Dkt. Biteko awawashia moto TANESCO, adai "Mmezoea matatizo, hatutakubali!"

Dkt. Biteko awawashia moto TANESCO, adai "Mmezoea matatizo, hatutakubali!"

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wakuu

Kash Kash karibu na uchaguzi

==

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, amekemea vikali utendaji wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) "Mmeanza kulala, mmezoea kazi, mmezoea matatizo. Mwaka mzima matatizo, tunarudi nyuma. Siwezi kukubali hiyo biashara ya kufika mahali tukazoea matatizo,"

Kauli hiyo imetokana na kutoridhishwa kwake na utendaji wa kituo hicho, ambacho kimeshindwa kutoa huduma bora kwa wananchi.

Dkt. Biteko ameagiza kufumuliwa na kuundwa upya kwa kituo hicho ndani ya wiki moja ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma zinazostahili.

Soma, Pia:
 
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko ameagiza kufumuliwa kwa Kituo cha Huduma kwa Wateja cha Shirika la Umeme Nchini, (TANESCO ) kufuatia kituo hicho kushindwa kuwahudumia Wananchi kwa viwango vinavyotarajiwa.

Ametoa agizo hilo leo jijini Dar es Salaam baada ya kutembelea kituo hicho pamoja na mambo mengine kufuatilia utekelezaji wa maelekezo yake aliyoyatoa mwezi Aprili, 2024.

Dkt. Biteko ameshangazwa na hatua ya TANESCO kuweka kando maelekezo ya mwezi Aprili 2024 yaliyolitaka Shirika hilo kuondokana na matumizi ya namba za kulipia kwenye utoaji wa huduma na kuomba namba ya bure ya huduma (free toll number) kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania -TCRA ili kuwapa unafuu wananchi wanaohitaji huduma za TANESCO.

“ Wewe ulishapiga simu, pesa yako ikakatwa na huduma usiipate? Wananchi wanaumia sana!” naagiza kuundwa upya kituo ili kuongeza ufanisi na tija kwa Wananchi, “kituo hiki kinategemewa na Watanzania wengi na huduma inayotolewa hapa hairidhishi kabisa,” amesema Dkt. Biteko.

Ameongeza kuwa, Serikali ya Rais Samia imetoa fedha nyingi kuhudumia kituo hicho lakini utendaji wake ni mbovu kuliko huduma ya kituo.

TANESCO ilielekezwa kuachana na matumizi ya namba za kulipia Kwenye utoaji wa huduma na kuomba namba ya bure ya huduma (toll number) kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania -TCRA ili kuwapa unafuu wa Wananchi wanapopiga kuhitaji huduma za TANESCO.

Dkt. Biteko ametoa wiki moja kwa uogozi wa TANESCO kufanya maboresho ya Kituo hicho na matokeo yake yawe wazi kwa Wananchi kutokana na huduma zake.

Akizungumzia utendaji wa Kituo hicho, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Abubakar Issa amesema kulikuwa na changamoto za kibajeti. Aidha amesema kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA watakaa haraka na kuanza matumizi ya namba bila malipo ili kutoa unafuu kwa wananchi na kuleta tija kwa watumiaji.

#KitengeUpdates
 
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko ameagiza kufumuliwa kwa Kituo cha Huduma kwa Wateja cha Shirika la Umeme Nchini, (TANESCO ) kufuatia kituo hicho kushindwa kuwahudumia Wananchi kwa viwango vinavyotarajiwa.

Ametoa agizo hilo leo jijini Dar es Salaam baada ya kutembelea kituo hicho pamoja na mambo mengine kufuatilia utekelezaji wa maelekezo yake aliyoyatoa mwezi Aprili, 2024.

Dkt. Biteko ameshangazwa na hatua ya TANESCO kuweka kando maelekezo ya mwezi Aprili 2024 yaliyolitaka Shirika hilo kuondokana na matumizi ya namba za kulipia kwenye utoaji wa huduma na kuomba namba ya bure ya huduma (free toll number) kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania -TCRA ili kuwapa unafuu wananchi wanaohitaji huduma za TANESCO.

“ Wewe ulishapiga simu, pesa yako ikakatwa na huduma usiipate? Wananchi wanaumia sana!” naagiza kuundwa upya kituo ili kuongeza ufanisi na tija kwa Wananchi, “kituo hiki kinategemewa na Watanzania wengi na huduma inayotolewa hapa hairidhishi kabisa,” amesema Dkt. Biteko.

Ameongeza kuwa, Serikali ya Rais Samia imetoa fedha nyingi kuhudumia kituo hicho lakini utendaji wake ni mbovu kuliko huduma ya kituo.

TANESCO ilielekezwa kuachana na matumizi ya namba za kulipia Kwenye utoaji wa huduma na kuomba namba ya bure ya huduma (toll number) kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania -TCRA ili kuwapa unafuu wa Wananchi wanapopiga kuhitaji huduma za TANESCO.

Dkt. Biteko ametoa wiki moja kwa uogozi wa TANESCO kufanya maboresho ya Kituo hicho na matokeo yake yawe wazi kwa Wananchi kutokana na huduma zake.

Akizungumzia utendaji wa Kituo hicho, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Abubakar Issa amesema kulikuwa na changamoto za kibajeti. Aidha amesema kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA watakaa haraka na kuanza matumizi ya namba bila malipo ili kutoa unafuu kwa wananchi na kuleta tija kwa watumiaji.

#KitengeUpdates
Wanashindwa hata na DUWASA!_Dodoma,maji ni uhai!
 
Hiyo namba ya toll free number TCRA wanagawa Bure? Na gharama zake kwa mwezi analipa nani? Aina nyingine ya wizi unaenda kufanyika
 
“ Wewe ulishapiga simu, pesa yako ikakatwa na huduma usiipate? Wananchi wanaumia sana!” naagiza kuundwa upya kituo ili kuongeza ufanisi na tija kwa Wananchi, “kituo hiki kinategemewa na Watanzania wengi na huduma inayotolewa hapa hairidhishi kabisa,” amesema Dkt. Biteko.

Ameongeza kuwa, Serikali ya Rais Samia imetoa fedha nyingi kuhudumia kituo hicho lakini utendaji wake ni mbovu kuliko huduma ya kituo.
Ningeshangaa kutoona huo mstari
Anyway wa kufumuliwa alitakiwa awe Mkurugenzi siyo kituo
 
Akizungumzia utendaji wa Kituo hicho, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Abubakar Issa amesema kulikuwa na changamoto za kibajeti.
Ameongeza kuwa, Serikali ya Rais Samia imetoa fedha nyingi kuhudumia kituo hicho lakini utendaji wake ni mbovu kuliko huduma ya kituo.
Nani mkweli hapo?
 
Back
Top Bottom