Diamond anatumbuiza ufunguzi AFCON, vyombo vyetu vya habari kimyaa

Diamond anatumbuiza ufunguzi AFCON, vyombo vyetu vya habari kimyaa

Clouds walitangaza mbona toka last week?? Mtusamehe, wabongo kwa sasa tusharogwa na Darassa mtoa post nawe usijinyime weka Muziki uburudike mambo mengine Mbele kwa Mbele.
 
Utadhani hili ni jambo la kawaida kwa msanii kutoka ardhi ya Tanzania akapewa heshima ya kutumbuiza uzinduzi wa mashindano makubwa kuliko yote Africa.

Diamond ameipa heshima Tanzania kwa kuwa msanii wa kwanza na pengine asitokee mwingine kutumbuiza uzinduzi wa mashindano ya AFCON. Lakini vyombo vyetu vya habari kimyaa kama hichi kitu ni cha kawaida. Sio blogs sio magazeti sio radio sio Tvs.

Wazalendo wa nchi hii tulitegemea hii habari iwe kubwa ili kuinspire hata wasanii wengine na vijana kwa ujumla. Lakini chuki roho mbaya majungu uswahili na utimu unatusumbua na kuturudisha nyuma wabongo.

Ndio maana Mrisho mpoto aliamua akaiwakilishe Kenya maana sisi wabongo buana!
Ni chombo kipi cha habari ambacho wewe ulitaka kilipoti maana hapa jamii forums ni chombo cha habari wewe umetoa na mimi ninesikia
 
Subiri afe wiki nzima redio na TV zitamsifu na kumwelezea alivyo msanii bora kutokea Tanzania

Nawaza kwa sauti
 
kutumbuiza tu imekuwa kelele,msomali KNAAN alitengeza waving flag iliyokuwa official song ya world cup lakini huko mogadishu hakukuwa na makelele kama haya tupunguzeni ushamba,maana tungekuwa na mtu kama wanyama anacheza ligi kuu ya uingereza sijui ingekuwaje ndo maana tunashangilia kina ajib wanaoenda kufanya majariubio team ya ligi daraja la kwanza misri wala haipo ligi kuu,tupunguze ushamba mara moja moja tuchukulie ni kawaida tu..kha
 
nimependa yule allan kingdom aliyefanya nyimbo na kanye west kaja hapa majuzi kimyakimya kusalimia upande wa mama hakuna mbwembwe za kipuuzi
 
duu kwa hiyo vyombo vya habari vyote hawampendi daimond?
 
Back
Top Bottom