Diamond Platnumz hili la kumfananisha demu (msichana) wako na Yesu (Mungu) utuombe radhi wakristo na utubu au wimbo wake ufungiwe na BASATA

Diamond Platnumz hili la kumfananisha demu (msichana) wako na Yesu (Mungu) utuombe radhi wakristo na utubu au wimbo wake ufungiwe na BASATA

Nimeusikiliza wimbo mpya wa Diamond Platnumz uitwao ongeza kiukweli anatakiwa atafute mhariri wa mashairi na mistari yake. Kwenye ngoma ya ongeza anasema "we ndo wangu yesu mkombozi sa mbona unaniacha mwenyewe" anamuongelea mwanamke/ msichana/demu wake.

Kwa hili Diamond hapana umeenda mbali mno na umetukosea Wakristo. Hivi mkristo aimbe wimbo amljnganishe demu wake na Mtume Mohammad au Allah atakuwa sawa?

Kwetu Wakristo Yesu ni Mungu kweli, mtu kweli Yohana Mtakatifu 1:1-10. Yesu ni Mungu mwana katika nafsi tatu za Mungu zinazofanya Utatu Mtakatifu.

Yesu aliacha kiti chake cha enzi kule mbinguni akauvaa mwili akashuka duniani ili atufie na kutukomboa sisi na dhambi zetu. Alisulubiwa akafa, akazikwa siku ya tatu akafufuka na sasa ameketi mkono wa kuume wa Mungu Baba na hapa tulipo tunasubiri arudi aje awahukumu walio hai na wafu. Maana ameahidi anakwenda kwa Baba kutuandalia makao na atakuja kutuchukua ili alipo nasi tuwepo. Je ni Yesu huyu wa kumlinganisha na demu wake kweli Diamond Platnumz?

Yesu huyu ambaye alikuwepo kabla ya ulimwengu kuumbwa ambaye maandiko yanasema vitu vyote viliumbwa kwa jina lake na pasipo yeye hakuna kilichoumbwa? Huyu ndiyo wa kumlinganisha na demu.


Ni kweli sanaa inahitaji ubunifu lakini siyo kwa kiwango hiki Diamond aombe radhi kwa kweli au wimbo wake ufungiwe na BASATA.
Bahati mbaya huwa sisikilizi!
But for this,no way!
Najua basata wamesikia na watalifanyia kazi!


JESUS IS LORD[emoji120]
 
Yohana 8:58
Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye IBRAHIMU ASIJAKUWAKO, MIMI NIKO.

NIKO ni jina la Mungu peke yake. Tunakutana na jina hilo pale Musa alipoongea na Mungu na kutumwa kuwakomboa wana wa Israeli kutoka Misri. Imeandikwa:

Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n'nani? Niwaambie nini? Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO (Kutoka 3:13-14).
Mkuu achana nae huyo haelewi chochote!
Yesu ni Mungu!

JESUS IS LORD[emoji120]
 
Nimeonja Utamu Wa Yesu
Ya Rose Muhando imekubaliwa na Wakristo kisa ni msanii wa Injili
Ila hii ya Leo imekataliwa na wakristo kisa ni Diamond

Mungu yuko wapi ya Ney imekubaliwa sikuona aliyeibuka kuipinga wala kusema haitakiwi
Ma Niggas huwa wanaimba nyimbo za kukejeli kule Marekani na za kuhusisha Freemasons kuipinga Imani ya Kristo hamkuibuka kupinga.

Wakati fulani niliwahi kumtongoza msichana akaniambia sikati kuolewa mwanaume pekee na rafiki yangu ni Yesu tu

Acha Nikae Kimya[emoji850][emoji850]
Unajua kuwa alichookiimba Rose hakukitoa hewani?
Read the bible!
Wakristo sio wajinga!
Rose hajukurupuka huo ni mstari upo kwenye biblia!

Ney kwenye winbo wake hajamtaja Yesu,kamtaja mungu!
Sasa ni mungu gani anajua yeye coz kuna mungu wengi tu waliojifunua kwa namna tofauti na wanaabudiwa na biblia IPO wazi!
,ila Mungu in mmoja tu!
Ila angekua specific ni mungu yupi tungeelewa!

Sio kila anaetaja mungu,anamaanisha Mungu(Jehova) there s a big difference!

JESUS IS LORD[emoji120]
 
Ninyi mnaolalamika sio Wakristo wa kweli. Sisi Wakristu hatuhukumu mtu. Yeyote mwenye makosa atahukumiwa siku ya mwisho.
 
Wewe unajua kusoma?
Siku 40 kabla ya kupaa kwake mwaka gani?

Unaelewa kwamba kurudi kunakozungumziwa hapa ni kwa mara ya pili baada ya huko "kupaa"?

Unaweza kuthibitisha alipaa, na kwamba habari za kupaa kwake si hadithi za uongo tu?
 
Siku 40 kabla ya kupaa kwake mwaka gani?

Unaelewa kwamba kurudi kunakozungumziwa hapa ni kwa mara ya pili baada ya huko "kupaa"?

Unaweza kuthibitisha alipaa, na kwamba habari za kupaa kwake si hadithi za uongo tu?
Unaweza kuthibitisha kuwa Mungu yupo?Msipende kuingilia imani za watu!Waache waamini wanavyoamini!
 
Mimi mwenyewe leo nitapaa mbinguni, nyinyi endeleeni kukaa hapo na ubwege wenu mnisubiri, mimi nitakuja kuwaokoa tu nyau nyie, okay?
 
Kama kiranga yupo basi nasogea benchi la mbele kushuhudia mechi
 
Unaweza kuthibitisha kuwa Mungu yupo?Msipende kuingilia imani za watu!Waache waamini wanavyoamini!
Wewe unayeuliza uthibitisho wa uwepo wa Mungu hujaingilia imani za watu?

Mbona unaweka sheria unayoivunja mwenyewe?

Unaelewa hata unachoandika wewe mwenyewe maana yake ni nini?
 
Wewe unayeuliza uthibitisho wa uwepo wa Mungu hujaingilia imani za watu?

Mbona unaweka sheria unayoivunja mwenyewe?

Unaelewa hata unachoandika wewe mwenyewe maana yake ni nini?
Hujaelewa,kumwambia mtu athibitishe kuwa Yesu sijui alifanya nini sio sawa!Ndio maana nikamuhoji na yeye kama anaweza kuthibitisha kama Mungu yupo!
Hapa namweleza kuwa mambo ya imani waachie wenye imani hiyo!
Hilo nalo ni gumu kuelewa?
 
Hujaelewa,kumwambia mtu athibitishe kuwa Yesu sijui alifanya nini sio sawa!Ndio maana nikamuhoji na yeye kama anaweza kuthibitisha kama Mungu yupo!
Hapa namweleza kuwa mambo ya imani waachie wenye imani hiyo!
Hilo nalo ni gumu kuelewa?
Sasa kama Diamond imani yake inamruhusu kumfananisha mpenzi wake na Yesu, akisema hilo, wanaomsakama watakuwa hawajaingilia imani yake?

Ukimsakama Mkristo kwa kula nguruwe, wakati imani yake haijamkataza kula nguruwe, hapo hujamuingilia imani yake?
 
Sasa kama Diamond imani yake inamruhusu kumfananisha mpenzi wake na Yesu, akisema hilo, wanaomsakama watakuwa hawajaingilia imani yake?

Ukimsakama Mkristo kwa kula nguruwe, wakati imani yake haijamkataza kula nguruwe, hapo hujamuingilia imani yake?
Kwanin yule aliyeikashifu quran alifukuzwa kazi na serikali?Vp kama imani yake inamwelekeza hivyo?Kumfananisha Yesu(ambapo kuna imani wanaamini ni Mungu wao) na demu wake ni kuwakosea heshima!
Kesho nao wanaweza kuamka na kuimba "maumbile yako ndiyo Mohamad SAW wangu"!
Huoni hapa ni kutafuta uvunjifu wa amani?Tena narudia,wakristo ni watu wastaarabu sana!Hayo maneno yangegeuzwa kwa imani ile na mungu wao akafananishwa na tupu ya mwanamke,ingekuwa balaa sasa hivi!
 
Kwanin yule aliyeikashifu quran alifukuzwa kazi na serikali?Vp kama imani yake inamwelekeza hivyo?Kumfananisha Yesu(ambapo kuna imani wanaamini ni Mungu wao) na demu wake ni kuwakosea heshima!
Kesho nao wanaweza kuamka na kuimba "maumbile yako ndiyo Mohamad SAW wangu"!
Huoni hapa ni kutafuta uvunjifu wa amani?Tena narudia,wakristo ni watu wastaarabu sana!Hayo maneno yangegeuzwa kwa imani ile na mungu wao akafananishwa na tupu ya mwanamke,ingekuwa balaa sasa hivi!
Kwani huyo aliyefukuzwa kazi alifukuzwa na Diamond?

Mbona unachanganya madawa?

Serikali yetu yenyewe haijielewi, inajisema haina dini, lakini Bunge linafunguliwa kwa dua.

Contradiction tupu.

Sasa hiyo ndiyo ya kuiangalia kama dira?
 
Hapa nilipo namsikiliza Ariana Grande anaimba God is a woman. Kawimbo katamu sana.
 
Kwani huyo aliyefukuzwa kazi alifukuzwa na Diamond?

Mbona unachanganya madawa?

Serikali yetu yenyewe haijielewi, inajisema haina dini, lakini Bunge linafunguliwa kwa dua.

Contradiction tupu.

Sasa hiyo ndiyo ya kuiangalia kama dira?
Sio sawa kukashifu imani ya watu wengine!Katika vitu ambavyo si vya kuchezea ni imani za watu,ni rahisi sana amani kutoweka!
Diamond amekosea kukashifu imani ya wakristo wanaoamini kuwa Yesu ni Mungu kisha yeye akamfananisha na Mwanamke wake!
Mtu anaweza kujibu kwa mtindo huo huo na kumfananisha Mohamad SAW na vitu vyao halafu ikaleta shida!
Yaani Diamond kakosa mistari ya kumfananisha na Demu wake mpaka amataje Yesu?Shenzi kabisa!
 
Sio sawa kukashifu imani ya watu wengine!Katika vitu ambavyo si vya kuchezea ni imani za watu,ni rahisi sana amani kutoweka!
Diamond amekosea kukashifu imani ya wakristo wanaoamini kuwa Yesu ni Mungu kisha yeye akamfananisha na Mwanamke wake!
Mtu anaweza kujibu kwa mtindo huo huo na kumfananisha Mohamad SAW na vitu vyao halafu ikaleta shida!
Yaani Diamond kakosa mistari ya kumfananisha na Demu wake mpaka amataje Yesu?Shenzi kabisa!
Kukashifu ni nini?

Na kama mimi imani yangu ni kukashifu ujinga, na imani yako ni ujinga, ukiniambia mimi niache kukashifu imani za watu wengine, wakati mimi imani yangu ni kukashifu imani za kijinga, hapo na wewe hujaikashifu imani yangu?
 
Back
Top Bottom