Dk. Kalemani: Serikali imetoa mabilioni kujenga maktaba kubwa kabisa ya hadhi ya Kanda ya Afrika Mashariki Chato

Yaani mambo ya ajabu kabisa
 
Mkataba kubwa yenye hadhi ya kanda ya Africa wakati zile za mkoa zimekufa kwa kukosa ukarabati, maboresho na ubunifu ili tupate vitabu vya maana
Hakika, maktaba nyingi zimechoka sana
 
BASI HAPO WASOMI WA MFUMO KRISTO MENO YOTE NJEE WANASHANGILIA TUH WAKAIBE PESA ZA WALALAHOI,ILA HAZITAWAPELEKA POPOTE PESA ZA DHULMA HIZO
 
Angeomba Kiwanda cha kuchakata na kusindika mazao wanayozalisha
 
Hiyo Maktaba ni moja ya agenda ndani ya ilani ya CCM, ama Wananchi ndo wameomba. Au ndo tuseme ni matakwa ya viongozi!
 
Asante Kalemani miaka 10 imekutosha 2025 mpishe Joseph J.M...naona familia sasa imekuchoka
 
Nikiskia jina KALEMANI
Nayaskia Maumivu tunayopitia tanesco[emoji29]
 
Unaweza kukuta Chato inakabiliwa na changamoto kubwa ya maji safi lakini mbunge wao bado haoni kuwa hicho ndicho kinapaswa kuwa ndiyo kipaumbele cha wananchi wake!

Katika ulimwengu wa e-books bado mbunge anataka ujenzi wa maktaba kubwa ya vitabu. Kwa hiyo "open cheque" aliyopewa angeliomba hata ujenzi wa chuo chenye hadhi ya kitaifa basi! Karaghabao!
 
Tatizo letu ni kutazama leo na kudhani kuwa maisha yanaisha kesho. Huko KIlimanjaro panasifika kwa kuzalisha wasomi nchi, umeshajiuliza miaka ile ya sitini na sabini palikuwa katika hali gani kielimu?.

Na sio Chato penye kujengwa maktaba kubwa, upo mpango wa kujenga chuo kikuu kikubwa kule Bukoba.

Elimu siku zote inafungua eneo duni na kulipatia vijana wenye maono na ujeuri wa kutaka kulibadilisha kiuchumi.
 
E-books haiondoi umuhimu wa kujenga maktaba au chuo kikuu. Dodoma hawajui umuhimu wa e-books?. Mbona kuna UDOM?.
 
Kule chato watu wanaojua kusoma hata robo hawafiki, wengi tabularasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…