Dkt. Bashiru piga moyo konde na usonge mbele

Dkt. Bashiru piga moyo konde na usonge mbele

Team JPM

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2018
Posts
1,197
Reaction score
1,826
Wakati nasoma chuo kikuu cha Dar es salaam enzi zile Hayati Dr.

Magufuli akimalizia masomo yake ya Shahada ya Uzamivu, nilimtambua Dkt Bashiru kama Msomi, Mzalendo, Mjamaa na mpenda mabadiliko ya dhati kwa maendeleo ya wananchi.

Kamwe sikutarajia kama IPO siku Dkt Bashiru atakuwa sehemu ya Chama tawala wala Serikali iliyopo madarakani maana viongozi wenzake wangempinga na kumtenga kutokana na imani na itikadi yake ya kuwakomboa watanzania kutoka katika umasikini, rushwa, maradhi na ujinga.

Naamini 100% kwamba Dkt Bashiru pia hakuwahi kufikiria kugombea vyeo vya kisiasa wala nafasi za uongozi.

Hulka yake, uzalendo wake na uchapa kazi wake ndizo tunu zilizomgusa JPM hadi kumuona kama msaada mkubwa katika kurudisha nidhamu ya chama na uwajibikaji wa chama kwa wananchi. Kazi hiyo aliifanya vyema na kurejesha nidhani, Hadji na sifa ya chama katika jamii.

Mafanikio ya Bashiru katika Chama, yalimuaminisha Mheshimiwa Hayati JPM kwamba Bashiru anafaa kuziba pengo LA katibu Mkuu Kiongozi
Hakika ni kwamba uteuzi wa Bashiru kushika Ukatibu Mkuu wa Chama, uliwashangaza wengi kama ambavyo pia uteuzi wa Bashiru kuwa Katibu Mkuu Kiongozi ulivyowashtua wengi.

Leo hii, mheshimiwa Rais Samia ametengua uteuzi huo kwa kumteua katibu Mkuu Mwingine na Kumteua Dkt Bashiru kuwa Mbunge.

Mheshimiwa Bashiru, hiki ni kipimo cha ukomavu na weledi ndani ya kipindi kifupi.

Kuwa na moyo thabiti na utulivu wa nafsi na kukubaliana na hali. Endelea kuchapa kazi kwa weledi, usithubutu kuungana na kundi lolote, simamia msimamo wako.

Tambua pia kwamba, mabadiliko makubwa uliyoanzisha katika chama yamekujengea chuki na uhasama mkubwa kwa mafisadi ndani na nje ya chama. Unapaswa kuchukua tahadhari zote za msingi.

Baada ya mtikisiko mfupi, utazidi kuwa imara zaidi na nyota yako itang'ara. Kila LA kheri katika Majukumu yako ya Kibunge, saidiana na Mh. Polepole kukiimarisha chama na kumuunga mkono kwa dhati Mama Yetu Samia Suluhu Hassan. Uamuzi wake usikurudishe nyuma, Songa Mbele
 
Ngojeni uchunguzi wa special Audi ya BOT nyie team Jiwe ndio muanze kujitetea! Huko nyuma mwalimu enzi zake alikuwa na wafuasi wengi lakini baada ya kufa wengi wao waliikana imani yake ya ujamaa!!! Kwahiyo Jiwe hatakuwa wa kwanza kukanwa!!! Chama chenu ni cha wanafiki. Bashiru sasa anaisoma namba!!!
 
Ngojeni uchunguzi wa special Audi ya BOT nyie team Jiwe ndio muanze kujitetea! Huko nyuma mwalimu enzi zake alikuwa na wafuasi wengi lakini baada ya kufa wengi wao waliikana imani yake ya ujamaa!!! Kwahiyo Jiwe hatakuwa wa kwanza kukanwa!!! Chama chenu ni cha wanafiki. Bashiru sasa anaisoma namba!!!
Hakuna siku nilifurahi kama leo mzee wa kuitumia dola kutawala leo hii kasukumizwa akabishane na kina Jah people na Kibajaji na Msukuma Kasheku
 
Tumpe muda Mh. Rais achape kazi, ateue timu anayoamini itamsaidia, tusimlaumu. Naamiini kuwa mh. Rais anafanya hivyo kwa nia njema kabisa.
 
Bashiru kupata Ubunge pekee haitoshi ilipaswa Awekwe pembeni sehemu ili upite uchunguzi makini sana na shaka hata na Uraia wake, Ilikuwaje Magu amfanye msimamizi wa watumishi wote TZ, hii inanipa ukakasi tungejikuta kila sehemu kuna wageni. Mama Samia kwa kweli tuna imani kubwa sana na wewe Mheshimiwa Rais
 
Asante sana Mh. Rais Samia Suluhu Hassan. Hakika kazi kubwa ya kumtoa Bashiru hapo Ikulu imekuongezea heshima kubwa mno. Nimefurahi mno unaepuka watu walioshiriki kwa kiasi kikubwa kuharibu Amani na Demokrasia Tanzania, kutesa watu na mambo mengi makubwa. Walioshirili kikubwa mno katika udikteta na ukandamizaji wa demokrasia. Walioshiriki na kutoa mbinu chafu za kugawa Tanzania kwa ukanda na ukabila. Mama yetu mpendwa RAIS leo umeliheshimisha Taifa la TANZANIA.

Mungu aendelee kukupa utulivu na umakini uendelee kusafisha na kupanga safu yako vizuri mno. Chanda chema huonekana Asubuhi. Hakika wewe ni chanda chema. Ninaiona Tanzania mpya ya Amani na FURAHA tena kwa watu wote na si kwa kikundi au kanda au kabila fulani. Mh. Rais wekeza pia juhudi katika kurejesha amani na Mshikamano bila kukali huyu katoka kanda ipi, kabila lipi na dini ipi.
Nimefurahi na Diplomasia umeitendea haki kabisa kwa kuangalia weledi. Tanzania mpya ndani na nje ya nchi.

I salute you Her Excellency, Samia Suluhu Hassan. May you be protected by Allah.
 
Hakuna siku nilifurahi kama leo mzee wa kuitumia dola kutawala leo hii kasukumizwa akabishane na kina Jah people na Kibajaji na Msukuma Kasheku
Mkuuu kufurahia Mabaya ya mwenzako ni dalili mbaya sana na ni hulka ya Kimaskini na inatupa picha kwamba wewe ni mtu wa aina gani.
Kikubwa tumwombee Bashiru apokee mabadiliko haya kwa mtazamo chanya. Kwa wanaomfahamu Bashiru tangu akiwa Department ya Political Science pale the Hill watakuwa mshahidi kwamba Kilichomponza Bashiru ni Nidhamu yake na Usikivu wake kwa Boss wake. Mhe. Balozi Kakurwa jipe Moyo haya ni mapito tu🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom