapa kuwa mhimili wake ndiyo uliojichmbia zaidi chini!

Naibu Spika wa Bunge, Tulia Ackson amezidi kulithibitisha hilo Jana, kwa kukiri kuwa mhimili wa Rais, unapaswa kuheshimiwa zaidi na haupaswi hata kukosolewa!!
 
Marekani, Uingereza, ni baadi ya wanaofanya vizuri katika separation.

Hapa Tulia anashindwa kumtofautisha Rais kama kiongozi wa Serikali na Rais kama kiongozi wa Dola. Rais kama kiongozi wa serikali yuko sawa na vingozi wa mihimili mingine.

Ila rais kama kongozi wa dola yuko juu ya mihimili yote mitatu. Hivyo Tulia anapaswa kujua ni mambo gani ni ya ki-dola na mambo gani ni ya ki- serikali.

Angalia hata masuala ya kuingiza nchi kwenye vita, pamoja na kuwa ni ya ki-dola moja kwa moja, bado rais analijulisha bunge kwani ultimately ndilo litatunga sheria ya mtumiza ya fedha za kupigana vita hivyo!

Nadhani hapa anapalilia kuwa spika - nasikia amechukua fomu!
 
Hata kama hamtaki, au kwavile mnapenda kuingiza siasa kwenye kila jambo, hapa nitarudia tena!

Kama hoja yako ni kutokana na issue ya Samia vs Ndugai, pale HAKUNA MHIMI ULIONGILIWA...

Ndugai sio MHIMILI kama mnavyojaribu kuaminishana bali BUNGE NDIO MHIMILI.

Mbunge anapoongea au kufanya kazi ya Kibunge NDANI YA BUNGE, ndipo anakuwa amefanya au kusema kwa niaba ya Mhimili!! Na anaposema kwa niaba ya Mhimili, hapo ukimwingilia au kum-challenge ndo utakuwa unau-challenge Mhimili kwa sababu, ingawaje Mhimili ni Bunge na sio Mbunge lakini bado Bunge haliwezi kuwa Bunge bila Wabunge!!

Ni kutokana na hilo, ndo maana Ibara ya 100(2) ya Katiba yetu inasema:
Bila ya kuahiri Katiba hii au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, Mbunge yeyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kutokana na jambo lolote alilolisema au kulifanya ndani ya Bunge au alilolileta Bungeni kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo.
Hapo utaona wazi kwamba, Comfort Zone kwa Mbunge ni Ndani ya Bunge! Akiwa ndani ya Bunge anakuwa anafanya kazi ya kibunge kwa niaba ya Bunge ambalo ndilo Mhimili!

Nje ya hapo, kama ilivyotokea kwa Ndugai, Mbunge/Spika au Ndugai mwenyewe atakuwa analindwa na Ibara ya 18(1) ambayo inazungumzia Uhuru wa Kutoa Maoni kwamba:-
Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.
Kwahiyo Samia angeweza kuhukumiwa kwa kuingilia Uhuru wa Kutoa Maoni na sio kuingilia Mhimili kwa sababu Ndugai kaongea aliyoongea akiwa na watu wa jamii yake kwenye mambo yao!

Hata hivyo, kumhukumu Samia kwamba ameingilia uhuru wa kutoa maoni inabidi utoe ushahidi kwamba Samia aliagiza Ndugai akamatwe au ajiuzulu!!

Kinyume chake, nilichokiona kwa Samia ni kile kile alichofanya Ndugai! Ndugai katumia uhuru wake wa kutoa maoni kumshangaa Samia na Samia nae akatoa uhuru wake wa maoni kumshangaa Ndugai!

Kama Ndugai ana uhuru wa kutoa maoni na kumshangaa Samia na mambo yake ya kukopa kopa, kwanini Samia nae asiwe na uhuru wa kutoa maoni na kumshangaa Ndugai kupinga hadharani jambo ambalo ameshiriki kupitisha?

Kama tunaamini Rais ameingilia Mhimili, kwanini Spika nae asionekane ameingilia mhimili mwingine?!

Hilo la kumshangaa Ndugai ndio linatufikisha kwenye kitu kinaitwa Collective Responsibility! Tuache ushabiki, Ndugai amekiuka misingi ya Collective Responsibility ya uongozi!!

Ibara ya 62(1) inasema Bunge litakuwa na sehemu mbili, yaani Rais na Wabunge! Kwa maana nyingine, SSH nae ni sehemu ya Bunge! Na kifungu kidogo cha 3 cha ibara husika kinasema:-
Iwapo jambo lolote lahitaji kuamuliwa au kutekelezwa na sehemu zote mbili za Bunge kwa mujibu wa masharti ya Katika hii au masharti ya sheria nyingine yoyote, basi jambo hilo halitahesabiwa kuwa limeamuliwa au limetekelezwa ipasavyo ila mpaka liwe limeamuliwa au limetekelezwa na Wabunge na vile vile na Rais, kwa mujibu wa madaraka yao kuhusu jambo hilo
Utaona hapo, jambo lolote halitahesabiwa kwamba limeamuliwa ipasavyo hadi limeamuliwa na Wabunge na vilevile Rais kwa sababu kama tulivyoona hapo juu, Rais na mwenyewe ni sehemu ya bunge.

Utaratibu ni kwamba, wakati wa Bunge la Bajeti ukifika, Waziri wa Fedha ataenda bungeni kusoma bajeti ya Makadario ya Mapato na Matumizi! Kwavile hata baada ya miaka 60 ya uhuru bado tunakuwa na budget deficit, katika soma yake ya bajeti hatimae Waziri atafikia sehemu kama hii:-

Mikopo.png

Na akishamaliza kusoma, waziri atatoa hoja na wakati ukifika, Wabunge wataijadili hotuba ya waziri na mwisho wa yote, Spika atawauliza wabunge wanaoikubali bajeti wasema ndiyo na wanaoipinga waseme sio!

Sasa kama tujuavyo wabunge wetu, ikishafika hapo itakuwa NDIYOOOOOOOOOOOO!! Kwa maana nyingine, Taasisi inayoongozwa na Spika, yaani Bunge, ambalo ndilo Mhimili, hatimae linamkubalia Waziri wa Fedha pamoja na mambo mengine, AKAKOPE PESA NJE!!

Sasa hapo ndipo inakuja dhana ya Collective Responsibility! Linapokuja suala la collective responsibility, kama jambo hukubaliani nalo unatakiwa kujiuzulu ili hatimae uwe na uhuru wa kuzungumza ni kwanini hakubaliani nalo!!

Na kwavile hapa tunazungumzia Spika/Mbunge, wala hakuwa na sababu ya kujiuzulu ulu ateme nyongo kwa sababu tayari Ibara ya 100(2) inampa uhuru wa kuongea chochote ndani ya bunge bila kuingiliwa na bila ya kuingiliwa na mamlaka yoyote provided analoongea lisiwe linakiuka sheria zingine!!

Sasa kama taasisi anayoongoza Ndugai ilishakubaliana na kupitisha bajeti iliyotaja suala la kukopa, huwezi tena kutoka nje na kuponda jambo lile lile uliloshiriki kuidhinisha, tena mara nyingi kwa mbwembwe na tambo!!!

Tena afadhali angekuwa mbunge wa kawaida, lakini Spika!! Tena Spika aliyepata uspika kwa mgongo wa chama kile kile!!
 
Hata kama hamtaki, au kwavile mnapenda kuingiza siasa kwenye kila jambo, hapa nitarudia tena!

Kama hoja yako ni kutokana na issue ya Samia vs Ndugai, pale HAKUNA MHIMI ULIONGILIWA...

Ndugai sio MHIMILI kama mnavyojaribu kuaminishana bali BUNGE NDIO MHIMILI.

Mbunge anapoongea au kufanya kazi ya Kibunge NDANI YA BUNGE, ndipo anakuwa amefanya au kusema kwa niaba ya Mhimili!! Na anaposema kwa niaba ya Mhimili, hapo ukimwingilia au kum-challenge ndo utakuwa unau-challenge Mhimili kwa sababu, ingawaje Mhimili ni Bunge na sio Mbunge lakini bado Bunge haliwezi kuwa Bunge bila Wabunge!!

Ni kutokana na hilo, ndo maana Ibara ya 100(2) ya Katiba yetu inasema:

Hapo utaona wazi kwamba, Comfort Zone kwa Mbunge ni Ndani ya Bunge! Akiwa ndani ya Bunge anakuwa anafanya kazi ya kibunge kwa niaba ya Bunge ambalo ndilo Mhimili!

Nje ya hapo, kama ilivyotokea kwa Ndugai, Mbunge/Spika au Ndugai mwenyewe atakuwa analindwa na Ibara ya 18(1) ambayo inazungumzia Uhuru wa Kutoa Maoni kwamba:-

Kwahiyo Samia angeweza kuhukumiwa kwa kuingilia Uhuru wa Kutoa Maoni na sio kuingilia Mhimili kwa sababu Ndugai kaongea aliyoongea akiwa na watu wa jamii yake kwenye mambo yao!

Hata hivyo, kumhukumu Samia kwamba ameingilia uhuru wa kutoa maoni inabidi utoe ushahidi kwamba Samia aliagiza Ndugai akamatwe au ajiuzulu!!

Kinyume chake, nilichokiona kwa Samia ni kile kile alichofanya Ndugai! Ndugai katumia uhuru wake wa kutoa maoni kumshangaa Samia na Samia nae akatoa uhuru wake wa maoni kumshangaa Ndugai!

Kama Ndugai ana uhuru wa kutoa maoni na kumshangaa Samia na mambo yake ya kukopa kopa, kwanini Samia nae asiwe na uhuru wa kutoa maoni na kumshangaa Ndugai kupinga hadharani jambo ambalo ameshiriki kupitisha?

Kama tunaamini Rais ameingilia Mhimili, kwanini Spika nae asionekane ameingilia mhimili mwingine?!

Hilo la kumshangaa Ndugai ndio linatufikisha kwenye kitu kinaitwa Collective Responsibility! Tuache ushabiki, Ndugai amekiuka misingi ya Collective Responsibility ya uongozi!!

Ibara ya 62(1) inasema Bunge litakuwa na sehemu mbili, yaani Rais na Wabunge! Kwa maana nyingine, SSH nae ni sehemu ya Bunge! Na kifungu kidogo cha 3 cha ibara husika kinasema:-

Utaona hapo, jambo lolote halitahesabiwa kwamba limeamuliwa ipasavyo hadi limeamuliwa na Wabunge na vilevile Rais kwa sababu kama tulivyoona hapo juu, Rais na mwenyewe ni sehemu ya bunge.

Utaratibu ni kwamba, wakati wa Bunge la Bajeti ukifika, Waziri wa Fedha ataenda bungeni kusoma bajeti ya Makadario ya Mapato na Matumizi! Kwavile hata baada ya miaka 60 ya uhuru bado tunakuwa na budget deficit, katika soma yake ya bajeti hatimae Waziri atafikia sehemu kama hii:-

View attachment 2076879
Na akishamaliza kusoma, waziri atatoa hoja na wakati ukifika, Wabunge wataijadili hotuba ya waziri na mwisho wa yote, Spika atawauliza wabunge wanaoikubali bajeti wasema ndiyo na wanaoipinga waseme sio!

Sasa kama tujuavyo wabunge wetu, ikishafika hapo itakuwa NDIYOOOOOOOOOOOO!! Kwa maana nyingine, Taasisi inayoongozwa na Spika, yaani Bunge, ambalo ndilo Mhimili, hatimae linamkubalia Waziri wa Fedha pamoja na mambo mengine, AKAKOPE PESA NJE!!

Sasa hapo ndipo inakuja dhana ya Collective Responsibility! Linapokuja suala la collective responsibility, kama jambo hukubaliani nalo unatakiwa kujiuzulu ili hatimae uwe na uhuru wa kuzungumza ni kwanini hakubaliani nalo!!

Na kwavile hapa tunazungumzia Spika/Mbunge, wala hakuwa na sababu ya kujiuzulu ulu ateme nyongo kwa sababu tayari Ibara ya 100(2) inampa uhuru wa kuongea chochote ndani ya bunge bila kuingiliwa na bila ya kuingiliwa na mamlaka yoyote provided analoongea lisiwe linakiuka sheria zingine!!

Sasa kama taasisi anayoongoza Ndugai ilishakubaliana na kupitisha bajeti iliyotaja suala la kukopa, huwezi tena kutoka nje na kuponda jambo lile lile uliloshiriki kuidhinisha, tena mara nyingi kwa mbwembwe na tambo!!!

Tena afadhali angekuwa mbunge wa kawaida, lakini Spika!! Tena Spika aliyepata uspika kwa mgongo wa chama kile kile!!
chige umejitahidi kudadavua.imenibidi nitulie kidogo ila kudigest bandiko lako na kwa kweli nimekuelewa vzr.congrats.
 
Jibu la swali lako juu ya mihimili mitatu ya Dola ni hili
6fef7902d4afd3d97d8dc37bbf2b6e70.png
 
Duniani kote kuna hii dhana ya mihimili ya mahakama, bunge na serikali kutokuingiliana (separation of powers) na kugawana madaraka bila kuathili mawasiliano kwa maana ya coordination baina yao kwa uendeshaji mzuri wa nchi. Ni kwa kiasi gani dhana hii inafanya kazi hapa kwetu?

Je kiuhalisia/in practice inawezekana kutenganisha mihimili hii isiingiliane kabisa na mambo yakaenda vizuri? Je kuna mifano ya Taifa lolote duniani lililofanikiwa kufanyia kazi dhana hii kwa mafanikio? Karibuni wataalam tujadili,
Doctrine ya separation of powers ipo very clear, lakini Nchi yetu imekumbatia mentality ya kijinga ya party supremacy. Hali hiyo inasababisha majaji wajione sehemu ya utekelezaji maagizo ya serikali katika judicial system, Rais anamuhukumu Mshitakiwa kabla ata kesi haijasikilizwa, kesi ya Mbowe ni mfano MZURI SANA,inge declare kauli ile ya Rais ni unconstitutional na kwamba itasababisha miscarriage of justice na hivyo kesi ya Mbowe ingefutwa. Bunge vilevile ambalo ni la chama kimoja,utakuta Bunge linaanzisha hoja ya kumpongeza Rais labda kwa kupata mkopo, yaani mambo ya kijinga sana. Mfano Naibu Spika anasema Rais yupo juu ya mihimili yote, nchi za wenzetu anatakia kujiuzulu kwa kukosa sifa ya kuwa kiongozi bungeni
 
Duniani kote kuna hii dhana ya mihimili ya mahakama, bunge na serikali kutokuingiliana (separation of powers) na kugawana madaraka bila kuathili mawasiliano kwa maana ya coordination baina yao kwa uendeshaji mzuri wa nchi. Ni kwa kiasi gani dhana hii inafanya kazi hapa kwetu?

Je, kiuhalisia/in practice inawezekana kutenganisha mihimili hii isiingiliane kabisa na mambo yakaenda vizuri? Je kuna mifano ya Taifa lolote duniani lililofanikiwa kufanyia kazi dhana hii kwa mafanikio? Karibuni wataalam tujadili.
Dhana ya mihimili kutokuingiliana sio sahihi,Hakuna namna mihimili inaweza kufanya kazi bila kuingiliana. Dhana kuu ya mihimili mitatu katika demokrasia ni "checks and balances" au mihimili kudhibitiana, zaidi sana ni kuzuia dola kupitiliza katika mamlaka yake "Government overeach" , mihimili ya bunge na mahakama huwa haina matatizo makubwa ya kuingilia na kubinya uhuru wa watu kinyume na haki za asili , sheria na taratibu.
 
Mbona iko wazi kabisa,Kuna mhimili uliojishindilia zaidi.......in jeipiemu voice
 
Back
Top Bottom