Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Dkt. Biteko amesema tabia ya kutobadilisha au kukarabati miundombinu kwa wakati pale inapoharibika inawakosesha wananchi huduma ya umeme kwa kipindi kirefu.
Amesema hayo tarehe 21 Februari, 2024 wakati wa ziara yake mkoani Njombe ambapo amewasha umeme katika Kijiji cha Ikwavila na Shule ya Sekondari ya Wasichana Njombe iliyoko wilayani Wanging'ombe pamoja na kukagua mindombinu ya uzalishaji umeme na nguzo za umeme katika kiwanda cha TANWAT.
Dkt. Biteko ametoa maagizo hayo baada ya Mbunge wa Wanging'ombe, Mhe. Dkt. Festo Dugange kueleza kuwa, Wilaya hiyo ina changamoto ya radi nyingi zinazosabababisha transfoma kuungua kwa takriban 50 hadi 60 kwa mwaka lakini ubadilishaji wake umekuwa ukichukua muda mrefu na hivyo kuathiri shughuli za kijamii na kiuchumi.
"Hili suala la transfoma inaungua halafu inachukua hadi mwezi mmoja kubadiliswa, uzembe huu haukubaliki, Idara ya Manunuzi TANESCO tumeibadilisha kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kama hii ya uzembe wakati vifaa hivi vinazalishwa kwenye viwanda vya ndani, tunataka watendaji hawa waone shida wanazopata wananchi na kuzitatua, kweli kuna changamoto ya umeme lakini kuna baadhi ya matatizo TANESCO wanaweza kuyamaliza." Amesema Dkt. Biteko
Amesema kuwa, Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan hataki kero ya umeme iendelee ndio mana utekelezaji wa mradi wa umeme wa Julius Nyerere (JHNPP) unaenda kwa kasi na sasa umefikia asilimia 99 na mtambo mmoja umekamilika utakaoingiza megawati 235 kwenye gridi mwezi huu huku mtambo mwingine ukitarajiwa kuingiza megawati nyingine 235 mwezi Machi mwaka huu.
Kuhusu ombi la Mbunge wa Wanging'ombe kupata laini ya umeme inayojitegemea kwani laini ya sasa inatumiwa pia na eneo Lupembe na TANWAT mkoani Njombe na hivyo kufanya umeme wilayani humo kuwa hafifu, ameagiza TANESCO kujenga kituo cha kupoza umeme wilayani humo ili kutengemaza hali ya upatikanaji umeme.
==============For English Audience Only=================
Deputy Prime Minister and Minister of Energy, Dr. Doto Biteko, has instructed experts to repair the electricity infrastructure promptly to enable citizens to access reliable electricity services. Dr. Biteko emphasized that the habit of not repairing or renovating infrastructure promptly when damaged deprives citizens of electricity services for extended periods.
He made these remarks on February 21, 2024, during his visit to Njombe region, where he inaugurated electricity in Ikwavila Village and Njombe Girls' Secondary School in Wanging'ombe district. Additionally, he inspected the electricity production infrastructure and power poles at the TANWAT factory.
Dr. Biteko issued these directives after Member of Parliament for Wanging'ombe, Dr. Festo Dugange, highlighted that the district faces numerous challenges, including frequent transformer damage, with approximately 50 to 60 transformers burning annually, and replacement taking an extended period, affecting social and economic activities.
He emphasized the unacceptability of this negligence and directed TANESCO's Procurement Department to address these issues promptly. Dr. Biteko noted that President Samia Suluhu Hassan is committed to resolving electricity challenges, with the Julius Nyerere Hydropower Project nearing completion, expected to add 235 megawatts to the grid this month and an additional 235 megawatts in March. Regarding the request for a separate electricity line for Wanging'ombe, as the current line is shared with Lupembe and TANWAT, leading to unreliable power supply, he instructed TANESCO to construct a substation in the district to stabilize electricity availability.