Dj Fetty atangaza rasmi kuacha kazi ya Utangazaji

Dj Fetty atangaza rasmi kuacha kazi ya Utangazaji

Councillor Salaah, boss wake mwanaFa mmiliki wa Silent Ocean wasafirishaji wakubwa wa mizigi toka China Kuja TZ..》》》》》SwaliJingine?

Mhuuhh!! Ok! Nikajua haliwi, amekaa ki 'tomboy'.
 
Anaenda kuolewa mke wa pili na saleh yule wa home shopping centre,yule wa china

Hata sio mke wa pili, salehe ana vimada kibao dunia nzima,anaweza akawa hata mke wa 10 maana wengine pia watakuwa wameolewa kisirisiri wakaambiwa ni wake wa pili....
 
Sijawahi kumkubali huyu dada hata siku moja panoja na redio yao hiyo.....

Milard Ayo akiondoka kipindi chake atapewa Fredwaa...

Wee lazima utakua msukuma...nawajua wasukuma kwa kupenda vitu vya kizee zee
 
ktk soko huria kubadili kazi ni jambo la kawaida sana, wafanyakaz wa umma tu ndio wanashangaa mamabo ya mtu kuhama kazi ila awe makini sana wasije ondoka kwa mbwembwe wakaishia kama kina maulid kitenge kaondoka yey ndo kapotea masikion mwa watu
 
ktk soko huria kubadili kazi ni jambo la kawaida sana, wafanyakaz wa umma tu ndio wanashangaa mamabo ya mtu kuhama kazi ila awe makini sana wasije ondoka kwa mbwembwe wakaishia kama kina maulid kitenge kaondoka yey ndo kapotea masikion mwa watu

Maulid Baraka wa kitenge sijamsikia mda mrefu si yuko RadioOne now?
 
watangazaji nao n kama wacheza mpira ,kila kukicha n transfer ili mladi dau likifika.
 
Dj Fetty kwa habari nilizodokezwa kutoka ndani ya Uhai media! Azam wamefikia dau atakuwa ndani ya studio za radio za azam media!! radio itakayo kuwa hewan mda si mrefu!

Ayo mtu wa watu nae yupo mbioni kutimka! so stay tune
aibu yako
 
Dj fetty ametangaza kuachana na utangazaji na kuwa Mjasiriamali kuanzia leo

==================

View attachment 287209

SURPRISE!
Aliyekuwa mmoja wa watangazaji wa kipindi maarufu cha burudani XXL cha Clouds FM, Fatma Hassan &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];Dj Fetty' leo Sept.15,2015 amewaaga rasmi wasikilizaji na wafanyakazi wenzake kwa madai ya kuachana na kazi ya utangazaji ili kuendeleza biashara zake mpya (Duka la Nguo la Fettylicious lililopo Dar free market).

Siku kadhaa zilizopita, Mwanachama mmoja wa JamiiForums katika jukwaa la Celebrities alihoji kuhusu ukimya wa Dj Fetty kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, hakika leo majibu yake yamepatikana!

Fetty amesikika kwenye kipindi hicho leo kwa mara ya mwisho kama sehemu ya kusema kwaheri.

Mtangazaji mwenza, Adam Mchomvu alipojaribu kuchombeza kwa kumhoji Dj fetty ni sababu ipi iliyomfanya aamue kuacha kazi yake ya muda mrefu kwa ajili ya biashara ya duka la nguo lililoanza juzi tu, huku akitolea mfano wa duka la Born 2 Shine lililoanza muda mrefu lakini mmiliki wake (B12) hakufikia uamuzi wa kuacha kazi, Fetty akajibu kwa ufupi tu kuwa 'majukumu hayafanani' na kila mtu ana namna anavyoshughulikia majukumu yake.

Katika hatua nyingine, kwa masikitiko makubwa mtangazaji huyo mahiri na mwenye mvuto wa kipekee katika utangazaji wa kizazi kipya alionekana mwenye majonzi na alishindwa kujizuia kutoa machozi na kufikia hatua ya kuvaa miwani ili kuficha taswira ya huzuni aliyonayo!


Pia, kuonyesha ni namna gani ameguswa na kuondoka kwa Dj Fetty, B-Dozen amekaririwa akisema,"Nakupenda sana fettythebest na siku ukitaka kuja kwenye [HASHTAG]#Xxl[/HASHTAG] we niambie utakuja tu mana bado tunakuhitaji".

Kipindi cha XXL ambacho huongozwa na B Dozen akishirikiana na Adam Mchomvu sasa kimepata member mpya, Kennedy The Remedy aliyechukua nafasi ya Fetty akitokea East Africa Radio (The Cruise).

Kennedy The Remmedy ameungana rasmi na familia ya XXL.
Itakuwa MAPEDESHEE washaafika BEI...Mtoto mzuri kama huyo ni wa kuwekwa ndani na kupata HUDUMA bila jasho....

Mungu amsimamie katika majukumu yake mapya..
 
Back
Top Bottom