Diamond azindua Pafyum yake ya Chibu, bei yake ni balaa

Ila jamani mbona laki kwa perfume/manukato (original) ni bei ya kawaida.Mnamuonea bwanamdogo.hizo perfume na bodyspray za bei nafuu tunazouziwa mtaani nyingi ni feki jamani huwezi uziwa spray ya nivea OG kwa alfu tano,kwa pesa hyo hupati hata deodorant OG. mavipodozi ya bei rahisi asilimia kubwa ni feki na mjiandae kwa kansa.
 

Mwandishi yupo sahihi..angebuni bidhaa ya buku tano tano.angepiga sana..lkn perfume halaf jiwe?..labda kalenga kumuuzia zari
 
Msanii asiyeishiwa ujuzi amekuja na jipya. msanii wa bongo flava diamond platnumz sasa azindua pafyumu yake. bei si ya kitoto. aitangaza kwa mbwembwe
 
Hahahaa daaah kwa bajeti hizi ni hatari tupu hapo hujahesabu na chumba cha kupanga ili ulale kumaliza siku yako
 
Pafyumu yenyew ina jina gumu kama dawa ya chango et 150 nitest dawa ya chango sijalogwa[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Mwambie atengeneze ata Boflo tule co pafyumu upake ujikute unanukia kama Fenesi[emoji14] [emoji14] [emoji14]
 
Mmmh... hapa sina la kusema ngoja nisubiri ya kiba huenda yeye akatujali mashabiki wake akapoza bei kdg

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
Hivi kwani ni lazima nae kiba atoe yake?mbona biashara nyingi tu?ubunifu mwingine utamsaidia kuteka soko lake kiba sio lazima huko alikoenda mwenzake
 
Hii pafum ni nzuri sana nimenunua Leo inarufu nzuri Na inaonekana inakaa mwilini vizuri haimsumbui hats yule aliekaa jirani yako kama ile kursumu ya kariakoo

Kursumu perfume [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Duh bei kubwa. Lipstic elfu 20 zikatushinda kununua sembuse pafyum ya laki na kitu aiseeee
 
Yaleyale ya Lipstick 50000
 
km huna helà tùlia wacha povu
 
Sio jambo baya, ila bei kubwa sana hii itapelekea wateja kua wachache, uhalisia ni kwamba Chibu ana mashabiki wengi wa hali zote ila kundi kubwa ni akina sisi wa mlo mmoja sasa ni vigumu kutumia laki moja kununua perfume.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…