Diamond Platnumz aahidi kuwafanyia kufuru wanatandale

Diamond Platnumz aahidi kuwafanyia kufuru wanatandale

Dong Jin

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2018
Posts
968
Reaction score
2,034
Katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa msanii wa muziki wa Bongo Fleva nchini Tanzania, Diamond Platnumz amewaahidi mambo yafuatayo wakazi wa Tandale (mahali alipozaliwa na kukulia)...

1. Kulipia BIMA ya Afya kwa watoto 300,na wakazi wengine 700 (Jumla watu 1000) ndani ya mwaka mmoja....

2. Kutoa mitaji kwa akina mama 200, ya shilingi za kitanzania 100,000/= mpaka 200,000/=

3. Kutoa Boda boda 20 kwa vijana wasio na ajira na kuwatengenezea aina fulani ya menejimenti ambapo kila siku kila kijana itampasa akabidhi sh. 10,000/= ambayo itatumika kununua bodaboda nyingine kwa ajili ya vijana wengine....

4. Kukarabati Shule zote za msingi zilizopo ndani ya Kata aliyozaliwa ya Tandale ikiwa ni pamoja na kuweka matank kwa ajili ya kuhifadhia maji...
maxresdefault.jpg
Diamond Platnumz
Diamond akiongea kwenye sherehe fupi iliyofanyika Live kupitia Wasafi TV, amesema kuwa siku ya Ijumaa Tarehe 5 Oktoba 2018 atatimiza ahadi hiyo ikiwa na pamoja kuchinja ng’ombe na kusherehekea na watu wake wa Tandale pamoja na wasanii wenzake, wageni mbalimbali kutoka serikalini na mashirika binafsi waliojitolea kumuunga mkono.
 
Katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa msanii wa muziki wa Bongo Fleva nchini Tanzania, Diamond Platnumz amewaahidi mambo yafuatayo wakazi wa Tandale (mahali alipozaliwa na kukulia)...

1. Kulipia BIMA ya Afya kwa watoto 300,na wakazi wengine 700 (Jumla watu 1000) ndani ya mwaka mmoja....

2. Kutoa mitaji kwa akina mama 200, ya shilingi za kitanzania 100,000/= mpaka 200,000/=

3. Kutoa Boda boda 20 kwa vijana wasio na ajira na kuwatengenezea aina fulani ya menejimenti ambapo kila siku kila kijana itampasa akabidhi sh. 10,000/= ambayo itatumika kununua bodaboda nyingine kwa ajili ya vijana wengine....

4. Kukarabati Shule zote za msingi zilizopo ndani ya Kata aliyozaliwa ya Tandale ikiwa ni pamoja na kuweka matank kwa ajili ya kuhifadhia maji...
maxresdefault.jpg
Diamond Platnumz
Diamond akiongea kwenye sherehe fupi iliyofanyika Live kupitia Wasafi TV, amesema kuwa siku ya Ijumaa Tarehe 5 Oktoba 2018 atatimiza ahadi hiyo ikiwa na pamoja kuchinja ng’ombe na kusherehekea na watu wake wa Tandale pamoja na wasanii wenzake, wageni mbalimbali kutoka serikalini na mashirika binafsi waliojitolea kumuunga mkono.
Ni Ngumu sana Kupitishwa kwenye kura za maoni ndani ya CCM labda aje UKAWA ndio atatimiza ndoto zake za kuwania Jimbo la Kinondoni.
 
Nzuri, ila naona Ngumu Kutimizilika!
Anaweza Mkuu:

Bima za Afya zinarange kati ya elfu 50 hadi elfu 84 kwa mwaka kwahiyo kwa watu 1000 ni Roughly 50m hadi 84m Avarage Tuweke 65m.

Mitaji ya kinamama laki moja kwa watu 200 maana yake ni 20m.

Bodaboda 20 Hiz Fekon/Skymark/San lG ni Avarage ya 1.5m kwa 20 Total ni mil 30

Kukarabati shule kata ya Tandale tukiassumue kama zipo nne au tano ,Tank za Litre 5000 kwa laki 5(Jumla 2m),Kupaka rangi shule hizo nne na kuchapia letsay kila shule mil 7.5 kwa shule nne au tano mil 30

Kwahiyo akiwa na 150m anaweza kufanya yote hayo.
 
Hongera nitaleta baada kutimiza ahadi
 
Katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa msanii wa muziki wa Bongo Fleva nchini Tanzania, Diamond Platnumz amewaahidi mambo yafuatayo wakazi wa Tandale (mahali alipozaliwa na kukulia)...

1. Kulipia BIMA ya Afya kwa watoto 300,na wakazi wengine 700 (Jumla watu 1000) ndani ya mwaka mmoja....

2. Kutoa mitaji kwa akina mama 200, ya shilingi za kitanzania 100,000/= mpaka 200,000/=

3. Kutoa Boda boda 20 kwa vijana wasio na ajira na kuwatengenezea aina fulani ya menejimenti ambapo kila siku kila kijana itampasa akabidhi sh. 10,000/= ambayo itatumika kununua bodaboda nyingine kwa ajili ya vijana wengine....

4. Kukarabati Shule zote za msingi zilizopo ndani ya Kata aliyozaliwa ya Tandale ikiwa ni pamoja na kuweka matank kwa ajili ya kuhifadhia maji...
maxresdefault.jpg
Diamond Platnumz
Diamond akiongea kwenye sherehe fupi iliyofanyika Live kupitia Wasafi TV, amesema kuwa siku ya Ijumaa Tarehe 5 Oktoba 2018 atatimiza ahadi hiyo ikiwa na pamoja kuchinja ng’ombe na kusherehekea na watu wake wa Tandale pamoja na wasanii wenzake, wageni mbalimbali kutoka serikalini na mashirika binafsi waliojitolea kumuunga mkono.
Mimi nadhani angemsaidia baba yake mzazi kwanza ningeona anazo akili kichwani.
 
Ni jambo zuri ALLAH akufanyie wepesi kwa hilo.

AMIN.
 
Asante sana Naseeb, hii mitaji ni kheri utoe laki tano tano kwa watu 50. Mtaji wa laki moja ni pasua kichwa.

Tandale kuchele turudini kwetu Kwamtogole
leo Kwa Mara Ya Kwanza Umetuonyesha Picha Halisi Ya Wew Hutoki Uswazi Ila Unaigiza Tu Humu Ndani
Mtaji Wa Laki Moja Uswazi Kwa Wamama Unafungua Biashara Zaidi Ya Moja. Ana Uwezo Wa Kupika Maandizi Vitumbua Na Supu Ya Kichwa Hapohapo Bila Shida
 
Asante sana Naseeb, hii mitaji ni kheri utoe laki tano tano kwa watu 50. Mtaji wa laki moja ni pasua kichwa.

Tandale kuchele turudini kwetu Kwamtogole
Laki moja mpaka mbili ni nyingi kwa wakazi wa maeneo hayo. Biashara kama ya genge, kuuza maji, mama ntilie au hata kuuza matunda ya sokoni nyingi ndo mitaji yake hiyo pengine hata pungufu ya hizo. Nafikiri huwa hakuna mtaji mdogo ila sema inategemeana na ushapu wa yule aliyepewa mtaji. Mfano huwezi ukachukua laki moja ukataka kuanzisha biashara ya saloon ya kike. Hiyo haitatosha. Mitaji kama hiyo ni kwa ajili ya zile biashara zinazotoka haraka na hizi ndiyo hufanywa na watu wengi
 
Dada kuna watu wanatumia mtaji wa elfu 50 na wanalaza elfu 20 faida kila siku ... Sio lazma awape nyingi ..kama hauna plan ya biashara ata upewe milioni 20 zitapotea tu .
Asante sana Naseeb, hii mitaji ni kheri utoe laki tano tano kwa watu 50. Mtaji wa laki moja ni pasua kichwa.

Tandale kuchele turudini kwetu Kwamtogole
 
Back
Top Bottom