Diamond fata ushauri huu mapema or else!

kuna mtu anaitwa cassim mganga, jamaa anajua sana, tena sana ila ndo hivyo tena....Diamond kama anaweza akaushe apige mzigo tuu, alafu lingine ni kwamba mimi si shabiki wake na haitokuja kutokea, lakini ktk mafanikio namuunga mkono anajua kazi inatakiwa iwe vipi, kuhusu mziki wake kwa kweli siupendi, sababu simuelewi anaimba nini, karibia nyimbo tatu za mwisho naona anazalilisha tu wanawake na kulamba lamba lile @#$_&+ hamna lingine, kila la kher diamond ila usiwatukane wenzako, umeshasahau maisha ya kimara na Tandale?
 
Mleta Uzi umeongea maneno mengi ya msingi na ya kumjenga msanii wetu Diamond ambaye kwa sasa ndio mwenye mafanikio zaidi kimuziki hapa nyumbani.

Lakini kuna mambo kadhaa umesahau kumshauri.Kwanza ,tungo za msanii huyu zimeanza kuwa na matusi sana hususani wimbo wa Salome.Asipo liangalia hili ataanguka.

Pili ,Asipende kujizifia sana kuhusu mafanikio yake na kutoa kauri za dharua kwa wale anaowazidi.Hili litamwangusha.

Cha mwisho , nachukua nafasi hii kukukosoa wewe mleta uzi kwa kauri yako eti Diamond ndiye aliyemrudisha/mpandisha Ali Kiba,hapo umepuyanga mbaya kabisa.

Ali Kiba ni msanii mwenye uwezo mkubwa sana wa kuimba huyo Diamond akasome.Diamond anajua biashara ya muziki +bahati/kupendwa lakini music wise Kiba ni Babaake.

Ali Kiba amejirudisha mwenyewe kimusiki huku akisapotiwa na mashabiki wake na bila kutafuta collaboration na wasanii wa nje kajulikana na kufanya vizuri hapa Afrika hususani mwaka huu.Katika mwaka huu kawa nominated kwenye tuzo za kimataifa zaidi ya nane na kushinda kadhaa.Sasa huko nako Diamond kamsaidiaje??

Ni hayo tu.

TeamTanzania
 
Kaka umeajaribu kujitetea apo mwishoni kuwa ww ni team Tanzania lkn katika bandiko lako inaoneaha kabisa ww una ushabiki fulani iv kwa sababu umejaribu kumpamba mmoja kwa sifa kedekede mara cjui hajafanya kolabo na kapata nomination kibao ile na sauti sol ilikuwa nn.....kama haimuhusu kwa nn aliipaform kwny tuzo za mtv-mama kila msanii na njia zake
 
Umeongea kiume

Diamond ni zaidi ya brand ya kitanzania, he is an African child

Aachane na makandokando, his humbleness ndio ilimfanya akamzidi Davido kirahisi sana when Davido started those tantrums, sasa naona na yeye anaenda kulekule kulikomwangusha Davido (Majigambo)

He also needs to go back to melodies, hizi marimba style za kinaijeria zinamfanya asiwe anavutia and easy to forget his songs
 
Yah word enzi za ukimuona, lala salama, mawazo, ntarejea, kesho that music was awesome hata my number 1 ilikuwa bado ya kitz.
Hizi unanimalizaga, sijui nini hazidumu yani baada ya mwezi hutaki hata kuusikia tena.
Mimi mpaka leo ukimuona iko kwa my play list songs...
 
kaingia mkenge wa quantity badala ya quality

Ukiangalia stars waliodumu sana africa kama akina youssou ndou, kofi olomide, franco, makeba, mutukudzi, salif keita, etc walibaki na identity ya muziki wao... si lazima kutoa wimbo kila wiki ili kuwa a mega star

Vilevile jamaa amebadili image, ile humble yake inapotea siku hadi siku na sasa ameanza kuwa mtu mtu wa kashfa na matusi kwa waliokosa... Even his image inabadilika, hata zile descent look imeanza kupewa extension ya manywele ya ajabu ajabu

Chibu is our star, arudi kwenye kioo na arudi kwenye origino...
 
Sure huu mziki wa kinaija anaofanya sasa haudumu masikioni mwa watu ila tu watu wanasubiri tu kuona video na dancing movies labda.
Baada ya mwezi over.
Na video sasa zinafanana na hii almost ni kwa wote I think wabadili ma director maana video lazima kuwe na sofa jeupe ama magari yamepaki wao wana dnce mbele, hotelin kitanda chenye shuka nyeupe, hotel kali.
Juzi nilikuwa natazama wimbo wa brick and lace wa love is wicked yani ile video ni so simple location kama frem za maduka za uswaz tu lakini hata ukiitazama leo video bado iko poa wakati imetoka nadhan 2008.
I think inabidi arudi kwenye his roots, seriously aache kuwa arogant AY nadhani ni kati ya wasanii wanaopendwa sana kwakuwa uwa ni mkimya..
 
Absolutely

I hope washauri wake wanasoma haya mawazo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…