Diamond hana washauri?

Diamond hana washauri?

mama duamond alizaliwa ndani ya ndoa basi anao wajibu kidini kumuangalia baba yake bt kama ni mwanaharamu(mtoto wa njee ya ndoa) basi mzee hana haki n haki inabakia kwa mama tuu
 
Kwa mtu yoyote ambaye amelelewa kwenye familia yenye wazazi wawili ambayo baba anatimiza wajibu wake ipasavyo.....

Katika familia ambayo asilimia tisini ya mafanikio yako yametokana na juhudi za wazazi wote wawili kwa kila mmoja kutimiza wajibu wake huwezi kumuelewa huyo kijana diamond.....au huwezi kuhisi vile anavyohisi anavyomuona baba yake......

Ila kama umezaliwa kwenye familia ambayo mama yako pekee anatakiwa adamke alfajiri kwenda kutafuta vibarua ambavyo muda mwingine ni za kumdhalilisha ilimradi tu wewe kijana uweze...kula vizuri ,kuvaa vizuri , kulala pazuri na hatimaye kupata elimu nzuri....
Katika familia ambayo kilele cha mafanikio yako yametokana mahangaiko ya mama yako kipenzi aliyelazimika kubeba majukumu ya watu wawili na kufanikiwa kukufikisha hapo.....unamuelewa vyema Daimond na unaelewa vile ambavyo yeye anahisi pindi aionapo sura ya baba yake......

Nina wakumbusha wanaume wenzangu kuwa kuitwa baba hakuishiii tu kwenye kumpa mimba mwanamke bali kwenye kutimiza majukumu yake kama mzazi ambaye kwa namna moja au nyingine anahusika na upatikanaji wa mimba hiyo.....
 
Kama hujawahi kutelekezwa na mzazi huenda ukaona Diamond anamakosa. Lakini kwa waliowahi wanajua uchungu wake. Kuna wakati mtoto anakosa hata hela ya percetamol lakini utasikia baba anahama bar na kuoa kila siku. Hivi baba huyu nae utapewa lawama baadae?

Kwa bahati nzuri, mzazi ambaye hakukulea, hakukujali, alikukana, alikuacha bila kujua utaishije, Hawezi kukupa LAANA abadani. Na hapa ndio maajabu ya Mungu yanapojionyesha.

Lakini pia kuna wakati wazazi wa namna hii wakabaki kua kama somo kwa akina baba wengine.
 
Fikiri tena, ukimaliza kufiri nakuomba ufikiri tena, nasema rudia tena kufiri, nakutaka ufikiri zaidi ya kufiri ulikofikiri,

Maneno yote aliyoyaandika mleta post hapo na kumuongoza mwenzako hasa kwa maandiko ya ki Imani ya DINI yake bado unafikiri hovyo hivyo ?

Kama umeshundwa kufikiri kwa muda huu pumzika na unywe maji maana hata swaumu...huna,

Na ukishindwa kufiri tafuta mtu akusaidie kufikiri ili ukiri kwamba ulikariri bila kufiri.
Nawe ungeamua kufikiri basi ungeiona mantiki ya muuliza swali! Je, mtoto ni Diamond peke yake? Jibu HAPANA... mwingine anayefahamika ni Queen Darleen! Je; Queen Darleen anamsaidia baba ake? Kama ndiyo ni kwanini hatumuoni Mzee Abdul akitumia magazeti ya udaku kama kawaida yake akionesha kumshukuru mwanae?! Au nae hamsaidii?! Kama nae hamsaidii ni kwanini hatuoni magazeti ya Shigongo yakiandika habari za Queen Darleen kutomsaidia baba ake?!

One more thing! Hivi ni kwanini issue zote zihusishe magazeti ya udaku? Unataka kusema celebrities wote wa Kibongo wanawajali wazazi wao? Mbona hatuwaoni hao wazee wakilalamika kwenye magazeti ya udaku?

February mwaka huu, magazeti hayo hayo ya Shigongo yaliandika habari za Mzee Abdul kwenda studio ya Diamond!
Screenshot_2016-06-23-13-39-41.png

Screenshot_2016-06-23-13-39-52.png

Screenshot_2016-06-23-13-40-29.png


Haya sasa nisaidie wewe! Global Publishers walijuaje kwamba Mzee Abdul alitaka kwenda Studio kwa Diamond hadi wakafanikiwa kupiga picha zote hizo not mentioning vile walivyofahamu kwamba anaenda hospital hadi wakafanikiwa kuwahi na kupiga picha akiwa bado mapokezi!!!

Ukiamua kufikiri hutachelewa kuona kwamba huyu Mzee anatumika na Shigongo kuuza magazeti yake ndio maana Diamond ana-keep distance na huyu mzee! Ingawaje mimi co Mungu but trust me; Diamond akishajiweka close na huyu mzee atakuja kujuta!
 
Mnao mlaumu Diamond hamjapitia aliopitia ,ndio sio vizuri anavofanya but muacheni mungu ndie hakimu nyie wenyewe mna dhambi ngapi ambazo hatuzijui
Fanyeni yenu waachieni mambo yao ya kifamilia
Wanaume ishini vizuri na wapendeni watoto wenu huwezi jua atakua nani baadae
Hata km umeachana na mama ake be there kwa ajili ya mtoto wako
Ndo kinachomtesa sasa hv baba Diamond anatafuta simphathy kwenye social media
hakuna dhambi yoyote hapo, mzazi ana wajibu kumlea na kumtunza mwanawe sasa kama kakataa , kwann yy atunzwe
 
kweli kabisa ilibidi amsamehe. kwani bila yeye diamond asingekuwepo. me naomba diamond amsamehe mshua. ampeleke hospital. mungu atamjalia zaidi na zaidi. rihanna nae alikuaga name bifu name baba yake ishu Kama hiyo lakini akamsamehe had I Leo mzee anakula bata maisha matamu
 
{وَقَضَى رَبُّكَ أَلاَّ تَعْبُدُواْ إِلاَّ إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَاناً إِمَّا يَبْلُغَنَّ عِندَكَ الْكِبَرَ أَحَدُهُمَا أَوْ كِلاَهُمَا فَلاَ تَقُل لَّهُمَا أُفٍّ وَلاَ تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلاً كَرِيماً* وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيراً}

وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ إِحْسَاناً

وَقَضَى رَبُّكَ أَلاَّ تَعْبُدُواْ إِلاَّ إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَاناً

وَاعْبُدُواْ اللّهَ وَلاَ تُشْرِكُواْ بِهِ شَيْئاً وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَاناً

برهما وحفظهما وصيانتهما وامتثال أوامرهما
باب تقديم بر الوالدين على التطوع بالصلاة وغيرها


Mimi nimeanza kupata wasiwasi kuona Al Qaeda wameingia humu JF, jamani tujihadhari sasa!
 
Anayejua baba wa mtoto ni MAMA pekeyake,inawezekana huyu ni baba wa bandia
 
Katika hili la mzazi wake wa kiume mimi binafsi limenigusa hasa kwa imani yangu ya dini. Siwezi kuhukumu moja kwa moja kwa maana sijui chanzo cha ugomvi wao wala status yao kwa sasa na pia MIMI SI HAKIMU, lakini nina haki ya kutoa maoni yangu hasa kumsaidia pia diamond ajitambue.

Katika hali ya kawaidia inatakiwa ingekuwa rahisi kama mzazi wako anapata msaada wako by then kila siku awe analalamika au tunamuona kwenye mitandao huo tayar ni udhaifu wako wewe mtoto kwa kuruhusu mzazi wako awe anakutia aibu wewe au familia yenu kwa ujumla. Kwa namna yoyote ni lazima suala la wazazi wako ukalipa umuhimu mkubwa sana katika maisha yako.

Katika mafundisho ya dini yanatufunza nini kuhusu wazazi?

Hakika ametakasika yule ambaye amewajibisha na kuamrisha wema na kutimiza haqqi na kuiegemeza kwa kila anaestahiki na akawajibisha haki kwa wazazi wawili, na ikawa ni amri iliyoenea kwa walimwengu wote. Hakika ameamrisha ALLAH tabaaraka wata’la katika aya nyingi kuwafanyia wema na ihsani wazazi wawili.
Mfano wa kauli yake aliposema:

{وَقَضَى رَبُّكَ أَلاَّ تَعْبُدُواْ إِلاَّ إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَاناً إِمَّا يَبْلُغَنَّ عِندَكَ الْكِبَرَ أَحَدُهُمَا أَوْ كِلاَهُمَا فَلاَ تَقُل لَّهُمَا أُفٍّ وَلاَ تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلاً كَرِيماً* وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيراً}
Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa hishima. Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma. Na useme: Mola wangu Mlezi! Warehemu kama walivyo nilea utotoni.


Akaamrisha ALLAH tabaaraka wata’la ihsani kwa wazazi wawili katika namna zote za wema, nao ni katika kauli [unapozungumza nao] pale aliposema [basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa hishima]. Vivyo hivyo kuwafanyia wema katika matendo; kimwili na kimali kwa kauli yake aliposema: (Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma).
Na akanyanyua ubora wanapofika katika hali ya uzee, kisha akakataza kuwavunjia adabu na kuwatusi, achilia mbali kuwaacha wakiteseka.
UWAJIBU WA KUWAFANYIA WEMA WAZAZI WAWILI.
Hakika ameamrisha Allah tabaaraka wata’la, na akawajibisha kwa njia ya wasia kuwafanyia wema wazazi wawili katika aya nyingi za qur’an. Pale ilipokuja amri ya wazi juu ya kuwatii, aliposema:
وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ إِحْسَاناً
Na tumemuusia mwanadamu awatendee wema wazazi wake wawili[1]

Ikaonesha wazi kuwa kuwafanyia wema wazazi wawili ni jambo la wajibu kwa kuwa ni wasia wa Allah kwetu. Bali akaliambatanisha jambo hilo la kuwafanyia wema wazazi wawili na twaa’ yake Allah tabaaraka wata’la pale aliposema:
وَقَضَى رَبُّكَ أَلاَّ تَعْبُدُواْ إِلاَّ إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَاناً
Na mola wako mlezi ameamrisha kuwa msimuabudie yeyote isipokuwa yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema.[2]

Na kauli yake aliposema:
وَاعْبُدُواْ اللّهَ وَلاَ تُشْرِكُواْ بِهِ شَيْئاً وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَاناً
Na mwabudieni Allah wala msimshirikishe na chochote, na muwafanyie wema wazazi wawili.[3]

Zikakusanya aya mbili hizi kuwa kufanyiwa wema wazazi wawili ni haqqi yao, bali akaifafanya haki hiyo kuwa ni ya pili baada ya tawheed yake Allah tabaaraka wata’la akionesha ukubwa wa jambo hilo [la kuwafanyia wema].
Amesema Al qurtwubiy [Allah amrehemu], kauli ya Allah “Na wazazi wawili kuwafanyia wema [ihsani]” maana yake ni:
برهما وحفظهما وصيانتهما وامتثال أوامرهما
Kuwafanyia wema na kuwahifadhi, kuwatunza na kutekeleza amri zao.

Katika kulisisitiza hilo, mpaka ikawa [wema kwa wazazi wawili] ni wenye kutangulizwa mbele hata kabla ya Sunnah za kujitolea kama vile Sunnah za kabla ya swala nk. Na kwa hili akaweka imamu muslim [Allah amrehemu] mlango katika swahih yake akiuita:
باب تقديم بر الوالدين على التطوع بالصلاة وغيرها

By the way mimi nimekubusha tu. Kama ni kweli mzazi hapati msaada basi ajitahidi kumsamehe, kama anapata msaada ila ndio umaarufu basi diamond anisemehe maana binadamu tumeumbwa kukusea. Na huu ni mwezi wa toba hakika atakuwa amenisamehe.
Asante.
Usituletee ujinga hapa, kwamba uislam ni dhaifu kiasi hiki, kwamba mwenye wajibu ni mtoto kwa Baba lakini Baba hawajibiki kwa lolote kwa mtoto ?????
 
Mimi nimeanza kupata wasiwasi kuona Al Qaeda wameingia humu JF, jamani tujihadhari sasa!
Hajui chochote kuhusu dini kajiandikia tu,kwanza kwa mujibu wa hiyo dini yake mtoto wa haramu (nje ya ndoa ) hawajibiki kwa lolote kwa Baba,angalau angeongelea kibinadamu angekuwa na pointi si dini. Mtoto wa haramu ni mali ya mama kwa mujibu wa hiyo dini yake na mtoto hapati dhawabu (malipo kwa mungu) kwa kumuhudumia huyo Baba, na hapati dhambi kwa kutomuhudumia. ( KUMBUKA MAMA DIAMOND NA HUYO BABA HAWAKUWA WAMEOANA)
 
Unainukuu Quran kwa mambo ya kipuuzi,halafu unakariri vifungu dhaifu ili wenye dini yao waione kuwa inamapungufu sana ili iweje, wabadili dini au .......... acha kuishirikisha dini kwa mambo ya kipuuzi.
 
Back
Top Bottom