Diamond Platinumz Fans' Special Thread: Njooni tukutane hapa

Matusi so maungwqna, chukizo kwa maulana.
Mwaitafuta laana, toka kwake ye rabana.
Itawagharimu sana, I tena bila maana.
Majirani tupendane, rai apewe mfalme.

Ukimtusi modereta , na kwa bani utatota.
Wala pole hutopata,masaibu kukukuta.
Na pia utajuta, wako ujinga kufuta.
Majirani tupendane, rai apewe mfalme.

Jukwaa la burudani, wala sio tafrani.
Hivi kwa sababu gani, taraghani kushamiri.
Acheni uhayawani, na matusi sio fani.
Majirani tupendane, rai apewe mfalme.

Mazigazi muungwana, na sio mjuaji sana .
Mpenda kuafikiana, kwa jambo lenye maana.
Mondi mutoto mubaya, na pia hanaga haya.
Majirani tupendane, rai apewe mfalme.
 

Asanteeeer Mazigazi
 
Last edited by a moderator:

Mkuu....vip naww kumbe ni mtunz mzur hiv....ile tuzo ya ktma ilikuwa inakuhusu hiv 😀😀😀
 

ahahahahaha we mtu nimekuvulia kofia khaaaa!!!sio kwa mashairi haya!!looh utadhani malenga wapya?
 

+Mondi mutoto mubaya, na pia hanaga haya.

+Majirani tupendane, rai apewe mfalme!

Hongera Mkuu kwa mashairi matamu
 
Diamond katisha sana uko instagram yaani asubuhi alikuwa na followers 809k imefika mchana ana followers 830k, yaani ndani ya masaa 4 kapata followes 20k, hadi mwenyewe anashangaa hawa watu wametoka wapi ghafla ivyo.

Ana ashki majinuni
 

my dear uliniita toka july 5...sorry niko busy na uchaguzi huku hadi week end kama hivi. Back to the theme: kulipa na kutolipa ni subjective. it all depend on how you define each varriable and how u operationalize (measure) them.
 
Jamani kwemaaa!!!!naonablowassa amevuruga utaratibu kabisa leo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…