Dini na Imani ni vitu viwili tofauti kabisa, tusivichanganye!

Dini na Imani ni vitu viwili tofauti kabisa, tusivichanganye!

TRIPLE H

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2013
Posts
651
Reaction score
349
Wakuu,
Habari zenu?
Katika zama na nyakati tofauti tofauti katika maeneo mbalimbali duniani kumekuwepo na mijadala inayohusisha imani na dini na mara nyingi vitu hivi viwili watu wengi wameshindwa kuvitofautisha.
DINI ni mfumo rasmi wa kitaasisi wenye lengo la kusadikisha watu juu ya mambo fulani fulani ya kiroho na kwa kawaida mtu awaye yote anapozaliwa anafuata dini ya wazazi/walezi wake kama ambavyo anafuata ukoo au kabila lao. Anakuzwa katika mentality kwamba dini hiyo ni bora zaidi kuliko dini zingine na walio wengi ukiigusa dini yake wanahamaki mno kiasi cha kutukana, kugombana na hata kupigana ikibidi. Hawa wanaweza kujitoa muhanga kutetea dini yao. Wako kila mahali duniani na wapo kwenye dini zote ulimwenguni.

Imani ni tofauti na dini.
Hii ni hali ya mguso wa ndani anayoipata mtu KWA KUSIKIA na kuanza kuifuatilia kibinafsi ili kuona kama aliyoyasikia ndivyo yalivyo au ni uzushi mtupu!
Mtu huyu hufuatilia kila kitu Kuhusu JAMBO HUSIKA na akijiridhisha UAMUA mwenyewe kutoka ndani KUAMINI juu ya jambo hilo na kulifuatilia ili kujiongezea uzoefu!
Mtu anayeamini kwa uhakika juu ya kitu/mtu/Mungu/mungu fulani SI MWEPESI WA KUBISHANA ila ni mjenzi wa hoja kusadikisha wengine na asipokubaliwa U-RELAX tu pasipo magomvi ya aina yoyote.

Ndio maana watu wa imani zaidi ya moja waliokomaa katika imani zao MARA NYINGI (si mara zote) huweza kuvumiliana na kuishi pamoja kwa amani na upendo, lkn wana-dini/washika-dini waliobobea ni ngumu kuishi pamoja kwa kuwa kila mmoja anaendeshwa na falsafa ya 'Mwamba ngoma.... '

Je, wewe ukijitathmini, unajiona MSHIKA DINI au MWAMINI?

Kuna ushirika, umoja, taasisi, elimu unayoipigania hata ikibidi kughalimu uhai wako mradi kisiguswe au una amini kibinafsi katika kitu/elimu/jambo/supernatural nk kwa namna ambayo hata ukipingwa na kukataliwa kiasi gani unaoana poa tu?

Utaelewa ukitafakari.
 
Mi nachojua ni mtu Aina ya diss-minder fulani tu...kuna muda hata unifanyie upuuzi gani nakucheki tu halafu nakausha basi.

Nadhani hayo mambo ya dini na imani yanategemea sana na Aina fulani ya asili ya mtu husika.

Ukiwa mkorofi hata ukiamini katika imani bado utabakia na ukorofi wako tu na utaonekana hata ukijificha vipi na vivyo hivyo kwa mpole, hata ujichangamshe vipi bado nasaba yako itaonekana wewe ni mpole tu sema unalazimisha ukorofi.
 
Mshana jr usiache kuja hapa, Eiyer usije ukapita pembeni.

Tatzo ni uelewa tu mkuu, mbona kila kitu kiko wazi na wala hakipatani na kingine kabsa.
Imani ni Jambo lingine kabsa huwezi kulifananisha na Dini.

Ukiwa na imani Thabiti kuna faida kubwa mno(Juu ya hicho unacho amini eg.. Mungu)
Unakuwa na amani isioweze kukatishwa na changamoto yyote, unakuwa Na furaha hata kama uko katika katika ya misukosuko mingi ya maisha.
Unaishi maisha yako mbele ya macho ya wengine, Ukiona mtu anabishana kuhusu unachoamini unamchulia mtu asie na ufahamu wa kutosha juu ya unachoamini.
Hutayumbushwa yumbishwa na mfundisho ya akina kiranga&alwattan humu JF ya kusema hakuna Mungu.
Unakuwa na selfdifense dhidi ya mafundisho ya ajabu ajabu.
Unakuwa mtu wa kupenda kujali mambo ya wengine.
 
Maranyingi naona dini ikitumika kueneza/kuelezea imani fulani. Kwa hiyo dini hutoa mwongozo wa namna imani husika inavyopaswa kuamini nawenendo wa kwamini huyo.
 
very true mkuu'' nakubaliana nawe katika hili""
 
In that context, IMANI haiwezi kutenganishwa na DINI. Ukiwa na imani inamaanisha unaamini kwa dhati kabisa moyoni mwako kwamba mafundisho uliyojifunza kutoka katika manuscript fulani (mfano biblia) ni ya kweli. Dini ni simply mkusanyiko wa watu wanaofuata mafundisho ya manuscript/school of thought fulani, ndani yao wapo wenye imani ya kweli, wapo walio sceptical, wapo wasioamini kabisa ila inawabidi wawemo tu kwenye kundi kwa sababu za kiusalama nk
 
Maranyingi naona dini ikitumika kueneza/kuelezea imani fulani. Kwa hiyo dini hutoa mwongozo wa namna imani husika inavyopaswa kuamini nawenendo wa kwamini huyo.
Kwani Biblia/Quran ni vitabu vya kutuelekeza Imani sahihi au ni vitabu vya kuelezea Dini sahihi ni Ipi??
 
Waebrania : Mlango 11

1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.
Sijawahi kujua uhalisia hasa wa Mstari Huuu.
LEO NIMEUTAMBUA THABITI.
 
Mi nachojua ni mtu Aina ya diss-minder fulani tu...kuna muda hata unifanyie upuuzi gani nakucheki tu halafu nakausha basi.

Nadhani hayo mambo ya dini na imani yanategemea sana na Aina fulani ya asili ya mtu husika.

Ukiwa mkorofi hata ukiamini katika imani bado utabakia na ukorofi wako tu na utaonekana hata ukijificha vipi na vivyo hivyo kwa mpole, hata ujichangamshe vipi bado nasaba yako itaonekana wewe ni mpole tu sema unalazimisha ukorofi.
Ili ndo Jawabu.
 
Maisha ya watu ni siasa

Siasa ni watu, watu wanadini

Bila watu hakuna dini na dini ni imani

Huwezi kuwa na siasa bila watu wenye dini

Na ukiwa na siasa ya watu wenye dini wao wanaimani na dini zao

Ndio maana

1. Rais huapa akiwa ameshika msahafu

2. Mawaziri, wabunge nao huapa wakishika msahafu

Huwezi kutenganisha maendeleo ya watu kutoka wanachokiamini
 
B. Siasa safi huleta maendeleo na amani

Siasa chafu huleta machafuko, kuzorota kwa uchumi na kutoweka amani

Ikifikia kutafuta amani viongozi wakiroho wanaombwa kuhimiza waumini wao kuienzi amani, kuwa watulivu na kutii viongozi wakisiasa

Kwanini wasikemee pale waonapo wanasiasa wanakengeuka na kuhatarisha amani?
 
C . viongozi wakisiasa ni waumini wa dini
Kama waumini wa dini, lazima watii nakufuata mafundisho ya viongozi wao wakiroho

Viongozi wakiroho wanawajibu
...kuhimiza amani kwa wote watawala na watawaliwa

.....kukemea uovu wa aina yoyote iwe wa wanasiasa au RAIA

Mbona kwenye kuwaombea viongozi wa kiroho wanatumika, vipi katika kukemea uovu tuseme siasa?
 
Tuache kuandika mada zakipumbavupumbavu tukidhalilisha kizazi hiki.

Viongozi wakiroho wakikaa kimya waumini wakachinjwa wote nani atakaenda huko misikitini na makanisani?

Unaanzaje kutenganisha dini na siasa endapo wanasiasa wanaswali Ama wanasali?

Dini na siasa kuvitenganisha nikuwaambia wanasiasa wasiwe waumini, wasiombewe wala wasiombe ushirikiano misikitini wala makanisani

Je inawezekana?
 
Back
Top Bottom