Diamond kapoteza mvuto?

Mtazoea tu hii ni dunia ya tatu , mbona huko dunia ya kwanza watu wamezoea na wanatengeneza pesa humo humo , ni suala la muda tu
 
Wewe umpende mobetto afu ufanikiwe kila siku mogogoro mara kesi mala nini Diamond nyota ilipungua baada ya kuwa na mobetto
 
Mkuu sijakuelewa ni ipi hasa hoja yako ? Emu fafanua
Hizi drama , ni jambo la kawaida sana , mfano kim kardashian mpaka video yake ya ngono tuliiona, lakini umeona trump alimuita ikulu kwa heshima kubwa kabisa, wenzetu wanaheshimu haki za mtu mmoja mmoja muhimu afike miaka 18, uhuru wa mtu uheshimiwe , muhimu asivunje sheria za nchi
 
Ooh hapo nimekuelewa mkuu. Ila kwa bongo hiyo inakukosesha ma deal nk
 
Watanzania katika ubora wao kama wote!!
Hivi ninyi mtaisha lini kujadili ya wenzenu na mkafanya yenu ili mpige hatua ili ninyi pia tuwajue??
Katika safari ya mafanikio kuna fluctuations za kutosha tu yaani Leo waweza panda kesho ukashuka,it's life just get used to it!
Hata bahari hupwa na kujaa so binadamu ni nani yeye asipande na kushuka??
Mwacheni kijana wa watu aendelee kuipeperusha bendera ya Tanzania.
Ninyi mmeshindwa hata kufanya juhudi za kujulikana hapo mtaani kwenu maana hamna lolote la maana mlifanyalo chini ya jua!
Chakusikitisha zaidi wanaume wazima mmekalia umbeya kuliko wake zenu,shame upon you!!
 
mtoa post aje na data za Davido na Wizkid..sio porojo, tunataka ushahidi kama huu
 
Samahani ndugu lini aliwahi kuwazidi davido na wizkid?
 
Kuna mijitu inaakili za kimavimavi tu. Sasa kama unamsikiliza kiba utamsikilizaje Diamond. Mimi namsikiliza Diamond. Nyimbo zake zinachuja kwapani kwako labda
 
Kuna sehemu Mondi anakosea,either management yake au yeye mwenyewe,maisha binafisi nakuchanganya na kazi vitamfanya apoteze mvuto!!

Diamond karanga ndo zishatoka sokoni,ingawa sio zake 100%, Chibu perfume,sijui ziko wapi ingawa nazo sio zake 100%!! Wasafi tv and Radio pia tutakuja sikia sio zake 100%!!

Tukirudi kwenye matangazo hasa ya coys kubwa kubwa,voda na dstv ndo hana tena contract nao,kabakiza Coca Cola tu,napo sio sana!!

Tukumbuke EA kuna mtu alikua anapiga show za ndani na Nje kama Jose Chameleon wa Uganda??? Hadi kuitwa Dr Chameleon!! Lakini kwa sasa,kapoa sana!! Ingawa sijui,kama ana miradi mikubwa sana! Maisha yanabadilika sana,zamani kutoka tegeta hadi posta kulikua na billboard outdoors nyingi sana roads,but kwa sasa hakuna kabisa,watu wanahamia kwenye digital advert!!!
 
Naweza nikasema Diamond na ruge wote wanategemeana kila mmoja amethirika kibiashara mfano ruge mpaka sasa fiesta inakuja lakini haieleweki wasanii gani atawatumia kujaza show mana mtaani ndo kunaongea mda wote wanasikiliza nyimbo za wasafi pia diamond wasanii wake mboso na lavalava wameshindwa kukuwa pia kuna wadhamini wakubwa wanashindwa kufanya mikataba nae kutokana na redio kubwa kutofanya promo ya kazi za diamond
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…