Diamond aachia kionjo Cha wimbo wake

Diamond aachia kionjo Cha wimbo wake

Msanii wa Kimataifa kutoka Tanzania Diamond Platnumz a.k.a baba lao wakati akiwa insta live akiwasiliana na mashabiki wake wa nchi tofauti tofauti ikiwemo kujibu maswali ya mashabiki wake akaamua kutoa kionjo Cha Baadhi ya mashairi ya moja ya wimbo wake ambao upo kwenye stoo ya nyimbo zake.

Kama ajatoa hiko kionjo akasema hii ngoma ni maalumu kwa Tanzania na East Africa sio ya international ni wimbo ambao ni una mashairi Sana ni wimbo wa taratibu alafu unaweza kusikiliza kwa muda mrefu bila kuuchoka kutokana na ufundi nilioutumia kuandika, Melody nzuri pamoja na production iliyotumika.Baadhi ya mashairi ya hiyo kionjo ni Kama ifuatavyo

"Si ugoko si kandambili,yaani vyote havikupendezi"
"Mwana ngoko usionawili,yaani tope usionautelezi"
"Utaishia kututabili,tubomoke inapita miezi"

"Ona umekosa nuru bahati huna,unaitwa kunguru ukifika wananuna
"Ndondondo mwanachururu asiyekuchuna,mengine nisikufuru"
Mkuu vipi nasikia huko karantini masaki kimeumana!
 
Habari za hivi huwezi kupewa
Salam SK yupo ICU
pia wasaidizi wawili wa Diamond wamekimbizwa Mloganzila hali ni mbaya ndiyomaana huoni tena zile video zakuimba wakiwa karantini Masaki.
Mungu awape afya njema wagonjwa wote.
 
Vipi mkuu mtu aliyepo icu anaruhusiwa kutumia simu??

Kwa sababu kama niliona post ya sallam dk 20 zilizopita
Salam SK yupo ICU
pia wasaidizi wawili wa Diamond wamekimbizwa Mloganzila hali ni mbaya ndiyomaana huoni tena zile video zakuimba wakiwa karantini Masaki.
Mungu awape afya njema wagonjwa wote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom