Diamond Platnumz ahoji kwanini Ali Kiba (mkongwe) hana media yake? Atoa onyo kushindanishwa na wasanii wa Tanzania 'ni wadogo sana kwake'

Kuna watu wanasema EP imebuma, nashindwa kuelewa wanatumia kigezo gani kusema hivyo. Maana hii ep kwa mujibu wa data mbalimbali kutoka music streaming platform imefanya balaa na ni kwa siku chache tu.
 
Sipingi kwamba Diamond sio msanii namba 3, ila mkuu hebu ata wewe ujiulize kwahiyo ukiambiwa utaje wasanii 10 Bora Africa huyo show majdozi unamtaja? Au

Kuna list zingine zinatoka hazina kichwa Wala Miguu, wasanii waliokaa hapo wengi wao kilichowaweka hapo ni mafanikio ya tuzo walizopata miaka ya nyuma

Ndugu yetu Diamond yupo hapo kutokana na zile tuzo za Mtv base alizokuwa anazoa miaka ya 2016-2018 na sio kwamba kafanya vizuri miaka ya hivi karibuni, na ata hao akina 2face,Ipupa,Savage,Yemi alade ni history za 3 yrs previously Ndio zimewaweka hapo

Ila tukija kwenye uhalisia Kwa hii miaka 3 Kwa kazi tu hao wizkid na burnaboy walipaswa kushika wao nafasi ya kwanza Hadi ya Tano Kisha akafatia Davido then ndio wasanii wengine, Kwa miaka hii 3 Mondi mafanikio makubwa ameyapata kwenye biashara na sio kazi yake, hao Jamaa wamemuacha mbali sana hivi Sasa

Anyway, me Bado najiuliza huyo show majdozi aliemuweka hapo kazingatia Nini? Yani kama huyo yupo hapo ata Rayvany alitakiwa kuwa top 10 Sasa maana haiingii Akilini kumweka huyo dada katika wasanii 10 Bora Africa na hiyo List tukaichukulia serious
 
Mkuu mbona kichwa chako Cha habari kinakinzana na BBC? BBC wanasema wasanii wa kuangaliwa mwaka 2021, Yani Kwa lugha nyepesi ni best upcoming artist ila wewe unatuandikia kuwa wasanii maarufu zaidi 10 wa Africa"

Labda mie Ndio sijaelewa Mkuu?
 
Mwaka Jana tu Diamond kama nominated kwenye Tuzo kubwa za BET kwenye kipengele Cha msanii Bora wa Africa akiwa sambamba na Burnaboy na Wizkid Hili umeshasahau? Hii inaonesha jinsi gani hamuwaheshimu wasanii wenu wa ndani hata wakiwa wanafanya vizuri.Mwaka Huu tu diamond aliteuliwa kufanya performance ya Grammy spin na kuwa msanii wa kwanza kwa east africa kuperform kwenye hiyo platform unavyoniambia kabebwa na mafanikio ya 2016-2018 na kuwa na doubt hata na ufuatiliaji wako wa mziki kiujumla
 
Yupo sawa,

Sema akakae Shule ya Uongozi kwanza kwa H.Baba ili ajifunze tambo, au kwa T.I.D🤣
 
Hivi kila msanii mkongwe napaswa afungue media kumbe, sikujua hili.
Only in Tanzania.
Diamond ni mkubwa na mengine nakubali.
Ila hao watangazaji wana maswali ya kijinga, sasa kuwa msanii mongwe na kuwa na media wapi na wapi.
 

Mkuu me ni kijana kama alivo Diamond na Naheshimu sana kazi Zake na hustling yake, we achana na hayo mambo ya nominations hayana uhalisia, ndomana Kuna mwaka Kiba alibeba tuzo ya Mtv ema mbele ya wizkid

Wizkid alikuwa hataki ata kuziskia tuzo za Mtv base na alikuwa ata akiwa kwenye nominations haendi na wala hapost cover kuomba kura Kwa sababu anajua mambo ya tuzo Yana ukiritimba mwingi

Tuache unafki na tuongee ukweli Wakati Diamond anakuwa nominated kwenye tuzo za BET category Moja na wizkid na burnaboy, Kwa moto ambao hao jamaa wameuwasha huyu Ndugu yetu Diamond alikuwa na ngoma Gani iliyomfanya akae pamoja na hao jamaa?

Unaongelea kufanya performance ya Grammy spin kuwa aliteuliwa? Ndugu Yangu hizo nafasi wanachekecha mameneja wanavyojua wao, na sio kwamba from no where tu anateuliwa msanii, hizo mambo ni sawa na kuandaa michuano ya Kombe la Africa, you have to fight for it

Wasanii kama kina wizkid wao mziki wao Ndio unawapeleka huko unyamwezini, unadhani diamond nae hizi GidiGidi Ndio zitamfikisha huko? Jamaa anajua kutumia opportunity, kaona kufika huko kwa mziki it's kinda harder, kaona afaiti kupata coverage kupitia hiyo performance na yeye anajua target yake ni nini
 
Eyce naona umetoa maelezo ambayo ni tofauti na sababu aliyotoa Diamond majaji wanahusikaa na hizo Tuzo ni watangazaji wa clouds, efm na east africa ambao hawapigi nyimbo zake ukiachana tu naivyo ni msanii ambaye hajapewa mrabaha na akasema kama hawajampa mrabaha ndio watampa hizo tuzo? Diamond alichoonyesha hizo tuzo hazipo kwenye system ya haki ndio maana kazisusia akauliza Tena msanii kama marioo ngoma zake zimechezwa karibia radio zote na mtaani lakini Cha ajabu hayupo kwenye list ya waliopata mrabaha
 
wewe kwa maelezo yako unaonekana ni hater tu na humkubali huyu kijana. Muda ni jibu tosha kwako, ngoja siku ziende utaelewa kuwa huyu kijana ni fighter
 
Ulichonijibu imeonesha kabisa una wivu pia ni hater wake kitu ambacho umeshindwa kujificha
 
Music stars to look out for = Upcoming stars
 
Nick alizigomea BET na hata familia nzima ya cash money baada ya BET kutumia official page yao kumdhihaki Nick baada ya kushindwa na Cardi B katika Grammy Awards. Pia Grammy Awards zishawahi kuwa boycotted mara nyingi sababu ya kuonekana kama zina ubaguzi kwa black artists kutokana na process zake

Ila huwezi sikia Nick akisema sistahili kuwekwa kwenye category moja na wasanii wengine kwenye grammy.. NEVER
 

Nilikuwa namjibu huyo jamaa aliyesema Diamond hastahili kushiriki hizo tuzo sababu yeye yupo kwenye league nyingine..
Ni kweli internationally, locally bado yupo katika competition kwenye kutoa quality works
 
Yy hatak kwasababu ya ukiritimba uliopo kwenye hizo tuzo, na si kwamba amedharau uwezo wa wasanii wengine. Hivyo kuzikataa sioni shida wale waliotayar washindane tu.
Jibu langu lilikuwa kwenye context ya comment ya huyo niliyemquote mkuu. Diamond akigoma kuchukua tuzo ni ha ki yake na hatokuwa wa kwanza maana hata dully alizigomea kili music awards
 
Ulichonijibu imeonesha kabisa una wivu pia ni hater wake kitu ambacho umeshindwa kujificha
Mkuu naomba nipinge Kwa Hoja, haiwezekani Kila kitu ukubali ndio uonekane unakubali juhudi za mtu flani, kwahiyo ukiwa sio hater ndio Kila kitu unakubali?

Me hakuna ata sehemu Moja nimembishia alichokisema Diamond, nimepinga hiyo list ya wasanii 10 Bora Africa, na nikauliza show majdozi amefikaje hapo namba 10? Show majdozi anamzidi nini Rayvany labda ambae ye kwenye list hayupo?

Kuna wasanii wapo hapo kutokana na mafanikio Yao ya miaka kadhaa nyuma, mfano 2face hapo ameingiaje? Savage Je? Yemi alade nae? Kuna Ipupa hapo nimemtaja, ila nyie mmeona Kwa Diamond tu

Nimeongelea status ambayo wameitengeneza Wizkid na burnaboy ni level ingine kabisa ata kukaa category Moja na Diamond kwenye tuzo za BET haimaanishi wako level Moja Kwa Sasa, ata Alikiba aliwahi kushinda tuzo ya Mtv ema mbele ya wizkid kwani Kuna mwaka Kiba amewahi kuwa level sawa na wizkid?

Diamond na hao jamaa waliwahi kuwa level 1 miaka ya nyuma ila sio miaka hii miaka ya Karibuni Mkuu, me sina chuki na mtu Bali naongea Facts, na Kama unataka kunipinga basi leta Facts pia, me nimchukie mtu hanijui simjui itanisaidia nini labda, Kila mtu anaona na kuheshimu hustle za Diamond ila sio sababu ya kunifanya niwe kibendera mfata upepo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…