Diamond Platnumz anahitaji kukua

Diamond Platnumz anahitaji kukua

Hivi alikiba ameenda hadi sasa unapoposti huu uzi? Au msiba uko insta alikopost? Weka picha ya kiba akiwa msibani.

The Future is in Our Brain,Tongue's&Hand's.
Leo nimeamini usemi wa TRUMP " kwamba mwafrika ni mtu mjinga"
Hivi ukipost kunaimpact gani kwa marehemu ?
au saiv kupost ndo ishala ya kwamba tuna uchungu sana?
Tuache kuendeshwa na mitandao bali tuishi kwa uhalisia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Well, sote tunajua kifo ni sehemu ya maisha na kwa yakini kifo ni wajibu kwa kila chenye uhai.

Kimsingi kifo kina definition nyingi sana kwa mwanaadamu na hizi definition zinatokana na imani zetu ambazo kwa asilimia kubwa ni mirathi ambayo tumerithi kutoka kwa wazazi wetu au familia zetu au mazingira ambayo yametuzunguka.

Japo kuna watu wengi sana ambao wamechukua dafina ya kukielezea kifo kutokana na mandhari ya uelewa wao ikiwemo watu wa dini, sayansi pamoja na mamluki wengine lakini mpaka sasa hakuna aliyekuja na ithibati ya hakika juu ya nadharia ya kifo. Hivyo basi, suala la kifo linazidi kubaki kuwa ni FUMBO TATA kwa Ibn-Adam.

Mimi ni miongoni mwa binaadamu ambao nimebahatika kuishi nchi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuishi na wananchi kutoka mataifa pande zote za dunia wenye imani, rangi, dini, kipato, siasa, elimu mbalimbali na zisizolingana.

Nimeishi na watu ambao watakupokea kwa ukarimu au kwa kawaida kutokana na dini au rangi au elimu au kipato chako.

Kadhalika, ninashukuru sana kuwa miongoni mwa waafrica wenye kutumia majina yenye asili ya kiafrica, yaani yenye asili ya kitanzania kwa majina yote 3, majina ambayo yaliasisiwa na wazee wetu kabda ya uvamizi wa kiimani barani Africa, kwa Tanzania ni takribani miaka 150 or so kabda ya Christianity, Islam, Atheism wa hakadha.

Kimsingi dini, siasa, ukabila na kadhalika, ni vitu ambavyo vime shindwa kabisa kumuunganisha binaadamu na kumfanya kuwa kitu kimoja na haitokuja kutokea vitu hivi kutufanya kuwa kitu kimoja, Abadan! Vitaendelea kututenganisha mpaka mwisho wa dunia, ikiwa huo mwisho upo.

Kifo ni kitu pekee ambacho kimebaki kama tumaini la kumuunganisha binaadamu, ni kipindi pekee cha ukimya ambacho kwa dakika chache humkumbusha binaadamu hatma na mustakabali wake hapa duniani, ni kitu pekee ambacho kimepelekea kujiuliza maswali mengi kuliko majibu kama who are we, what came before, how life came to be? where God came from, nani aliyeumba maisha ?na aliyeumba maisha aliumbwa na nani? These are very honesty questions na majibu yake ni dhana ya binaadamu inayomfanya aishi kwa utulivu hapa dunia, lakini ukweli wake kwa yakini haufahamiki. NI FUMBO TATA.


Kifo, ni kitu pekee ambacho tumeona wengi hupatana na kusahau tofauti zao na kwa sababu ya huruma ya kifo, wengi hukusanyika na kuonesha upendo na huruma ya kuwa sisi ni kitu kimoja na hii ni njia yetu sote, ni suala la muda tu kwa maana hakuna aliye juu ya kifo.

Ikiwa binaadamu unashindwa kujirudi katika kipindi cha kifo na kujumuika na kadamnasi, basi shida ipo kubwa. Ndugu yetu bwana Diamond Platnumz hatujui shida yake na marehemu ni nini inayo mpelekea kushindwa kuonesha Maturity ambayo ime create attention na maswali mengi kuliko majibu.

Attention ambayo imekuja kwa sababu Naseeb ni msanii kwenye tasnia ya mziki ambayo kimsingi Ruge ana nafasi yake kubwa sana na hata kazi wameshawahi kufanya pamoja mara si haba.

Kwa namna moja au nyingine D ana shombo ya Ruge kwenye mafanikio yake aliyoyapata miaka michache nyuma na Ruge atabaki kuwa ndugu wa D pamoja na tofauti zao. Ruge M ana mabaya yake kama ilivyo kwa binaadamu wengine, lakini pia ana mazuri yake.

Paul Makonda ameweza kuziba masikio na kujumuika kwenye msiba,hii ndiyo Maturity na haina maana kuwa makonda anajisafisha, la hasha! anaonesha ukubwa na ubinaadamu.

Aidha, Makonda, Ruge M na Naseeb A ni makada wa CCM wenye nidhamu ya hali ya juu kwenye chama na kwa mwenyekiti wa chama. Appointment ya Makonda kuwa mlezi wa WCB haikuwa kwa bahati mbaya,

D anapaswa kujitafakari na kujitathmini, japo anaamini hili pia litapita, lakini asiamini kuwa litapita kwenye vifua vya mashabiki wake na hata kwa viongozi wa chama tawala ambao kimsingi wanamtizama kwa macho ya chini.

—Imani yake ni kuwa hataki kuwa mnafiki, lakini sio kila imani ni sahihi.

Kuna list kubwa ya wasanii ambao walipotea kwa kushindwa kuwa na Maturity na mtazamo chanya wa maisha.

Mwisho, nachelea kusema anachofanya Dplatnumz ni kibri, ninaamini kuwa ni ukosefu wa exposure na maturity. Na kusafiri sana nje haimaanishi ndiyo exposure.

Exposure ni kuwa na mtazamo chanya katika maisha juu ya yale ambayo unatofautiana na wengine.

—they say , the way you see the problem is the problem.

Cordially,

MK54, February 28, 2019
------------
Upuuuuzi mtupu. Umeandikaa ngonjera nyingi Kama unamtongoza demu wa kihindi
Siku nyingine uandike kwa ufupi? Hatuna muda wa kusoma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunaishi kwenye dunia ya kibepari na bado tunalalamika kunyonywa akili kumkichwa ukishangaa inakula kwako...huyo diamond na mgt yake nao ni wanyonyaji tena makatili haswaaa (refer rich mavoko case), wana hila za kila namna, wamejaa chuki na visasi inapokuja kwenye suala la maslahi ni jambo lingine...anzisheni biashara zenu afu muwe fair tuone
 
Kwani akikua atakua ana fufua watu?
Pambana na hali yako kiongozi


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Umeandika ujinga "samahani ila ndio ukweli wenyewe" diamond ni mtu wa karibu sana na CMG kuliko unavyodhani.
.
Sasa naomba unijibu hili swali watu wako wakaribu ama ndugu zako waliotangulia mbele za haki uliwahi kuwapost instagram au Facebook kwamba R.I.P na ni nini maana ya kufanya hivyo je ni ushamba? Kuonyesha umeguswa sana? Au ni nini?
 
Ujinga ni ule ule tuuu watu mmekua wajinga kweli baba jitu zima na manywele yako ya mkundu unakaa unamwandikia nani haya?
 
Kuna mzazi alimkaripia mwanae kwa kumwambia "kama mimi nisingekusomesha usingefika hapo ulipo, unishukuru mimi nakwambia"
Mtoto nae akajibu "kama na mimi nisingekazana kwenye masomo, hela yako ingeenda bure nakwambia, unishukuru mimi"

Wakati fulani tukubali kuwa, kunisaidia kupanda kutoka sehemu moja kwenda nyingine, sio kigezo cha kuninyanyasa utakavyo, hapana.
Kitendo cha kutopost chochote kwenye page zake, kwa wenye akili tushajua msimamo wake ukoje. Itoshe sasa tujikite kwenye kuomboleza msiba hadi tutakapoanua matanga.
 
Kwani wangapi hawajaenda?!Profesa,Sugu,Vanessa,Jux,Mimi Mars ushawaona wamekwenda?!vipi Idrissa Sultani,Wemasepetu,Gigymoney,Ushawaona wamekwenda?!
Nikkimbishi,Jide,Alikiba na watu wake,ushawaona?!
.
Unafiki mbaya sana,mwacheni Diamond sio lazima kila mtu amlilie huyo Ruge!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi hua nakasirika sana mtu kusema flani kapitia kwa flani ndio akatoka..!Napinga kwa herufi kubwa.KUTOKA ni kipaji cha mtu.So ukiona msanii katoka ni kipaji chake na juhudi zake.Hapo mnaposema kapitia kwa nani sijui kwa nani!Hao ni kama daraja tu na hata asingepitia kwa huyo tokana na juhudi zake angetoka tu sema labda angechelewa "you never know"..
Kwa akili za kawaida mtu akifa hana thamani tena.Uende msiban ama usiende lazima atazikwa.
Nashaanga sana kuona mtu analaum flani hajaenda msibani badala ya kulaumu kwa nini hakwenda wakati akiwa mgonjwa.Upendo wa kweli au hata ukiwa wa kinafiki ni kuoneshana tukiwa hai.
Asante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ana maamuzi yake huwezi jua maana msiba bado haujaisha na asipoenda poa tu, kwani unajua walizinguanaga wapi? Kuna watu ndugu wa damu wengine wamekosana na walezi au wazazi wao na wameapizana kutozikana Diamond ye nani kwa Ruge? Achanane na maisha ya watu kila mtu UZI MOND VS RUGE[emoji34][emoji34][emoji34][emoji34][emoji34]

Sent using Jamii Forums mobile app
Povu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom