Pre GE2025 Dkt. Biteko: Kule Bukombe tuliwahi kuchagua Wapinzani tunaelewa madhara yake, nawasihi wananchi wote chagueni CCM

Pre GE2025 Dkt. Biteko: Kule Bukombe tuliwahi kuchagua Wapinzani tunaelewa madhara yake, nawasihi wananchi wote chagueni CCM

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Naibu Waziri mkuu Dr Biteko amesema uchaguzi wa serikali za mitaa uko Karibu hivyo Wananchi wajipange kufanya uamuzi wa busara wa kuichagua CCM

Dr Biteko amewashukuru Wananchi wa Mbogwe kwa kuichagua CCM miaka yote, "Kule Bukombe tuliwahi kuchagua Wapinzani tunaelewa madhara yake" amesisitiza Naibu Waziri mkuu

Chanzo: Upendo TV
 
Kama huyu ndiye naibu waziri mkuu, basi tumepigwa.

Huyu mwalimu wa shule ya msingi Biteko hana kitu kichwani kabisa. Ama kweli ccm hutoa vyeo kwa mbumbumbu.

Hivi amewahi kuongea cha maana huyu? Wapi? Na lini?
 
Kinachowaharibia upinzani ni kupinga kila kitu kiasi cha kufikia kujipinga hata wao wenyewe kwa mambo ambayo mengine yapo wazi kabisa, safari ya maendeleo ni hatua kwa hatua, na hakuna muujiza
 
Yuko sahihi kwa kiasi fulani. Tulikuwa na wabunge wa upinzani, ukafika wakati wakawa wanapinga kila kitu, mpaka miradi ya maendeleo kwenye majimbo yao wenyewe; eti kazi ya upinzani ni kupinga! Upuuzi mtupu.
Mbunge gani aliyefanya hivyo?
 
Kama huyu ndiye naibu waziri mkuu, basi tumepigwa.

Huyu mwalimu wa shule ya msingi Biteko hana kitu kichwani kabisa. Ama kweli ccm hutoa vyeo kwa mbumbumbu.

Hivi amewahi kuongea cha maana huyu? Wapi? Na lini?
Zaidi ya Vitisho tu
 
Yuko sahihi kwa kiasi fulani. Tulikuwa na wabunge wa upinzani, ukafika wakati wakawa wanapinga kila kitu, mpaka miradi ya maendeleo kwenye majimbo yao wenyewe; eti kazi ya upinzani ni kupinga! Upuuzi mtu
Unapo- comment hapa ujue hadhira ya jf imeelimika, sio kwamba unawasiliana na wajinga kama wale wanaogawiwa kofia na kanga za kijani wakati wa uchafuzi. Sema kabisa mbunge gani wa upinzani alipinga kila kitu.

Tunajua wabunge wa upinzani wamekuwa wakiikosoa/ kuipinga serikali ktk yale mambo ambayo mtu yeyote mwenye akili, anayependa kuona ustawi wa taifa letu anaona wazi wanasiasa wa ccm wamekosea, tena mara nyingi kwa makusudi.

Mfano, nani asiyejua wabunge wa upinzani walivyolalamikia mikataba ya madini na gesi, wakafukuzwa bungeni, ikapitishwa na wabunge wa ccm, baadae ccm haohao wanakuja kuvunja mikataba hiyo bila kufuata taratibu na kulitia taifa katika hasara kubwa?

Tuambie huyo mbunge wa uipinzani aliyepinga mradi wa maji, afya, elimu etc ni yupi?

Kauli ya biteko inadhihirisha jinsi ccm wasivyo tayari kwa demokkrasia. Haina tofauti na kauli ya magufuli kwamba ukichagua upinzani hutapata maendeleo - magufuli alimaanisha yeye na serikali yake walikuwa wanatumia madaraka yao vibaya kubagua wananchi waliotumia haki yao ya kidemokrasia kuchagua wawakilishi wanaowataka, ambao sio ccm.

Ni sawa na kauli ya saa mia moja kwamba hata ukichagua upinzani, ccm ndiyo itakutawala.
 
Watatengwa kama Mbeya.Toka tumewaweka pembeni Wapinzani maendelea ya Mkoa Sasa ni kemkem.

Ni ujinga kuchagua Wapinzani ambao hawawezi kushika Dola then sijui watakuwa wanatekelezaje Ilani.
 
Back
Top Bottom