Diamond Platnumz badili mwenendo before it’s too late!

Diamond Platnumz badili mwenendo before it’s too late!

Sijafananisha attitude au perception ya mtu, nimefaninisha mazingira ya kazi note that.

Kabla ya Diamond lini uliona mwanamuziki wa kibongo amekuwa nominated for BET? Ila kwa nigeria ata upcoming ni rahisi kwake kupata hiyo fursa eg tems na sbb kubwa ni mazingira ya kazi yao ya Sanaa yapo juu kuliko ya yetu ya bongo na ndio maana kwenye tuzo kila siku tunamsikia Diamond tu kwann
So what is your point?

Diamond anatumia madawa ya kulevya kwa sababu ya mazingira ya kazi?
 
Kuna watu wengi wataona ni vigumu sana kufanya kitu sahihi hapa, ambacho ni kumhurumia Diamond kama mgonjwa/victim.

Kwa sababu jamii yetu inaangalia pesa kama kila kitu. Yani ukiweza kupata pesa tu, unaonekana mjanja.

Sasa watu wanamshangaa Diamond, imekuwaje amepata ujanja wa kupanda ngazi kwenye usanii wenye competition sana, halafu ashindwe kuji control kwenye madawa ya kulevya?

Ukiangalia hili jambo ni tatizo dunia nzima. Ni kama vile wasanii wanapata pressure sana kuwa creative na kubaki on top, wanapata pressure kuandikwa sana, tunawaingilia maisha yao binafsi sana kama tunawajua personally wakati hatuwajui kihivyo, mwishowe wanaji boost kwa madawa kama coping mechanism.

It is very hard to argue for sympathy for Diamond, kama mtu, kama mgonjwa, kwa sababu jamii yetu inaangalia umasikini wa fedha kama ndiyo tatizo kubwa, haiangalii umasikini wa akili na mambo yanayohusu afya ya akili kama tatizo.

Mimi nilikuwapo katika watu walioanzisha Bongoflava siku hizo, ila niliamua kutoendelea huko, kwa sababu niliona gharama ya u star kwenye kutokuwa na privacy.

Hili ni jambo kubwa sana ambalo watu wanalichukulia poa tu.
Nisingeweza kusema zaidi, asante Mkuu Kiranga
 
Kwa msanii husasani hawa wa bongo kwanza wote wanatumia vilevi eg pombe kali sbb kubwa ni makundi na kupata ujasiri kwenye kazi.

Kupanda kwenye jukwaa kwa zaidi ya saa 1 na watu wakushangilie tu sio kazi rahisi
Sawa sawa ,wengine kuiga tu, uzuri nimeishi hayo mazingira ya uuzaji na uvutaji ngada , hawa wasanii wengine wafuata mkumbo

Sasa kama Diamond anakula unadhani chawa wake itakuaje? Si watafuata mkumbo
 
Bro mie nimepoteza madogo zaidi ya watatu kwa Ngada, akiwemo Langa, D Roby na wengineo ,maeneo ya Msasani /oysterbay ,mikocheni

Uzuri nimekaa na wauza Ngada na wavutaji, kuna madogo waliingia ktk ngada ile kujifanya wanyamwezi ,wakishua ,wako juu , kumbe wanapotea
Hilo lilitakiwa kukufanya uwe na empathy/sympathy zaidi kwa hawa watu.

Nashangaa unavyosema huna hurumankwa hawa watu wakati kwako hili si jambo abstract una mifano ya watu wa karibu.

Watu waliosoma kwa undani haya matatizo wanasema uraibu ni ugonjwa.

Inawezekana tusiuone kuwa ni ugonjwa kwa sababu ninugonjwa wa kisaikolojia zaidi.

Sasa unachofanya hapa ni kusema kwamba huna hurumankwa mgonjwa.

Ni sawa na kusema kwamba humuonei huruma mtu anayeumwa Malaria.
 
Uwe muelewa basi, nani kasema ana majukumu mengi kuliko Elon? Nimesema mazingira ya kazi ya Diamond na Elon ni tofauti, Diamond ana mazingira magumu ya kazi kuliko Elon, katikati ya wasafi festival Diamond alisafiri kwenda Marekani kama sikosei mara 2 ndani mwezi mmoja. Sasa hapo unazijua changamoto za usafiri kati ya Elon na Diamond alaf bado arudi ajiandae wasafi festival?

Hao wasio tumia madawa ata kutumbuiza kwa masaa zaidi ya 2 kwenye stage na kwa nguvu km ya Diamond wanaweza?
Dah! Ile heshima yote niliyokupa nimeiondosha!

Yani kwamba Elon Musk ana mazingira rahisi ya kazi kuliko Diamond? Hivi unajua unamuongelea tajiri namba 1 wa Dunia nzima?
Mtu mpaka kufikia kuwa tajiri namba moja awe na mazingira rahisi ya kazi? Acha tu huko kumfananisha na Diamond.

Basi, mjadala wetu umekwisha.
 
Naandika hii thread kwa machungu sana, hili limeniwia vigumu sana kulisema hapa, lakini imenibidi!

Siandiki nionekane nilisema, wala sipendi siku thread hii ije kufukuliwa kwamba yametimia, wala siandiki kama umbea. Hili ni suala serious juu ya kijana mwenzetu huyu maarufu pengine kuliko kijana yeyote kutokea katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya.

Ni nini kimekusibu Naseeb? Kwanini ulifikia uamuzi huo wa kutumbukia huko ulikotumbukia? Imeniumiza sana, kweli!
Mimi sio shabiki wako, ila siwezi kupinga wewe ni Icon, watu wanakutazama kama nembo ya upambanaji!
Na sidhani kama unajua wewe ni mtu mkubwa kiasi gani! Mambo mengi ambayo huwa unafanya yanathibitisha hilo, hili pia likiwemo.

Ndugu unayesoma haya, kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa masuala ya wasanii na maisha yao hasa hapa kwetu Bongo lazima utakuwa umewahi kusikia tetesi za Diamond kutumia madawa ya kulevya, mengi yamesemwa… wengi wamesema.

Alianza Harmonize kipindi wapo kwenye ‘bifu’ kali baada ya kuachana na iliyokuwa label iliyomsimamia katika safari yake ya muziki ambayo mmiliki ni Diamond, kila mtu anajua jinsi mtifuano ulivyokuwa mkali baada ya Harmonize kuondoka.
Na katika mtifuano huo ndipo Harmonize alituhabarisha kuwa Diamond ni mteja wa madawa ya kulevya, binafsi sikuamini na niliomba isiwe kweli.
Sikuamini kwakuwa katika ugomvi kila mmoja atasema lolote la kumuumiza mgomvi wake, haikuwa na mashiko sana.

‘Dada wa Taifa’ Mange nae mwaka huu amehakikisha kwa kujiamini kabisa kuwa Diamond anatumia madawa ya kulevya, amesema hivyo mara nyingi… pia sikuamini.

Sasa baada ya maneno na tuhuma hizo juu yake mimi binafsi nikaingia ‘chimbo’
Kila mmoja ana chanzo chake kikuu cha habari, hasa kwa sisi wadau wa habari zote ngumu na nyepesi…
Nikauliza ili nijihakikishie je ni kweli yanayosemwa!
Nilichoambiwa ndicho kimenifanya niandike hii thread, nilijibiwa kiufupi kabisa, “NI KWELI ANATUMIA”

Siko hapa kubishana wala kumshawishi yeyote akubaliane na chanzo changu, mimi mwenyewe ndio naujua uzito wa chanzo changu hicho nyeti. Kiufupi ni kwamba chanzo changu hiki kikiniambia kesho nitafariki naanza kabisa kutubu!

Lengo kuu ni kuongea na muhusika mkuu, Jamii Forums ni platform kubwa pengine atafikishiwa haya.

Tafadhali Naseeb, badili mwenendo. Bado hujafikia hatua mbaya, unaweza kuacha kuanzia sasa ukarudi ktk hali yako ya kawaida.
Hukuona yaliyomkuta Whitney Houston? Wewe una ukubwa gani kumzidi malkia yule wa muziki wa muda wote?

Mifano ni mingi, kwa maslahi ya Taifa tusingependa siku ifike na wewe tukutolee mfano.
Wewe ndiye unayeujua ukweli zaidi kwanini umefikia hatua hiyo, ila tafakari nafasi yako ulipo na ubadilike.

Nifah
Tukikuita uthibitishe haya uliyoyaandika utaweza kuthibisha?
 
Dah! Ile heshima yote niliyokupa nimeiondosha!

Yani kwamba Elon Musk ana mazingira rahisi ya kazi kuliko Diamond? Hivi unajua unamuongelea tajiri namba 1 wa Dunia nzima?
Mtu mpaka kufikia kuwa tajiri namba moja awe na mazingira rahisi ya kazi? Acha tu huko kumfananisha na Diamond.

Basi, mjadala wetu umekwisha.
Sasa ww nikuulize swali mazingira ya kazi ya Elon unayafaninisha na ya Diamond? Kumbuka Tz ni nchi inayoendelea ila huyo Elon nchi yake ilishaendelea, je?

Katika utendaji kazi wa kila siku bwana Elon ana vitu wezeshi vingi tena vyenye teknolojia kubwa kuliko ata Diamond mfano ishu ya bandari na Dp, watu wa Dp worldwide wanadai wana mifumo wezeshi kuliko ss wa Tz so ata wakifanya kazi nyingi kwa siku energy wanayotumia inakuwa tofauti na mamlaka husika za bandari wangefanya the applied to Diamond na Elon.

Siwezi kumfaninisha Elon na Diamond maana Elon ni safari nyingine na ndio maana nasema majukumu ya ki ukurugenzi na msanii ndio vinamfanya tumuone Diamond km mnavyodai nyie
 
Fatilia mtiririko wa hoja usidakie vitu kwa juu
Mtiririko wa hoja kutoka wapi? Wewe ndiye uliyeshindwa kuonesha post hii ilitoa hoja hii.

Mpaka sasa unaonekana kama mtu unayesema uongo kwamba kuna hoja ulitoa wakati hujatoa.

Ndiyo maana huwezi hata kuweka ushahidi wa link au post namba kwamba post hii nilitoa hoja hii.

Nitafuatiliaje mtiririko wa hoja hapo sasa?

Siamini kama una mtiririko wowote wa hoja, thibitisha hilo kwanza kwa kutoa posts na namba zake na links.
 
Kabisa kabisa
Sasa inakuwaje unakosa huruma kwa mgonjwa?

Unasema umewaonya na hawakusikilizi, unajuaje unapowaonya wana will power ya kukusikiliza na kushinda huo ugonjwa wa akili?

Unajuaje kuwaonya tu kunatosha?

Ukikutana na mtu ana homa ya Malaria unaweza kusema huna huruma kwa mtu mwenye ugonjwa wa Malaria?

Ukikutana na kichaa anaokota makopo uchi, unaweza kusema kuwa huna huruma na mtu mwenye ugonjwa wa kichaa?
 
Mtiririko wa hoja kutoka wapi? Wewe ndiye uliyeshindwa kuonesha post hii ilitoa hoja hii.

Mpaka sasa unaonekana kama mtu unayesema uongo kwamba kuna hoja ulitoa wakati hujatoa.

Ndiyo maana huwezi hata kuweka ushahidi wa link au post namba kwamba post hii nilitoa hoja hii.

Nitafuatiliaje mtiririko wa hoja hapo sasa?

Siamini kama una mtiririko wowote wa hoja, thibitisha hilo kwanza kwa kutoa posts na namba zake na links.
Mkuu basi endelea kudakia vitu kwa juu
 
Uwe muelewa basi, nani kasema ana majukumu mengi kuliko Elon? Nimesema mazingira ya kazi ya Diamond na Elon ni tofauti, Diamond ana mazingira magumu ya kazi kuliko Elon, katikati ya wasafi festival Diamond alisafiri kwenda Marekani kama sikosei mara 2 ndani mwezi mmoja. Sasa hapo unazijua changamoto za usafiri kati ya Elon na Diamond alaf bado arudi ajiandae wasafi festival?

Hao wasio tumia madawa ata kutumbuiza kwa masaa zaidi ya 2 kwenye stage na kwa nguvu km ya Diamond wanaweza?
Kusafiri mara mbili kwa mwezi kwenda Marekani ni mazingira magumu? Unajua Elon anasafiri mara ngapi kwa mwezi?

Kwani Chid Benz, TID au Lord Eyez walikuwa wanatumbuiza kwa muda wa saa ngapi jukwaani? Huku wakitumia dawa za kulevya?

Ondoka kwenye fikra za kutafsiri uwezo wa kutumbuiza muda mrefu, kuwa siyo utumiaji dawa za kulevya. Iko tofauti.

Ova
 
Back
Top Bottom