Diamond alalamika baada ya show yake Ujerumani kuvurugika

Diamond alalamika baada ya show yake Ujerumani kuvurugika

fungi

JF-Expert Member
Joined
Mar 18, 2014
Posts
2,539
Reaction score
4,672
Kiukweli nimesikitishwa sana na uandaaji wa kampuni hii ya BRITTS EVENTS iliyoandaa show ya Stuttgart Germany.

Kinachoniuma na kunisikitisha zaidi ni jinsi watu walivyoamua kujitolea kuja kutusupport vijana wao kwa wingi, halafu mwisho wa s
iku promoter anatupeleka wasanii kwenye show saa kumi alfajiri.

Najua ni kiasi gani mmeumia na kuwa disappointed, Lakini naomba mtambue kuwa halikuwa ni kosa langu, coz mimi ni mgeni tu, na nafata maelekezo ya promoter, hivyo nisingeweza kujiamulia kuja muda ninaoutaka mimi.

Haya ndio madhara ya ndugu zetu Mapromoter wa nje kutotaka kuamini na kukubali kuwa mziki wa East Africa sasa umekuwa, mwisho wa siku wanaandaa show kwenye venue ndogo halafu watu wanajaa hadi wanakosa pa kusimama na kuwabidi wapande kwa stage walau wapate pa kupumua.



10645180_792957570726059_971533261137472193_n.jpg


====================================================================


Watu kadhaa wamejeruhiwa mjini Stuttgart baada ya kutokea vurugu zilizotokana na kushindwa kufanya onyesho lake la Jumamosi ya Agosti 30, mwanamzuki wa muziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania, Nassib Abdul maarufu kama Diamond Platnum. Mwamamuziki huyo aliefika katika ukumbi alfajiri ya kuamkia Jumapili aliokolewa na polisi kutoka katika mikono ya mashabiki wenye hasira. Onyesho hili liliandaliwa na kampuni ya Kinaijeria iitwayo Brotes Events kwa kushirikiana na watanzania kadhaa wa hapa Ujerumani.

Chanzo: DW
=============================================




Diamond-Platnumz-Stuttgart.jpg

Gari ya Polisi iliyoibuka kumuokoa Diamond kufuatia sakata la mashabiki wake kupandwa na jazba







Sehemu ya ukumbi ulioharibiwa vibaya na washabiki mjini stuttgart,ujerumani

Stuttgart,Ujerumani,

Usiku wa Jumamosi ya Tarehe 30.Augost 2014, majira ya saa 10 alfajiri Mwanamuziki nyota wa Bongo Flaver Nasib Abdul aka Diamond Platnumz alijikuta katika hali ya hatari hadi kuokolewa na Polisi mjini Stuttgart,ujerumani,baada ya washabiki waliokuwa na hasira kuchoka kusubiri show,washabiki hao waliokuwa wamelipa ticket euro 25 kwa kiingilio waliahidiwa kuwa show ingeanza saa 4.00 usiku,lakini walijikuta wakisubiri hadi majira ya saa10 usiku au alfajiri ndipo mwanamuziki Diamond alipoletwa jukwaani na promota wake raia wa Nigeria anajiita kama Britts Event.

Hapo ndipo washabiki walipoona kuwa hawakutendewa haki walianza kurusha chupa na kutaka kumvamia mwanamuziki Diamond na promota wake,Kilichowakera zaidi washabiki ni pamoja na vyombo vibovu vilivyofungwa katika ukumbi huo kitu ambacho kiliwafanya washabiki kuvunja hadi vyombo vya muziki ma-Djs walishambuliwa na wapo Hosptalini kwa sasa.

Mmoja wa Djs hao alipoteza Lap top yake ,mwanadada DJ Flor alipatwa shock mshtuko wa moyo na kukimbizwa hosptali, washabiki hao walimpa kipigo DJ Drazee naye yupo hoi hospatal.

Polisi nchini ujerumani wanamesema tukio hili la aibu halijawahi kutokea,kuwa msanii kuchelewa kufika jukwaani kwa ujerumani ni kitu cha hatari kwani washabiki wa ujerumani wanaheshimu sana muda wao.

Mpaka sasa polisi wanamsaka mwandaaji wa onyesho hilo na wamesema kuwa wanachunguza thamani ya hasara hiliyosababishwa na ghasia hizo na pia itamfungulia mashataka promoter huyo raia wa Nigeria,ambaye pia anachunguzwa kwa kusemekana anajihusisha na mtandao fulani wa biashara.

Magazeti ya Stuttgart; yameandika "Washabiki wa hasira nawe DIAMOND"

source:stuttgarter-nachrichten.de



my take: Muda ni kitu Muhimu
 
Asante kwa taarifa..........lakini wala hakuna jipya kuchelewa kwenye show zake huyo kijana ndio zake,sijui ndio anaingia kwa mananzil....asiwachoshe wenzie...........
 
Diamond kwa level zake na mameneja kibao hawajui hata ratiba ya show? Unakwendaje kwenye show bila kujua ratiba? Alafu swala la muda ni kazi ya meneja kuhakikisha promota anaheshimu mkataba ambao muda ni sehemu yake.Yaani msanii mkubwa na meneja wako mnakaa tu hadi alfajiri ndio mnapelekwa ukumbini na nyie mnakwenda kama kuku tu.Diamond anastahili lawama na siku nyingine atambue lawama za msanii kuchelewa inaharibu zaidi jina la msanii si promota hivyo anapaswa kuhakikisha swala la promota kuheshimu muda linakuwa sehemu ya mkataba.
 
Hamna msanii hapa kazi kubana pua tu.ngoma ali kiba

Ameshaanza kutapatapa kuona mwenzie anafunika kwenye fiesta mikoani,yeye ile kill music ya kwao kigoma naskia aliwaboa watu pia
 
Pole ake mwaya
Ila shoo morning hyo kitu maajabu jaman ila hakuambiwa muda anaofanya shoo mapema maana izi kama komedy
 
huko hamna wazungu? naona ngozi nyeusi tu, halafu mbona ka grosary vile!

Wajerumani huwezi wakuta kwenye Show za vichochoroni, ukowakuta ni wale wala ndumu wanaokwenda kwa matazamio ya kupata ndumu toka kwa mablack... Dai awe makini, maana kila black Europe ni promoter, wana njaa hata fisi hafai. Mara nyingi wanawachelewesha wasanii ili wauze walau vinywaji kwanza.. Life tight jamaa
 
suala ni kuwa ameona kapiga show uchochoron na kajuwa pics zitafika tz kaamua kujiwah et ukumbi hautosh
 
suala ni kuwa ameona kapiga show uchochoron na kajuwa pics zitafika tz kaamua kujiwah et ukumbi hautosh

Ha ha ha ha my ribs ile hapo padogo kama sebuleni mbona bora za fiesta unakuwa huru sasa msanii ana perfom huku watu wamemzingira wengi
 
Back
Top Bottom