Djigui Diarra ataendelea kuwa kipa bora, kwa sasa hana mpinzani!

Djigui Diarra ataendelea kuwa kipa bora, kwa sasa hana mpinzani!

Majok majok

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2023
Posts
783
Reaction score
2,057
Kuna vimaneno vimeanza kusambazwa na mbumbumbu kuanza kumfananisha Diarra na kipa wao Ayoubu Lakred!

Anayeweza kuwalinganisha wawili hao kwa sasa kwa maana ni Kama unalinganisha kichuguu na mlima!

Unamlinganisha kipa aliyefanya vizuri kwenye mechi 3 dhidi ya kipa aliyeonyesha ubora wake miaka 2 mtawalia!

Ukienda kwenye rekodi bado Ayoubu ni cha mtoto mbele ya Diarra, Diarra kaisaidia timu yake kucheza fainali ya kombe la shirikisho barani Afrika akiwa na kiwango Bora kabisa na akiwa ni miongoni mwa makipa wa kisasa!

Kachaguliwa na caf kuwa miongoni mwa makipa 10 Bora wa afrika utamlinganishaje na Ayoubu?

Mambo ya kucheza kwa kiwango Cha juu Diarra ni mambo anayoyafanya Kila mechi na imeshakuwa kawaida kwake ndio maana ikitokea akacheza vibaya mechi moja lazima ajadiliwe, habari za kuokoa penalty kwenye hatua muhimu kwake siyo story Tena ishakuwa ni kawaida kwake na ashathibitisha ilo!

Unapataje ujasiri wa kuanza kuwalinganisha hawa wawili? Misimu 2 mfululizo kaisaidia timu yake kubeba ubingwa wa Tanzania akiwa na kiwango Bora uku akiibuka kuwa kipa Bora wa msimu!! unaanzaje kuweka mlinganisho?

Nenda kaangalie timu ya Taifa ya Mali kikosi chote kina wachezaji 2 tu wanaocheza barani Africa na mojawapo ni Diarra kutoka yanga! Waliobaki wote wanakipiga ulaya kwenye timu kubwa kubwa!

Nafikiri kiwango Cha uelewa wa mpira tunatofautiana Kuna wale bendera fuata upepo mashabiki oya oya walioujulia mpira ukubwani, na Kuna wale wazee wa mihemko, pia Kuna wale wanaojua lakini wanajizima data ili wasionekane tu wanampa maua yake kwa kuwa Yuko yanga!

Lakini pia huwezi kumlinganisha mchezaji aliyecheza si zaidi ya mechi kumi na baadhi yake akiwa kafanya vizuri mechi 4 halafu umuweke fungu moja na aliyecheza misimu 2 kwa ubora utakuwa una kichaa Cha mbwa!
 
Ayoub Lakred na Diarra hawawezi kufanana kwa vitu vingi tu, kuanzia profile zao kimpira, bei zao sokoni, mishahara yao, na viwango vyao. Hebu niambie, ukiachana na ligi ya bongo huyo Diarra kafanya nini huko alikotoka?

Kama tunamsifia Diarra kwa kuangalia alichokifanya haoa bongo, basi hata kwa Ayoub tuangalie anafanya nini kwa hapa bongo (bila kuangalia kacheza mechi ngapi)

Kwa vigezo hivyo vichache tu hapo juu, Ayoub Lakred amemuacha mbali sana Diarra.
 
Yeyote anayeweza kuthubutu kumuweka Diarra na Ayoub kwenye mzani mmoja hana akili timamu & haujui mpira.

Jana Diarra kaniinua kwenye kiti mara 2, ile save ya dunia kwenye one on one na mchezaji wa Medeama na ile penalty!
Na ndiye man of the match.

Bila zile save 2 huenda tungekuwa tunaongea mengine huku matumaini ya robo fainali yakiishia palepale kwa Mkapa.
 
Ayoub Lakred na Diarra hawawezi kufanana kwa vitu vingi tu, kuanzia profile zao kimpira, bei zao sokoni, mishahara yao, na viwango vyao. Hebu niambie, ukiachana na ligi ya bongo huyo Diarra kafanya nini huko alikotoka?

Kama tunamsifia Diarra kwa kuangalia alichokifanya haoa bongo, basi hata kwa Ayoub tuangalie anafanya nini kwa hapa bongo (bila kuangalia kacheza mechi ngapi)

Kwa vigezo hivyo vichache tu hapo juu, Ayoub Lakred amemuacha mbali sana Diarra.
Tuambie uyo ayoubu kafanya Nini hapa bongo Kama unavyosema tuanzie hapo na sisi tukuambie diarra kafanya Nini hapa bongo!
 
Diarra inabidi tumpe tu mke, mwanamke wa kitanzania kama Zawadi.
Anaupiga mwingii!
 
Ayoub Lakred na Diarra hawawezi kufanana kwa vitu vingi tu, kuanzia profile zao kimpira, bei zao sokoni, mishahara yao, na viwango vyao. Hebu niambie, ukiachana na ligi ya bongo huyo Diarra kafanya nini huko alikotoka?

Kama tunamsifia Diarra kwa kuangalia alichokifanya haoa bongo, basi hata kwa Ayoub tuangalie anafanya nini kwa hapa bongo (bila kuangalia kacheza mechi ngapi)

Kwa vigezo hivyo vichache tu hapo juu, Ayoub Lakred amemuacha mbali sana Diarra.
Master taja eneo tukamjengee rage mnara wake
 
Ayoub Lakred na Diarra hawawezi kufanana kwa vitu vingi tu, kuanzia profile zao kimpira, bei zao sokoni, mishahara yao, na viwango vyao. Hebu niambie, ukiachana na ligi ya bongo huyo Diarra kafanya nini huko alikotoka?

Kama tunamsifia Diarra kwa kuangalia alichokifanya haoa bongo, basi hata kwa Ayoub tuangalie anafanya nini kwa hapa bongo (bila kuangalia kacheza mechi ngapi)

Kwa vigezo hivyo vichache tu hapo juu, Ayoub Lakred amemuacha mbali sana Diarra.
[emoji2961]
 
Yeyote anayeweza kuthubutu kumuweka Diarra na Ayoub kwenye mzani mmoja hana akili timamu & haujui mpira.

Jana Diarra kaniinua kwenye kiti mara 2, ile save ya dunia kwenye one on one na mchezaji wa Medeama na ile penalty!
Na ndiye man of the match.

Bila zile save 2 huenda tungekuwa tunaongea mengine huku matumaini ya robo fainali yakiishia palepale kwa Mkapa.
Save nyepesi sana ile uliamua kunyanyuka kwenye siti kwa emotions zako tu.
 
Ayoub Lakred na Diarra hawawezi kufanana kwa vitu vingi tu, kuanzia profile zao kimpira, bei zao sokoni, mishahara yao, na viwango vyao. Hebu niambie, ukiachana na ligi ya bongo huyo Diarra kafanya nini huko alikotoka?

Kama tunamsifia Diarra kwa kuangalia alichokifanya haoa bongo, basi hata kwa Ayoub tuangalie anafanya nini kwa hapa bongo (bila kuangalia kacheza mechi ngapi)

Kwa vigezo hivyo vichache tu hapo juu, Ayoub Lakred amemuacha mbali sana Diarra.
Pia ngoja nikupe wasifu wa diarra uko alikotoka na wewe utupe wasifu wa uyo ayoub wako uko alikotoka ili twende sawa Kama unavyotoka;

DJIGUI DIARRA kafanya yafatayo alikotoka;
-kacheza kombe la Dunia under20 timu ya Taifa ya Mali akiwa kipa namba 1, na kuiwezesha kufika nusu fainali uku akidaka penalty 2 kwenye robo fainali dhidi ya ujerumani!

-Amecheza fainali AFCON under23 akiwa kipa no.1 wa timu ya Taifa ya Mali!

-kwenye tuzo za caf 2015 aliorodheshwa kwenye (5)Bora ya magolikipa Bora chipukizi barani Africa!

-Diarra kacheza timu ya Taifa ya wakubwa 2016 CHAN na kuisaidia timu ya Taifa ya Mali kutinga hatua ya fainali dhidi ya congo uku diarra akipangusa penalty 3 katika mechi 6 alizocheza kwenye michuano iyo!

-2020 diarra aliisaidia timu yake ya Taifa ya Mali kutinga Tena fainali ya CHAN walicheza dhidi ya Morocco na kuweka rekodi ya kucheza dk 365 bila kuruhusu goli ikiwemo kupangusa penalty muhimu kwenye hatua ya nusu fainali dhidi ya guinea!

-diarra kacheza hatua ya 16 Bora michuano ya AFCON mwaka 2019 akucheza mechi zote kwa dk 90!

-Diaara akiwa kwao aliondoka akiwa amebeba makombe 5 ya LIGI kuu Mali, makombe 2 ya Mali super cup, makombe 3 ya Malien cup(FA),

Nafikiri nasubilia pia utuletee cv ya bwana lakred uko alikotoka alichokifanya kabla atujakuletea wasifu wa Diarra hapa alipo na alichokifanya!
 
Back
Top Bottom