Kwa nini usifanye degree ya mass comunication? Nionavyo mimi japo fani yenu imeingiliwa na makanjanja lkn ukiifanyya kwa kuzingatia weledi basi unaweza kujiajiri mwenyewe na ukapiga hatua kubwa tu.
Kama unakimbilia ualimu ili upate urahisi wa kuajiriwa haraka basi fikiria mara mbili mbili, kuna wenzio wanataka kutoka huko ilhali wewe unataka kuingia.
Hebu fikiria kujiajiri na kutengeneza ajira kupitia hiyo hiyo diploma yako kwanza kisha nadhani ukisoma degree yake utakuwa umeongeza weledi katika kile unachokifanya.
My take. Hakuna furaha ya kweli na uhuru wa dhati unaoweza kuupata kwa kazi ya kuajiriwa. Utakuwa mtumwa tu in one way or another wa kumtimizia mwenzio ndoto zake. Think outside the box mkuu.