Dini Dini Dini Dini.....Sasa miye nimeanza kuboreka na hizi threads za dini, Je wewe?

Je, Sehemu ya Dini/Imani Ifungwe au Isifungwe hapa JF?!

  • Isifungwe

    Votes: 14 43.8%
  • Ifungwe

    Votes: 8 25.0%
  • Irekebishwe

    Votes: 10 31.3%

  • Total voters
    32
  • Poll closed .
Status
Not open for further replies.

Na serikali ianze uchunguzi kuhusu baadhi ya madhehebu hapa nchini kwani kuna baadhi yanapotosha ukweli na yatasababisha mgawanyiko nchini...
 
Kwa upande wangu kidogo na-beg kuwa na msimamo tofauti.....!
Mara nyingi watumishi wahubirio kweli huzushiwa maneno ambayo si yao.....! We have to listern to this pastor badala ya kusikia maneno toka kwa RPC,OCD hata KATIBU TARAFA....!
Mengi yamewahi kuzushwa juu ya watumishi wa Mungu kama Z.Kakobe, D. Maboya,Gwajima,Kulola,Lwakatare nk...!
Na katika hili hata jamii inayozunguka hapo inaweza ikawa imepotoshwa vile vile
The only reliable source of this issue is the Pastor himself,elders of the church and current members( sio waasi ambao huweza sema mabaya tu)
Tukishapata haya sasa tunaweza kuwa na ground ya kuanza mazungumzo haya.....! NIMEELEWEKA?
 
Serikali imefanya vibaya maana wanajua haya yaliwahi kutokea uganda basi wangepeleka maaskali kanzu wake mle ndani kudhibiti hali yoyote ile ambnayo ni tofauti. maana Dini ni imani na inawezekana kwa imani na mahesabu ya Dini husika walishauona mwisho wa Dunia kama jinsi wanavyotazamia sio wajinga wale waumini wanafanya wanachokiamini kuwa ni kweli, Namaliza kwa kusema Serikali iwaache tuone huo mwisho ulivyo. Duniani kuna vituko vingi!!!
 
Umesikika Msanii! sasa tulia sikiliza.

Dini tulizonazo tumerithi kutoka kwa wazazi wetu huwezi kuzaliwa na wazazi wakristo na wewe ukawa Mwisilamu ni mwiko, maana mtoto utamlea kwa kumpeleka Madrasa au Sunday School, sasa huko wanafundishwa nini , Vurugu ndio iko hapo. wapo wanaojifunza maadili mema na wapo wanaojifunza ushari kila kukicha badala ya kuchambua kitabu chake anaanza kuchambua kitabu cha mwenzake matokeo ni nini ndio haya tunayoyaona sasa.

Waislamu wanaamini Kuruani imeshuka haikuandikwa hapa duniani, hilo halina ubishi na wakristo hawapingi kwa sababu hawajifunzi kubishana na hawa watu wanapandikizwa ubishi huu ambao sio asili yao. Sasa na wao wakristo wanaposema Yesu ni Mungu ubishi unaozuka hapo utafikiri umewatukana waumini hawa, sijui ni kwa nini wakati wao walisema Kitabu chao kimeandikwa na Mungu na wanaamini hivyo lakini wanashindwa kuamini kuwa Yesu ni Mungu.

JF ina mada nyingi mno ni forum pekee ambayo unaweza ukasoma usiku na mchana bila mada zingine kuziona wala kuzipitia hivyo kusema kwamba wachangiaji wameishiwa hoja ndio maana wamekimbilia kwenye Dini Si kweli NGOJA NIKUPE USHAURI WA BULE USIANGALIE THREAD ZA DINI, UTAKUWA NA AMANI.lakini acha watu waseme tunagundua vingi maana akili ya binadamu hukua kwa kujadiri mambo, na Uhuishwa kwa kusikia na hushituka kwa kuona.
 
Hii section ya dini ifutwe...tunakoelekea ni kubaya..Steve D naye alishatoa mapendekezo kama haya!

Nina wasi2 tunakoelekea na thread za dini!
 
Mimi nadhani section ya dini isifungwe kwa kuwa kwa sasa waislam Tunaongoza kwa hoja motomoto na uwezo wa kutetea dini yetu.Yeyote anayetaka section hii ifungwe ni wazi kuwa kashindwa kutetea anachoamini. Hakuna cha kashfa wala nini hii ni kampeni kabambe inayoendeshwa na walioshindwa kwenye maandiko.
 
Mijadala ya dini endapo itatumika vibaya basi na ifutwe,lakini kama itatumika kelimisha walengwa wa dini husika haina tatizo.Mijadala ya dini isimamie katika kuimarisha misingi ya dini yao na sio kuanza kuanzisha madai ya kwamba dini fulani haifai,hii inaweza kusababisha mfarakano wa mkubwa sana katika jamii.

Ikumbukwe kwamba dini ni imani na kila mtu anao uhuru wa kuabudu anapoona ukweli upo na sio kuanza kukashifu dini fulani kwamba eti haifai.

Mjadala huu usifungwe isipokua kukashifiana kusiwepo kwa kuamini kwamba wote hatuwezi tukaacha uislamu na tukahamia ktk ukristu vivyo hivyo wakristu wote hawawezi wakaacha ukristu na kwenda uislamu.

MUNGU ATUONGOZE KWA HILI.
 
Mimi sikubaliani kabisa na mawazo yako. Kwani naona yanaelekea upande mmoja. Kuna hoja nzito na za maana zilizotolewa ila inaonekana wafuasi wa upande fulani wanapoguswa ndo inakuja hoja ya matusi. Hakuna matusi ila we dare to talk openly. Na kwanza hiyo poll yenu imepitishwa na nani mbona maamuzi ni ya haraka mno wakati wengine wamelala na wengine bado kufika kwenye mitandao?
Acheni hoja zimiminwe na mkishindwa kujibu hoja hizo basi kaeni kimya ama mkubali kushindwa. Hapa hakuna maandamano ila kuna kuheshimu michango ya watu.
 

1. Mimi ni memba wa kudumu kule kwenye zile thread za Deen & Imaan sijaona hizo hoja motomoto unazosema nd. Slave, au labda mwenzangu unasoma maandishi kutoka kulia kwenda kushoto? Mhh..

2. Kwa upande wangu naomba hiyo section ya Deen & Imaan indelee hivyohivyo, najua kuna watu wanakerwa na 'deen'(its actually a cult) & 'mtume' wao muflisi kuanikwa hadharani, wanaleta vituko viingi(wenyewe wanaita ushahidi)..lakini kelele zao tunazidhibiti..taratibu ukweli unaanza kushamiri..
 
Last edited by a moderator:

...Great Stuff SteveD.

Naunga mkono hoja, hako ka section kanaboa!

IMANI kila mtu na yake, ndio maana ikasemwa, "mimi nina Dini yangu, nawe una yako!", ukiona watu wanahitalafiana mpaka wakaanza kutukanana na kudhalilisha dini za wenzao na mitume ujue IMANI ishawapungukia hao!. wanafuata 'USHABIKI', kama wale washabiki wa Lords Resistance Army, Al Qaeda, Kibwetereism, Branch Davidian (waco fire!) nk!!!

nitarudi...
 
...Ndugu, wazo jingine lililonijia kutokana na kuthamini michango ya wale wanaopinga mawazo yangu ya: kufungwa jumla jumla, kufungwa kwa siku kadhaa katika wiki,au lile la kuruhusu mada moja kwa siku kwa member; ni kwamba:

... labda basi wachangiaji wa mada za imani/dini zilizo na msimamo mkali na zenye kuleta utata au kuonekana zinakashifu au kudharilisha imani/dini za wengine - wawekewe mtego maalum; yaani waombe kwa Admin u-membership utakao waruhusu wao kuchangia mada hizo katika mrengo huo, hivyo kuifanya forum ya dini/imani au kipengele chake kiwe cha baadhi ya watu fulani tu. Na kwa maana hiyo kipengele hicho (forum/subforum) isionekane kwa watazamaji na washiriki wa JF kwa ujumla, mithili ya forum ya 'mambo ya kikubwa'. Ambako member ni lazima a-apply kwa admin kuangalia au kupost huko. Ahsanteni.

SteveD.
 
... mithili ya forum ya 'mambo ya kikubwa'. Ambako member ni lazima a-apply kwa admin kuangalia au kupost huko. Ahsanteni.

SteveD.

Hapo utakuwa unakosea mheshimiwa..masuala ya deen na imaan sio optional ya nyongeza..Hapa tunazungumzia na kujadili mustakabali wa roho za watu, iweje tuiweke kihivyo?

Hapo sio mzee..
 
Hapo utakuwa unakosea mheshimiwa..masuala ya deen na imaan sio optional ya nyongeza..Hapa tunazungumzia na kujadili mustakabali wa roho za watu, iweje tuiweke kihivyo?

Hapo sio mzee..

Mtindio, nashukuru kwa hoja yako. Nimetoa wazo hilo kutokana na kuona maneno mengi ya kukashifiana ambayo wewe ukiwa mmojawapo na wengineo wengi wapinzani wako mnayaendekeza. Kwa kweli mara nyingi mimi sioni hekima, unyenyekevu, busara au mwonjo wowote wa ucha Mungu kwenye mengi mnayoshindania. Ndiyo maana nikatoa hilo wazo likiwa mojawapo ya mapendekezo mbalimbali niliyokwishatoa.

Kama nilivyosema kuna baadhi ya mliowachangiaji huko hoja zenu zilizo nyingi zimekaa ki-fundamentalist (naomba mnisamehe kwa kutumia neno hili), hivyo katika kuepusha kuwakwanza wasomaji wengi na wacha Mungu walio moderate, nimependekeza hilo wazo, ya kuwa forum ya dini inaweza kuwekewa subforum yake ambayo mtu itabidi akubaliane na masharti ya kuwa atakachokisoma kule kinaweza kumfedhehesha, kumpandisha jazba n.k. Vitu ambavyo vikiandikwa kwenye majukwaa au kuongelewa kwenye open forum kama vilivyo vingine vitaacha adha mioyoni mwa waumini wengine.

Mtindiowaubongo, kama utakumbuka sawasawa, kabla ya jukwaa la mambo ya kikubwa kulikuwa na jukwaa la games/sports & entertainment, member fulani fulani walikuwa wanajaribu kuweka hata picha za ngono kwenye hilo jukwaa. Mpaka hapo lilipo tenganishwa na kuwa na majukwaa kama matatu hivi, la mambo ya kikubwa, la michezo na la entertainment. Hapa utakubaliana nami kwamba kuna member wengi waliomba ruhusa ya kuweza kuingia kwenye mambo ya kikubwa na kuweza kudiscuss kule without limitations, but at the same time watu tuliwezeshwa kuweka picha zenye rather ya 'ku- entertain' kwenye jukwaa la entertainment na kuepusha shari maana kuna picha nyingine zenye kuintatein ziko off-scale, hivo ni xrated na inabidi pelekwa kwenye mambo ya kikubwa.

Natumaini umenielewa, samahani kwa maneno mengi.

SteveD.
 

Asante kwa reply.

Suala la 'kukashifu' hilo nafikiri tulishalimaliza, kwani kuna kipindi kuna kijimtu aliwa-pump mods ili wa-press ban, niliomba tu-define 'kashfa' na 'matusi', tukashindwa kufikia muafaka..Kama tatizo ni 'kashfa' na 'matusi' ni vyema tulifanyie hili kazi na kuona mwisho wake, kuliko kulifanya jambo la deen na imaan kuwa jambo linastahili passwords na limited access..

Shukrani..
 
Imani za kidini ni zaidi ya vituko vinavyojadiliwa hapa. Japo sijapitia hoja nyingi sana kwa sababu hakuna chakujifunza kwenye hoja hizo, chache nilizopitia hapa hazina uhusiano na kile tunachojaribu kujadili. Hoja nyingi zinajaribu kujadili au kupata majibu ya maswali ya dini za kiislamu na kikristo. Lakini watoa hoja na wajibu maswali wanaandika vituko ambavyo kwa kweli vinashusha hadhi ya Forum, nia ya mijadala na hata kukashifu ukweli wa imani zenyewe. Sidhani kuna haja ya kuvumilia jambo lolote linalopotosha ukweli. Ni hatari kwetu. Wengi wetu tunataka kutumia ubabaishaji wa ufahamu wa juu juu kujaribu kuonyesha kwamba tuna ufahamu mkubwa sana wa maswala ya imani. Na hivyo kubahatisha kutoa hoja au kukashifu dini za wengine bila sababu
Ningeomba kuwakilisha ombi la kufuta mijadala hii ya dini. Ili kama kuna wale walio na haja ya kujua ukweli kuhusiana na maswala ya imani wajifunze kwa wazazi, makanisani, misikitini, vyuoni na kwingineko. Wale walio na imani wabaki na imani zao bila kujisikia kukashifiwa. Kwa kweli sioni uwezekano mkubwa sana wa mtu kumjua Mungu kupitia JF
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…