Dira ya Taífa 2100 Kwa Maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kisiasa

Dira ya Taífa 2100 Kwa Maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kisiasa

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Anaandika, Robert Heriel

Mtibeli

MALENGO


  1. Kurahisisha maisha ya watu katika uzalishaji na shughuli zao za kila siku.
  2. Kukuza uwezo wa mtu mmoja mmoja kuchangia nguvu, maarifa, ujuzi na kipaji katika ujenzi wa taifa.
  3. Kuboresha na kuhakikisha haki na sheria za kulinda utu wa raia vipo kwa ukamilifu katika katiba.
  4. Kuwaandaa watu na kutunza mazingira na kukabiliana na matokeo ya mabadiliko ya tabia nchi.
  5. Kubadilisha mtazamo wa wananchi katika kuunda ulimwengu wa wakati ujao.
  6. Kuweka mpango wa ongezeko la watu lenye tija.
  7. Kuwa na sera ya taifa kwa kila sekta itakayotumiwa na vyama vya siasa kwa mujibu wa sheria.
  8. Kuyatenga maeneo ya nchi kijiografia kulingana na asili, tabia ya nchi, maumbile ya dunia, n.k. mathalani:
A. Kanda za Kilimo

Patakuwa na kanda za kilimo zitakazotengwa na serikali kwa ajili ya watu, mashirika na makampuni kufanya shughuli za kilimo. Kanda za kilimo zitatengwa kulingana na mazao yanayokubali eneo husika kulingana na tabia ya nchi na udongo. Kanda za kilimo zitabeba mazao yote yanayokubali eneo husika. Kanda ya kilimo cha korosho, nanasi na mihogo inaweza kuwa Mtwara, Lindi, Pwani, na Tanga. Kanda ya kilimo cha matunda Tanga, Morogoro na Mbeya. Kanda ya kilimo cha ndizi, Mbeya, Bukoba na Kilimanjaro, miongoni mwa mazao mengine.

Katika kutekeleza hili, serikali ni lazima iandae mazingira ya kutoleta mvurugano na watu hasa wale wa kipato cha chini. Serikali baada ya kufanya utafiti na kuzitenga hizo kanda itafanya kama ifuatavyo:

I) Kuandaa afisa kilimo wa kutosha kwa kila kata nchi nzima. Kwa kata ambazo zipo mjini hakutakuwa na afisa kilimo. Kila serikali ya mitaa iwe na ofisi ya afisa kilimo. Hapa nazungumzia ofisi zilizo katika maeneo ya kilimo. Maafisa kilimo watakuwa na majukumu ya kuhakikisha kilimo kwa kata yao kinafanikiwa. Hili iliwezekane pawe na afisa kilimo wilaya, mkoa, na taifa. Hawa serikali iandae majukumu yao. Jukumu kubwa ni kuhakikisha kilimo kinafanya vizuri na mazao ya chakula na biashara yanazalishwa kulingana na hesabu walizopewa.

II) Kila mkulima apewe kibali cha kulima kutoka kwa afisa kilimo kata. Kila kata ambayo ipo ndani ya kanda iwe na kibali chake cha kulima mazao fulani. Hivyo kibali kitaeleza ni mazao gani mkulima wa eneo husika anatakiwa kulima. Sio mkulima alime apendavyo bila kufuata kibali kilichowekwa na wataalamu wa kilimo. Mbinu hii italinda zaidi soko la ndani bila kutegemea soko la nje ya nchi. Wakulima wengi hujikuta wanatumia nguvu kubwa kulima kwa jasho na damu na Mungu wakati mwingine huwabariki lakini wanajikuta katika tatizo la soko kwa maana wakivuna wanashangaa kila mtu nchi nzima kavuna mahindi au nyanya na kufanya bidhaa kushuka thamani na wao kupata hasara. Hii ni tofauti na mazao kama korosho ambayo hulimwa katika mazingira maalumu.

III) Miundombinu ya kilimo kuboreshwa nchi nzima. Kuanzia mbolea, dawa, mbegu, mifumo ya umwagiliaji, teknolojia za kisasa za kilimo na upatikanaji wa barabara. Pamoja na maabara ya kilimo kwa kila kanda nchini.

IV) Ikiwa yapo makampuni binafsi ya kilimo yenye viwanda yataona yatahatarishiwa maslahi yao, serikali itaweka na kuwapa utaratibu wa kiwango cha idadi ya mazao yanayotakiwa kuzalishwa kwa mwaka. Kila kampuni lizalishe kulingana na uwezo wake na ikitokea limeshindwa kwa miaka mitatu mfululizo lifutiwe usajili.

V) Wafanyabiashara wa mazao wapewe njia na eneo la biashara na wasajiliwe kwenye mifumo ya kidigitali. Serikali isajili wanunuzi wa mazao na kuwapangia maeneo ya kuuza. Mfano, Taikon nataka kufanya biashara ya mazao, naingia kwenye mfumo maalumu wa serikali najisajili kisha mfumo unanionyesha sehemu gani nikauzie mzigo wangu. Itakuwa kazi ya afisa kilimo kujua kata yake imezalisha kiasi gani cha mazao, wakulima wa eneo husika watamueleza afisa kilimo kuwa wao kila mmoja anakiasi gani anataka kuuza na kipi hakipo kwenye kata husika. Mfumo utakuwa unakuonyesha utoe wapi mzigo ukauze wapi. Na sio watu wapeleke mzigo sehemu mmoja labda Dar huku mizigo mingine ikiharibika kwa kukosa wateja na maeneo mengine kukosa kabisa au kuuziwa nafaka au zao fulani kwa gharama ya juu.

VI) Bei zitawekwa kwenye mfumo na haitaruhusiwa kwa wafanyabiashara kuja na bei yao. Mfanyabiashara ataingia kwenye mfumo na kuona wapi bei anayoimudu na atakayoweza kupata faida.

VII) Serikali kuandaa maonyesho ya kitaifa ya kilimo kwa kila kanda za kilimo. Maonyesho hayo yataambatana na sikukuu ya wakulima.

VIII) Wakulima watakaosajiliwa wataundiwa chama chao, bima yao ambayo zitahusika katika maslahi yao ikiwemo maslahi ya kupewa pensheni kila mwezi watakapozeeka kama wafanyakazi wengine.

IX) Serikali kuweka ghala la chakula la taifa lililoboreshwa.

X) Vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na filamu zenye kuhamasisha kilimo, chakula na lishe bora zitaongezewa nguvu.

Serikali haitafanya kilimo na biashara ila itaweka mazingira wezeshi na rahisi kwa vijana na wote watakaoamua kujiingiza katika shughuli hiyo.

Taifa likishakuwa na chakula moja kwa moja litakuwa na utulivu, amani, na maendeleo. Hatua ya kwanza ya maendeleo kwa binadamu ni kurahisisha upatikanaji wa chakula na sehemu pekee ya kupata chakula ni kwenye kilimo na ufugaji.

B. Kanda ya Ufugaji

Ufugaji wa mifugo kama ng'ombe, mbuzi, kondoo, kuku, bata, sungura, nyuki, samaki, miongoni mwa mifugo mingine ni lazima uwekwe kwa lengo la kutunza na kuhifadhi mazingira na kurahisisha mahitaji ya watu kupata mazao ya mifugo hiyo, na kujipatia kipato.

Nashauri, serikali iweke kanda za ufugaji kwa kuzingatia tabia ya nchi na utamaduni.

Serikali itafanya hivi:

I) Kutakuwa na kanda za ufugaji kwa wafugaji wa kuhamahama. Watachorewa ramani ya wapi pa kulishia mifugo yao. Itakuwa ni kosa kisheria kwa mfugaji au wafugaji au kampuni ya kifugaji kufuga eneo ambalo halijachorwa kwenye ramani ya wafugaji.

II) Serikali itatengeneza mabwawa ya maji yatokanayo na mvua.

III) Serikali itaweka ranchi kuu mbili:

a) Ranchi kubwa - Hii itakuwa porini au nje kabisa ya mji ambapo hakuna muingiliano baina ya mifugo na watu.

b) Ranchi ndogo - Serikali itaanzisha ranchi ndogo ndogo katikati ya majiji ambapo wakazi wa mjini kabisa wanaopenda kufuga watakuwa wakiweka mifugo yao humo. Haitakuwa ruhusa kwa mtu kufuga kuku kwenye nyumba yake akiwa katikati ya jiji. Hizo ranchi ndogondogo zinaweza kupewa hata kampuni binafsi kuziendesha. Wanaokaa nje ya miji ndio watakuwa na ruhusa ya kufuga kuku au bata, au ng'ombe kwa idadi ambayo serikali itaona itafaa ili kutosumbua watu wengine. Litakuwa ni kosa kisheria kusikia sauti ya jogoo akiwika, au kuku au mbuzi au ng'ombe wakizagaa zagaa mitaani katika miji ilhali kuna sehemu ya kuwatunza. Haki za wanyama zitazingatiwa. Ikiwa mtu au kampuni haina uwezo wa kufuga mnyama yeyote haitakuwa ni uhalali wa kufuga kwani itamtesa mnyama huyo na kuleta usumbufu kwa watu wengine.

IV) Kutakuwa na machinjio za kisasa ambapo mifugo itakuwa inachinjwa hapo. Wenye bucha wote sharti wawe wamesajiliwa na chombo maalumu cha serikali.

V) Mazao ya mifugo kama nyama, ngozi, na mifupa yatawekewa bei elekezi.

VI) Wafugaji wote ambao kazi ya ufugaji watakuwa na chama chao, bima yao na uzeeni watakuwa wakipewa pensheni.

VII) Kitaundwa chombo maalumu cha serikali kinachosimamia na kuendesha shughuli za ufugaji wa samaki.

VIII) Vitaanzishwa vituo vya maziwa na wauza maziwa wote wawe wamesajiliwa.

IX) Kutakuwa na masoko yaliyoboreshwa ya mifugo kama kuku, sungura, bata, samaki n.k.

X) Kila eneo lililotengwa kwa mifugo atakuwepo afisa mifugo.

XI) Serikali itajenga maabara na hospitali kwa ajili ya kutibu wanyama na kufanya tafiti.

XII) Kitaundwa chombo cha kusimamia na kulinda haki za wanyama wa kufugwa.

C. Kanda ya Misitu na Uoto wa Asili

Maeneo ya misitu yatakayotengwa yataongezwa. Upandaji wa miti utahamasishwa. Misitu na miti itakua katika makundi mawili:

I) Misitu na miti ya porini pasipokuwa na makazi.

II) Misitu na miti ya kwenye makazi ya watu. Serikali itahamasisha wananchi kupanda miti na kila kata itapewa idadi ya miti ya kupanda kwa mwaka. Kila kata itatenga maeneo ya kuotesha miche ya miti.

Serikali itaongeza maeneo ya misitu kwa:

  1. Kupanda miti ya misitu na maua ya asili katika vyanzo vya maji, na vyanzo vya mito na vijito.
  2. Kupanda miti na maua ya asili katika maeneo oevu, mashamba na mapori.
  3. Kuzuia uharibifu wa miti na maua asilia kwenye vyanzo vya maji.
D. Kanda za Viwanda

Viwanda vitajengwa kulingana na vyanzo vikuu vya malighafi kama vile madini, kilimo, misitu na bidhaa kutoka kwenye mbuga za wanyama pori na vinginevyo.

Serikali itafanya hivi:

I) Kuongeza uwezeshi kwenye elimu ya ufundi na VETA. Hii ni kuhakikisha vijana wengi wanapenda na kujiunga na vyuo hivyo ili baadae wawe na utaalamu wa kutengeneza bidhaa, viwanda vikishajengwa.

II) Kujenga jengo au kugeuza moja ya majengo katika kila mji ambalo mafundi watachukua maeneo na kufanya kazi zao za uzalishaji. Mathalani fundi seremala, fundi cherehani, fundi viatu, fundi magari, fundi hodari wa kutengeneza vifaa vya kilimo kama matrekta, wavuvi wa samaki n.k. hawa wote wawe na jengo lao rasmi.

III) Kila mwaka kuandaa maonyesho ya viwanda vidogo na kutoa tuzo kwa ubunifu na uhodari wa kazi zao.

IV) Serikali kuweka sheria za kodi na vibali rahisi kwa viwanda na bidhaa zinazoagizwa nje ya nchi.

MASOKO, BIASHARA NA UJASIRIAMALI

Serikali itaweka njia rahisi kwa kila raia kufanya biashara au ujasiriamali rasmi na inayolipa kodi.

Serikali itafanya hivi:

I) Tin number itaunganishwa na mfumo wa kifedha wa simu ya kila raia aliyefikia umri wa kulipa kodi. Biashara yeyote ile mtu akifanya kwa kutumia mfumo wa kifedha wa simu kodi itakatwa moja kwa moja na kuingia mfuko wa serikali.

II) Wajasiriamali wote wa kipato cha chini watajisajili katika mfumo huu na serikali itawapa vitambulisho vyao vya biashara.

III) Wajasiriamali wote wanaolipa kodi na wanatumia mfumo wa Tin number watalipwa pensheni wakati wa uzeeni. Watakao shindwa kulipa kodi ya kipato kwa miaka mitatu mfululizo watafutiwa usajili.

IV) Maeneo ya pembeni mwa barabara nyakati za jioni yatatumika kwa wajasiriamali na machinga kwa usimamizi maalumu wa serikali.

V) Kuweka mfumo maalumu kwa madalali, mawakala, wasimamizi na mameneja binafsi. Kwa mfano mnada wa wanyama wafanye kazi zao kwa utaratibu na kila mmoja anayehusika na madalali asajiliwe rasmi na serikali.

VI) Bodaboda hazitaingia highway isipokuwa wenye mafunzo na kupewa leseni ya kuendesha highway.

MAHUSIANO, NDOA NA FAMILIA

Sheria za kudhibiti mahusiano, ndoa na familia zitaboreshwa kwa mujibu wa sheria na haki za binadamu.

Serikali itafanya hivi:

I) Sheria ya ubakaji itabaki palepale adhabu miaka 30.

II) Biashara ya ukahaba iruhusiwe na watakaoifanya wasajiliwe na walipe kodi.

III) Mwanamke kubeba mimba pasipo ridhaa ya mwanaume liwe kosa kisheria. Hili halitawahusu wale waliolewa au walio kwenye uhusiano wa kimapenzi.

IV) Sheria ya kuruhusu kutoa mimba itungwe hasa mimba zilizo katika mazingira maalumu kama ubakaji. Mwanamke aliyechokozwa asitoe mimba kwa ridhaa ya mwanaume wake ni uhalifu na adhabu ya uhalifu huo iwe kali ili kuogopesha.

V) Sheria ya baba atakayeshindwa kutunza watoto apewe adhabu kali.

VI) Kila mwanafamilia sharti afanye kazi. Hii ni kuhakikisha mtu asitegemee kuwa mzigo wa familia nyingine na kumfanya mzazi mmoja kuwa kicheche na kuwa msumbufu wa wengine.

VII) Sheria za kugawa mali zitazingatia mchango wa kila mmoja ndani ya ndoa. Si kweli kuwa mwanamke au mwanaume kugawa mali nusu nusu bila kujua yupi kati yao alikuwa na mchango mkubwa zaidi.

VIII) Haki za watoto wa nje ya ndoa zitazingatiwa kulingana na sheria za asili. Hii ni kusema ni kipi kinachoeleweka ndani ya mila na desturi za eneo husika au jamii hiyo.
 
DIRA YA TAÍFA 2100 KWA MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

MALENGO
1. Kurahisisha Maisha ya Watu katika uzalishaji na shughuli zào za kîla Siku.
2. Kukuza uwezo wa Mtu mmojammoja kuchangia nguvu, maarifa, ujuzi na kipaji katika ujenzi wa taifa.
3. Kuboresha na kuhakikisha Haki na sheria za kulinda ûtu wa raia vipo Kwa ukamilifu katika Katiba.
4. Kuwaandaa Watu na Kûtunza Mazingira na kukabiliana na matokoè ya mabadiliko ya tàbia nchi.

5. Kubadilisha mtazamo WA wananchi katika kuundea ulimwengu wa Wakati Ujao.
6. Kuweka mpàngo wa ongezeko la Watu Lenye Tija

7. Kuwa na Sera ya Taífa Kwa kîla sekta itakayotumiwa na vyama vya siasa Kwa Mujibu wa Sheria.

8. Kuyatenga maeneo ya nchi kijiografia Kulingana na asili, tàbia ya nchi, maumbile ya Dunia n.k. mathalani
A . Kanda za Kilimo.
Patakuwa na kanda za Kilimo zitakazotengwa na serikali kwaajili ya Watu na mashirika na makampuni kufanya shughuli za Kilimo.
Kanda za Kilimo zitatengwa Kulingana na mazao yanayokubali eneo husika Kulingana na tàbia ya nchi na udongo.
Kanda za Kilimo zitabeba mazao yôte yanayokubali eneo husika.
Kanda ya Kilimo cha Korosho, nanasi na mihogo inaweza kuwa Mtwara, Lindi, Pwani, na Tanga.
Kanda ya Kilimo cha matunda Tanga, Morogoro na Mbeya.
Kanda ya Kilimo cha Ndizi, Mbeya, Bukoba na Kilimanjaro. Miongoni mazao mengine.

Katika kutekeleza hili serikali NI lazima iandae mazîngira ya kutoleta mvurugano na Watu hasa wale Watu WA kipato cha chini. Serikali baàda ya kufanya utafiti na kuzitenga hizô kanda itafanya kama ifuatavyo;
I) kuandaa afisa kîlimo wakutosha Kwa kîla kata nchi nzima. Kwa kata Ambazo zîpo Mjini hakutakuwa na Afisa Kilimo.
Kîla serikali ya mitaa íwe na ofisi ya Afisa Kilimo. Hapa nazungumzia ofisi zilizo katika maeneo ya Kilimo. Maafisa Kilimo watakuwa na majukumu ya kuhakikisha Kilimo Kwa kata Yao kinafanikiwa.
Hili ili liwezekane Pawe na Afisa Kilimo Wilaya, Mkoa, na Taífa.
Hawa serikali iandae majukumu yao. Jukumu kûbwa NI kuhakikisha Kilimo kinafanya Vizuri na mazao ya chàkula na biashara yanazalishwa Kulingana na hesabu walizopewa.

Ii). Kîla Mkulima apewe Kibali cha Kulima kutoka kwa Afisa Kilimo Kata.
Kîla kata àmbayo Ipo ndàni ya kanda íwe na Kibali chake cha Kulima mazao Fulani. Hivyo kibali kitaeleza NI mazao gàni mkulima WA eneo husika anatakiwa Kulima.
Sio Mkulima alime apendavyo bila kufuata Kibali kilichowekwa na wataalamu wa Kilimo.
Mbinu hii italinda zaidi soko la ndàni Bila kutegemea soko la nje ya nchi.
Wakulima wengi hûjikuta wanatumia Ñguvu kûbwa Kulima Kwa jasho na damu na Mungu Wakati MWINGINE huwabariki lakini wanajikuta katika tatizo la soko Kwa maana wakivuna wanashangaa kîla MTU nchi nzima kavuna mahindi au nyanya na kufanya bidhaa kushuka thamani na waô kupata hasara.
Hii NI tofauti na mazao kama Korosho àmbayo hulimwa katika mazîngira maalumu.

Iii) Miundombinu ya Kilimo Kuboreshwa nchi nzima. Kuanzia Mbolea, Dawa, mbegu, mifumo ya umwagiliaji, teknolojia za kisasa za kilimo na upatikanaji wa Barabara.
Pàmoja na maabara ya Kilimo Kwa kîla Kanda nchini.

iv) Ikiwa Yapo makampuni binafsi ya Kilimo yenye viwanda yataona yatahatarishiwa maslahi Yao, serikali itaweka na kuwapa utaratibu wa kiwango cha idadi ya mazao yanayotakiwa kuzalishwa Kwa mwaka. Kîla Kampuni lizalishe Kulingana na uwezo wake na ikitokea limeshindwa Kwa Miaka mitatu mfululizo lifutiwe usajili.

V) wafanyabiashara WA mazao Wapewe routes na eneo la biashara na wasajiliwe kwèñye mifumo ya kidigitali.
Serikali isajili wanunua mazao na kuwapangia maeneo ya kuuza.
Mfano, Taikon nataka kufanya biashara ya mazao, naingia kwèñye mfumo maalumu wa serikali najisajili Kisha mfumo unanionyesha sehemu gàni nikauzie mzigo wàngu.
Itakuwa Kazi ya Afisa Kilimo kujua kata yake imezalisha kiasi gani cha mazao, wakulima WA eneo husika watamueleza afisa Kîlimo kuwa waô kîla mmoja anakiasi gàni anataka kuuza na kipi hakipo kwèñye kata husika.
Mfumo utakuwa unakuonyesha utoe Wapi mzigo ukauze Wapi.

Na sio Watu wapeleke mzigo sehemu mmoja labda Dar huku Mizigo mingine ikiharibika Kwa kukosa wateja na maeneo mengine kukosa Kabisa au kuuziwa nafaka au zào Fulani Kwa gharama ya juu.

vi) Bei zitawekwa kwèñye mfumo na haitaruhusiwa Kwa wafanyabiashara kuja na bei Yao. Mfanyabiashara ataingia kwèñye mfumo na kuona Wapi bei anayoimudu na atakayoweza kupata faîda.

vi) serikali kuandaa Maonyesho ya kitaifa ya Kilimo Kwa kîla Kanda za Kilimo. Maonyesho hayo yataambatana na sikukuu ya wakulima.

Vii) wakulima watakaosajiliwa wataundiwa chama Chao, bima Yao àmbayo zitahusika katika maslahi Yao ikiwemo maslahi ya kupewa pension kîla Mwezi watakapozeeka kama wafanyakazi Wengine.

viii) Serikali kuweka ghala la chàkula la Taífa lililoboreshwa.

Ix) Vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na Filamu Zenye kuhamasisha Kilimo, chàkula na lishe Bora zitaongezewa Ñguvu.


Serikali haifatanya Kilimo na biashara ila itaweka mazîngira wezeshi na rahisi Kwa Vijana na wôte watakaoamua kujiingiza katika shughuli hiyo.

Taifa likishakuwa na chàkula Moja Kwa Moja litakuwa na UTULIVU, Amani, na MAENDELEO. Hatua ya Kwanza ya maendeleo Kwa binadamu ni kurahisisha upatikanaji wa chàkula na sehemu pekee ya kupata chàkula ni kwenye Kilimo na Ufugaji.

B. KANDA YA UFUGAJI
Ufugaji wa mifugo kama Ng'ombe, mbuzi, kondoo, kuku, bats, sungura, nyuki, samaki, miongoni mwa mifugo mingine NI lazima uwekwe Kwa lengo la Kûtunza n kuhifadhi mazîngira na kurahisisha mahitaji ya watu kupata mazao ya mifugo hiyo, na kujipatia kipato.

Nashauri, Serikali iweke Kanda za Ufugaji Kwa kuzingatia tàbia ya nchi na ûtamaduni.
Serikali itafanya hivi;

I) kutakuwa na kanda za Ufugaji Kwa Wafugaji WA kuhamahama. Watachorewa ramani ya Wapi pa kulishia mifugo Yao.
Itakuwa ni Kosa kisheria Kwa mfugaji au Wafugaji au Kampuni ya kifugaji kufuga eneo ambalo halijachorwa kwenye ramani ya Wafugaji

ii) Serikali itatengeneza mabwawa ya Maji yatokanayo na Mvua.

iii) Serikali itaweka Ranchi kuu Mbili;
a) Ranchi kûbwa
Hii itakuwa porini au nje Kabisa ya Mji àmbapo hakuna Muingiliano Baina ya mifugo na Watu.

b) Ranchi ndogo
Serikali itaanzisha Ranchi ndogo ndogo katikati ya Majiji àmbapo wakazi wa mjini Kabisa WANAOPENDA kufuga watakuwa Wakiweka mifugo Yao Humo.
Haitakuwa ruhusa Kwa Mtu kufuga Kuku kwèñye Nyumba yake akiwa katikati ya jiji.
Hizô Ranchi ndogondogo zinaweza kupewa hata Kampuni binafsi kuziendesha.

Wanaokaa nje ya miji ndîo watakuwa na ruhusa ya kufuga Kuku au bata, au ng'ombe Kwa idadi àmbayo serikali itaona itafaa ili kutosumbua Watu Wengine.

Litakuwa NI Kosa kisheria kûsikia sauti ya jogoo akiwika, au Kuku au mbuzi au ng'ombe wakizagaa zagaa mitaani katika miji ilhali kûna sehemu ya kuwatunza.

Haki za wanyama zitazingatiwa. Ikiwa MTU au Kampuni haina uwezo wa kufuga mnyama yeyote haitakuwa n uhalali WA kufuga kwani itamtesa mnyama huyo na kuleta usumbufu Kwa watu Wengine.

Iv) Kutakuwa na machinjio za kisasa àmbayo mifugo itakuwa inachinjwa Hapo.
Wenye bucha wôte sharti wawe wamesajiliwa na chombo maalumu cha serikali

V) mazao ya mifugo kama nyama, ngozi, na mifupa yatawekewa bei elekezi.

Vi) Wafugaji wôte AMBAO Kazi ya Ufugaji watakuwa na chama Chao, na watakuwa na bima na uzeeni watakuwa wakipewa pension

vii) Kitaandaliwa chombo maalumu cha serikali kinachosimamia na kuendesha shughuli za Ufugaji wa samaki.
Hii itatoa backup na kuongeza uzalishaji WA samaki Bila kutegemea Bahari, maziwa, mabwawa na Mito.

Viii) Vitaanzishwa vituo vya maziwa na wauza maziwa wôte wawe wamesajiliwa

viii) Kutakuwa na masoko yaliyoboreshwa ya Mifugo kama Kuku, sungura, bata, Samaki n.k.
Serikali itaweka maeneo maalumu Kwa biashara hiyo àmbapo wafugaji au wafanyabiashara wataleta Mifugo Yao ili wateja waweze kuja kununua.

viii) kîla Eneo Lililotengwa Kwa Mifugo atakuwepo Afisa Mifugo

ix) Serikali itajenga Maabara na hospital kwaajili ya kutibu wanyama na kufanya tafiti.

x) Kitaundwa chombo cha kusimamia na kulinda Haki za wanyama wa kufugwa.

C. KANDA YA MISITU NA UOTO WA ASILI.
Maeneo ya misitu yatakayotengwa yataongezwa.
Upandaji wa miti utahamasishwa.
I) Kutakuwa na Misitu na miti ya Porini pasipokuwa na Makazi na
ii) Misitu na miti ya kwèñye Makazi ya Watu.
Serikali itaweka Sheria kîla Mkoa au Eneo angalau úwe na idadi Fulani ya miti.
Misitu na miti ya Makazi ya Watu italenga kutoa hewa Safi, vivuli, na sehemu za starehe na burudani, sehemu za Sanaa kama uigizaji, na kama sehemu ya wanafunzi kujifunza.
MIsitu itapandwa Kulingana Eneo Fulani Kulingana na asili yake, ardhi na tàbia ya nchi.
D. KANDA ZA VIWANDA.
Ili kuwa na connection ya kisekta, viwanda vitajengwa Kulingana na vyanzo vikuu vya malighafi. Hatà hivyo viwanda hivyo vitakavyotegemea chanzo cha malighafi zilipo (extraction of raw materials (primary)),

Viwanda vikubwa vijengwe maeneo maalumu hasa nje ya miji lakini Karibu na bandari(yaweza kuwa Bandari ya nchi kavu au Karibu na Bahari).

Ili kuchochea viwanda;
I) serikali iongeze uwezeshi Kwenye Elimu ya ufundi na Veta.

ii) Serikali ijenge jengo au kugeuzwa Moja ya majengo katika kîla Mji àmbalo mafundi watachukua maeneo na kufanya Kazi zào za uzalishaji.
iii) Serikali kupitia majengo hayo na mfumo utakaoweka uandae kîla mwaka Maonyesho ya viwanda vidogo huku kîla mwaka apewe MTU Tuzo aliyegundua au kubuni au kutengeneza
Bidhaa nzuri yenye tija kwèñye jamii, Watu wadau na Watu watapewa nafasi ya Kúpiga Kura kisha washindi watapewa Tuzo na kiasi Fulani cha Pesa ambacho kitakuza Ndoto za Mhusika aliyeshinda.
Hii itachochea ubunifu na ugunduzi.
Bidhaa zitakazoshinda zitawekwa kisekta ili kîla sekta kuwa na ubunifu

iv) Bidhaa zinazoshinda zipewe Promo ili zitumike kwèñye jamii. Viongozi wakubwa, Baadhi ya Wasanii wakubwa AMBAO wataingia ubia na wizara ya viwanda watakuwa Kazi yao kuzipa promo Bidhaa hizô ili watañzania wapende vyakwao.

v) Sheria za Kodi za kwèñye viwanda na vibali zirahisishwe huku Bidhaa Zinazoagizwa nje ya nchi zichajiwe Kodi kûbwa au zizuiewe kuingia nchini.

MASOKO, BIASHARA NA UJASIRIAMALI.

1. Serikali itaweka njia rahisi Kwa kîla raia kufanya biashara au UJASIRIAMALI.
Hapa njia rahisi inayolengwa na biashara yoyote NI Ile rasmi na inayolipa Kodi.
Biashara au shuguli yoyote isiyolipa Kodi haitahesabika kama biashara au shughuli.

2. Tin number itaunganishwa na mfumo wa kifedha wa Simu ya kîla raia aliyefikia umri WA kulipa Kodi.
Wajasiriamali wote wa kipato cha chini watajisajili katika mfumo huu.
Kama akitoa huduma au akiuza kitu itampasa aingie kwèñye menu ya Simu yake, Kisha malipo ya serikali, Kisha ingiza Tin number yako, Kisha bei ya Bidhaa au huduma uliyouza, jina au Namba ya simu au Tin number ya uliyemuuzia kisha unasend.

Mteja asiyekuwa na risiti au meseji ya aliponunulia itakuwa ni Kosa kisheria na lazima mifano iwepo ili kuwapa Wengine fundisho.

3. Wajasiriamali wote wanaolipa Kodi na wanatumia mfumo wa Tin number utakaondaliwa watalipwa pensheni wakati WA uzeeni.

4. Maeneo ya Pembeni mwa Barabara nyakati za jioni yatatumika kwa wajasiriamali na machinga Kwa usimamizi maalumu wa serikali. Bila uchafuzi Wala kubughuzi watembea Kwa miguu.

5. Serikali itaweka mfumo maalumu Kwa madalali, mawakala, wasimamizi na mameneja binafsi.
Mfano, Madalali real estate, madalali Kazi, madalali WA magari na Vyombo vya Moto,
Mawakala WA real estate, mawakala WA Kazi, mawakala WA Vyombo vya Moto, mawakala WA wachezaji Mpira, mawakala WA mabondia, mawakala na wasimamizi na mameneja WA Wasanii kama wanamuziki n.k.
Mfumo ulinde Haki ya mteja na mtoa huduma Kulingana na mikataba au makubaliano Yao kwa mujibu wa sheria za nchi.
Wote watoe Kodi. Kodi nyingi ziwe Kwa mfumo wa kidigitali ili kupunguza rushwa katikati

6. Bodaboda hazitaingia Highway isipokuwa weñye mafunzo na kupewa leseni y kuendesha Highway.
Atakayevunja Sheria atapewa adhabu Kali ikiwezekana kîfungo kuanzia Miaka 10 huku aliyesabisha ajali na Hana leseni hiyo maalumu akifungwa Maisha Kwa Kosa la mauaji ya kukusudia.
Polisi kata watashughulikia Jambo Hilo.

MAHUSIANO NDOA NA FAMILIA
1. Sheria ya ubakaji itabaki palepale adhabu Miaka 30.

2. Biashara ya ukahaba iruhusiwe na watakaoifanya wasajiliwe na walipe Kodi.

3. Mwanamke kubeba Mimba pasipo ridhaa ya Mwanaume liwe Kosa kisheria

4. Sheria ya kuruhusu kutoa Mimba itungwe hasa Mimba zilizo katika mazîngira maalumu kama ubakaji(Mwanamke kubeba Mimba pasipo ridhaa yake), pia mwanaume kubebewa mimba pasipo ridhaa yake.

5. Sheria ya Baba atakayeshindwa Kûtunza Watoto apewe adhabu Kali.
Lakini hii itakuwa Haki Ikiwa Watoto hao aliwazaa Kwa hiyari Yake. Kama alibebewa mimba bila hiyari Yake Sheria hii haitafanya Kazi.

6. Kîla mwanafamilia sharti afanye Kazi. Mke na Mume lazima wôte wafanye Kazi.
Ikiwa Mume atamzuia Mke kufanya Kazi na Siku akataka kuachana na Mkewe au Mkewe akataka kumuacha Mwanaume huyo atampa Mkewe Asilimia 60% ya Mali zilizokuwepo.

Ikiwa wôte watakuwa wanafanyakazi na Siku ikatokea wakataka kuachana Basi kîla mmoja atapigiwa hesabu Kulingana na kipato chake alichozalisha ndàni ya Ndoa.
Ikiwa mmoja kamuumiza Mwingine Kwa kukusudia labda akitaka kuachana na Mumewe Basi nusu ya Mali alizogawiwa atampa mwenzake kama fidia.
Mfano, Mke kam-cheat Mumewe.
Mumewe kamfumania, alafu akampa talaka.
Mahakama itawagawia Mali kadiri ya walivyochuma kîla mmoja Kisha Yule aliyetenda Kosa mgao wake utagawa nusu na kupewa Mhanga.
Mfano Mume kapewa na Mahakama 60%
Mke kapewa 40%
Alafu Mke ndio kakosea yàani kafumaniwa Basi hiyo 40% itagawanywa nusu Kwa nusu yaani 20% ataongezewa Mumewe kwèñye Ile 60%

Lakini Ikiwa Mume alimzuia Mkewe asifanye Kazi Basi itatumika Ile Sheria ya juu Bila kujali Nani mkosaji.

Ikiwa Mume ndiye kafumaniwa Basi mgawo wake ndîo utakatwa nusu yaani Ile 60% itakatwa na kuwa 30%, Kisha 30% atapewa Mkewe (Mhanga)
Sheria hii inapunguza Kwa kiasi kikubwa Usaliti ndàni ya Ndoa.

Wôte na Yule aliye-cheat na Mke WA Mtu au Mume WA MTU sheria itamfunga jela Kwa Miaka serikali itakayopanga, Taikon ameweka Miaka miwili.

Kahaba hatafungwa Kwa sababu yeye yupo kazini na Hajaenda kushawishi MTU na hahitaji kushawishiwa.
Mke au Mume atakayelala na kahaba atafungwa miezi sita.

Mtoto wa nje ya Ndoa atarithi Kwa Mama yake.
Sheria itakayotumika itahusu Sheria ya asili àmbayo inampa Mamlaka Mwanamke kuamua Mimba iingie au isiingie. Mimba ibaki au isibaki tumboni.Mwanaume hatapewa Mamlaka Wala Hana uhalali WA kuamua Mimba iingie Wala isiingie.

Kuhusu kutumia zana za Kuzuia mimba, kama lengo NI starehe hakuna ulazima WA zana hivyo mwenye mamlaka ya Mimba kuingia au kutokuingia ndio atakuwa na wajibu wa kujilinda.

Mwanamke yeyote àmbaye hajaolewa na HAYUPO kwèñye Ndoa na haishi na Mwanaume Kwa zaidi angalau miezi mitatu akifanya mapenzi na Mwanaume itahesabika wanafanya starehe na Wala lengo Lao halikuwa kuzaa Mtoto.

Ikiwa Mtoto atazaliwa katika mazîngira hayo, Mwanamke ndiye atakuwa na mamlaka na Mtoto huyo. Ataamua aitwe Nani, asomeje, aishije.
Mwanaume hatakuwa na Haki ya kumwita Mtoto wake. Hata akiwa Mkubwa Mwanaume Hana Haki ya Mtoto huyo.

Iundwe Sheria Kali yenye adhabu ya kîfungo Kwa Mwanaume (Baba) àmbaye ataleta usumbufu Kwa mwanamke au Mtoto ambaye hakumlea na aliwatelekeza au Mtoto aliyezaliwa Kwa sababu ya starehe na ambaye hakutaka kumtunza.

Mwanamke akiolewa sehemu àmbayo tayari Mwanaume anafamilia au akaolewa Mke WA pili au Watatu, alafu Mumewe akafa, Mgao wa mali atakaopata ni mali zote zilizochumwa tangu aolewe.
Hatakuwa na Haki ya kugombea Mali Ambazo hakuwepo zikichumwa, ila kama aliowakuta wakimpa Kwa hiyari Yao anaruhusa kuzichukua.

Ikiwa anamtoto mdogo au Watoto, Basi Mali zitagawanywa vivyohivyo Kulingana na mûda aliokuwa kwèñye hiyo Ndoa. Yàani Watoto wake pia hawatapewa Haki Sawa na wale Watoto waliozaliwa kipindi Mali zinatafutwa.

Haitakuwa HAKI kwàke na Watoto wake kupewa Sawa na wale aliowakuta. Huo utakuwa unyonyaji na dhulma.

Ikiwa Mwanamke MTU Mzima mwenye Mali akaamua kuolewa na Mwanaume Mwingine au kijana, alafu huyo Mwanamke anawatoto, alafu akafa Kwa ghafla Bila kuandika wosia, Mwanaume huyo mgeni hatakuwa na haki ya Kurithi Mali zote alizozikuta atawaachia Watoto au familia ya Mwanamke. Yeye atapewa tuu vizawadi na Yale yaliyochumwa tangu alipoingia kwèñye hiyo Ndoa.

Ikiwa Mlikuwa kwèñye Dini Moja wewe na Mkeo/mumeo au Mlikuwa na Dini tofauti lakini mkaridhiana muishi pàmoja hivyohivyo alafu ikatokea mmoja wenu akabadili Dini ñyiñgine àmbayo mmoja haridhii, huyo aliyebadili Dini ndiye atahesabika kama chanzo cha mgogoro na endapo mtataka kugawa Mali, mkishagawana aliyeanzisha mgogoro ndiye Mgao wake utakatwa Nusu.
Kwa sababu ameenda kinyume na makubaliano mliyokuwa mmepatana tangu awali.

Itakuwa Haki Kwa Mzazi kumkataa Mtoto na kwenda Mahakamani kutaka Mtoto huyo asitumie majina yake ikiwa Mtoto huyo ameasi maadili ya Baba yake.

Halikadhalika Mtoto akikua Mkubwa anahaki ya kutotumia majina ya Baba yake.

Ikiwa Mzazi amemlea Mtoto awezavyo na vile aonavyo, Mtoto akataka ziada ya Mzazi amlee kadiri ya maono yake(maono ya Mtoto) Mzazi anahaki ya kuandikishana na mtoto kuwa Siku akifanikiwa amlipe kiwango fulani watakachopatana.
Ikiwa Mzazi atamlea Mtoto vile Mzazi aonavyo hatakuwa na Haki ya kumlipisha Mtoto huyo. Mtoto atafanya Kwa hisani.

Mama na Baba watakapotengana watawajibika Kutoa nusu Kwa nusu Pesa ya matunzo Kwa Watoto.
Kwèñye Ndoa Hakuna Haki Sawa lakini nje ya Ndoa kûna Haki Sawa.

Wanandoa wakishaachana Hakuna àmbaye atakuwa na wajibu Kwa mwenzake isipokuwa Kwa Watoto tuu.
Yàani Mwanaume hatamtunza Mwanamke Wala Mwanamke hatamtunza Mwanaume labda Kwa hiyari Yao.

Ikiwa kuna Mtoto wa nje unampenda, na unàtaka umfanyie mazuri NI Vizuri umuandikishe Mali mapema ukiwa hai Kwa sababu hatakuwa na Haki Sawa na hao wa ndàni ya Ndoa yako. Na ikiwa anayohaki hiyo Basi hata Watoto WA Mkeo AMBAO siô wako wanayohaki hiyohiyo katika Ndoa Yenu.

Kisheria Hakuna Ndoa yako au familia yako, au Nyumba yako ila kûna familia Yenu yàani wewe na Mkeo/mumeo.
Ndio maana kile àmbacho utataka kukifanya Kwa Mtoto wako WA nje elewa kuwa hata Mke wako Mtoto wake àmbaye hajazaa na wéwe anahaki hiyohiyo.

VIONGOZI NA UTAWALA

1. Kiongozi yoyote lazima apatikane ndàni ya Ndoa. Kiongozi Halali.
Ingawaje hii itaonekana kuwatenga Watoto na Watu waliozaliwa nje ya Ndoa au Kabla ya Ndoa Kwa kuonekana hawana Makosa zaidi ya Makosa ya Wazazi waô lakini Akili Kiongozi yoyote atokane na Ndoa.
MTU asiyetokana na Ndoa anaweza kuhudumu katika Kazi zingine za utumishi lakini siô kuwa Kiongozi.

2. Kiongozi yeyote lazima awe na Familia. Yàani awe Mke au Mume WA MTU.
Kiongozi ambaye Ndoa yake itavunjika na sababu ikawa yeye atapoteza Sifa ya kuwa Kiongozi wa Umma

3. Katiba ya Nchi iwafanye Watu wôte wawe Sawa na kutoa Haki Kwa wôte.

4. Chama Kiwe Kimoja lakini kwèñye chaguzi ndîo wagombea wawe wengi weñye mirengo tofauti.
Demokrasia ya chama Kimoja Kwa nchi inayoanza na Maskini NI nzuri kuliko Demokrasia ya vyama vingi.

5. Rais ashtakiwe kama Watu Wengine Ikiwa atatenda Kosa,.

6.,

7.


Ngoja kidôgo

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
Wewe wataka kuturudisha kwenye ujamaa, hizo ni fikra za ki-communist kumpagia binaadamu la kufanya kama mnyama, tuko kwenye free market economy, kwanini unipangie zao la kulima?
 
Back
Top Bottom