Naamini mpenz anapatikana sehemu yoyote iwe kanisani ,mtandaoni,msikitini,kazini ,chuo etc ni vile kujitambua wewe mwenyewe nini unataka na kuwa makini,nina rafiki yangu wa kike alikutana na mwanaume fb na hawakuwa wanajuana yule mwanaume alikuwa anakaa nje ya tz,walianza kuchat kama marafiki then yule kaka akamwambia ametokea kumpenda yule dada japokuwa walionana kwenye picha tu na kuongea kwenye simu,wakakubaliana kuwa wapenzi na yule kaka atakuja tz ili wajuane vizuri na wazazi wao watambue uhusiano wao,baada ya kudate kwa miez mitatu kwa simu na sms yule rafiki yangu akatumiwa ujumbe na mwanamke mwingine kuwa huyo mwanaume anayewasiliana nae kila saa yeye anaishi naye,yuel dada akamuuliza yule kaka naye akakubali akasema na aligombana naye kwa sababu hiyo na yeye akasema kweli mimi nipo tayari kumuacha kwa sababu nahisi kuwa nakupenda sana japokuwa hawajawah kuonana naye ila nakupenda zaidi kushinda huyu ninayemjua,wakamua kuendelea kwa masharti kwamba kila mtu awe free kumpigia mwenzake simu saa yoyote hata usiku wa manane,wakaendelea hivyo kwa miezi 8 kila dk mawasiliano yule kaka akaja Tz na wakaendelea vizuri na mwezi wa 9 wanafunga ndoa yao.