Jumbe Brown
JF-Expert Member
- Jun 23, 2020
- 12,077
- 12,786
Uamaarufu pekee hausaidii kushinda chaguzi.....Mshambulizi wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba, aliangushwa katika raundi ya kwanza ya upigaji kura wa Urais wa Shirikisho la Soka la nchini Ivory Coast ( FIF) kwa kupata kura 21 huku mahasimu wake Diallo (kura 59) na Diabaté (kura 50)
Katika raundi ya pili, Idriss Diallo, mfanyabiashara na mjumbe mkuu wa sasa wa FIF, aliibuka mshindi kwa kumuondoa aliyekuwa makamu wa Rais wa FIF Sory Diabaté kwa kura 63 dhidi ya 61
Uchaguzi wa Jumamosi katika mji mkuu wa kisiasa wa Yamoussoukro uliahirishwa mara kadhaa tangu 2020, hasa kutokana na masuala ya kuhusu kustahiki kwa baadhi ya wagombea, huku Drogba akiwa miongoni mwao.
Chanzo: BBC
Chaguzi ni MIPANGO IMARA ...ya muda mfupi na mrefu.....