Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Vigwaza kimeadhimisha miaka 48 ya kuzaliwa kwake, huku kikitoa wito wa kuepuka ubaguzi katika mchakato wa uchaguzi mkuu.
Mwenyekiti wa chama hicho, Athumani Kimui, ameeleza kuwa CCM haikubali kuwepo kwa ubaguzi baina ya wanachama wake, akisisitiza kwamba uchaguzi wa viongozi unapaswa kufanywa kwa kuzingatia sifa zao, badala ya kutegemea vipengele vingine vya kibaguzi.
Kimui ameongeza kuwa chama hicho, tangu kuanzishwa kwake, hakijawahi kuwa na ubaguzi, na amesisitiza kwamba jambo hili linapaswa kuendelea kulaaniwa. Amesisitiza pia umuhimu wa vikao vya chama vinavyopangwa kwenye kalenda rasmi, kwani vikao hivyo vitasaidia kuimarisha chama, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Vigwaza kimeadhimisha miaka 48 ya kuzaliwa kwake, huku kikitoa wito wa kuepuka ubaguzi katika mchakato wa uchaguzi mkuu.
Mwenyekiti wa chama hicho, Athumani Kimui, ameeleza kuwa CCM haikubali kuwepo kwa ubaguzi baina ya wanachama wake, akisisitiza kwamba uchaguzi wa viongozi unapaswa kufanywa kwa kuzingatia sifa zao, badala ya kutegemea vipengele vingine vya kibaguzi.
Kimui ameongeza kuwa chama hicho, tangu kuanzishwa kwake, hakijawahi kuwa na ubaguzi, na amesisitiza kwamba jambo hili linapaswa kuendelea kulaaniwa. Amesisitiza pia umuhimu wa vikao vya chama vinavyopangwa kwenye kalenda rasmi, kwani vikao hivyo vitasaidia kuimarisha chama, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.