Mpangawangu
JF-Expert Member
- Mar 5, 2014
- 887
- 965
Nimesoma tamko la TEC
Kwanza tamko limesomwa na mtu mmoja bila kuwepo na askofu mwingine yeyote.
Aliyesoma na kuandika tamko amekuwa miongoni mwa watu wanaopinga mkataba wa bandari kwa nyakati tofauti hata kabla ya tamko la leo. TEC imetumika kama Jukwaa lilisaidia Slaa na Kitima kufikisha hoja zao.
Rejea mjadala mdaharo uliowashirikisha Rostam, Kitila Mkumbo, Zitto, Lema, Shekh Ponda, Balile na Dkt. Kitima mwenyewe.
Kwenye madahalo watu wote walikubaliana kuhusu umuhimu wa uwekezaji, Kitima pekee ndie alikuwa na hoja tofauti, akasema haoni sababu ya kukabidhi uhuru wetu kwa waarabu, akapinga uwekezaji na kutaka mkataba tuachane nao, tuwaachie vijana wa kitanzania waendeshe, akaongeza kuwa hata wakiiba watatumia pesa hizo humuhumu nchini(ingia youtube andika mdaharo wa bandari utaona ninachokisema)
Leo ameibuka kama katibu wa TEC nafasi iliyowahi kushikwa na Dkt. Slaa.
Anatoa tamko kwamba TEC inapinga uwekezaji na wanamuamuru Rais Ufute mkataba.
Kwenye andiko lake ametoa hoja kubwa tatu.
1. Kwenye andiko lake anadai Mihimili iheshimiane, isiingiliwe hapa alimaanisha Kesi ya Mwabukusi ambayo kwa vyovyote Kitima alihusika kuifungua.
Kushindwa kwa Mwabukusi ni sawa na kushindwa kwa Kitima, lazima Kitima atafute plan B.
Kitima kwenye andiko lake anasema mihimili isiingiliane, kila muhimili uwe huru.
Kwake anaamini walishindwa kesi kwakuwa mahakama haikuwa na uhuru wa kufanya maamuzi, Kitima ni kama anasema mahakama ilishinikizwa kutoa yale maamuzi.
Halafu anafanya makosa kwenye andiko hilohilo kuhusu hoja hiyo kwa mushinikiza Rais Samia kutengua maamuzi ya bunge ambao ni muhimili mwingine wa dola ambao awali amesema mihimili isiingiliwe.
Hapa anahalalisha kuingiliwa kwa munimili wa Bunge ili kufanikisha malengo yake.
Rais akiingilia bunge atakuwa naendelea kuvunja katiba, kukosea kwa kufanya kile ambacho Kitima anapinga kwenye Tamko lake.
2. Kuhusu hoja ya kutaka Bandari iendeshwe na wazawa, kwamba haijawahi kuendeshwa na wageni, amesahau kuwa Bandari imeendeshwa na TICS kwa miaka 22 hakulisema hili kwa makusudi, huenda anatamani TICS ndio iendelee badala ya DP-World ili kulinda maslahi binafsi aliyonayo bandarini.
Hapa Kitima ni kama ana msalahi binafsi anayoyapigania kwa kutumia mwamvuli wa TEC, hoja yake inamashaka. Kumbukeni sakata la ESCROW kuna hadi viongozi wa dini ambao walinufaika na wizi wa ESCROW sio wasafi kwa kiwango hicho.
3. Kitima na Dkt. Slaa ni watu wenye Itikadi kali ya ukristo(Udini)
Kuna Wakristo wasiokuwa na ubaguzi halafu kuna Slaa na Kitima waliopea kwenye Udini.
Sio utamaduni wetu Watanzania kunadiliana habari za udini ma Ukabila, lakini kwa muktadha huu nitalisemea ili muwajue vizuri.
Kwa nyakati tofauti Kitima ameonesha ni mtu mwenye chuki ya kidini na mdini sana tangu akiwa Makamu mkuu wa chuo cha St Augustine Mwanza.
Nakumbuka wakati wa utawala wa Rais Kikwete kwenye kipindi cha star TV chini ya Dotto Bulendu kitima aliilaumu serikali ya Rais Kikwete kwa kuruhusu waarabu wenye ndevu hadi kifuani kuzagaa Kariakoo, alisema kwamba wale wenye ndevu ndio magaidi kwamba serikali inawatazama haiwachukulii hatua.
Yaani kwenye ule mjadala, kitima akaona ndevu ni tishio kwake.
Ndiyo maana Tangu utawala uchukuliwe na Rais Magufuli, Mkatoliki mwenzake Kitima hajawahi kujitokeza hadharani kuipinga serikalinya magufulipamoja na chamgamoto zote za Utawala wa Magufuli.
Kadhalika Dkt. Slaa, kwenye utawala wa Magufuli hakuwahi kuishambulia serikali kwa lolote hata pale palipokuwa na makosa ya wazi, baadae Slaa alipewa zawadi ya cheo kuwa balozi wa tanzania kwa kazi nzuri ya Kuhujumu demokrasia yetu.
Baadae alirudishwa nyumbani baada ya kumaliza muda wake wakati wa utawala wa Rais samia, hadi hivi karibuni kwenye sakata la mbowe, Slaa alisema mbowe anaweza kuwa gaidi kwamba mashtaka aliyoshtakiwa nayo yalikuwa halali, hapa alitoa kauli ya kumfurahisha Rais samia kwa lengo la kuwinda zawadi ya cheo kipya.
Rais Samia amejipambanua kuwa hataki wapambe ni kiongozi anaetembea kwenye 4R, msisitizo ukiwa mwafaka wa kitaifa.
Watu kama slaa ambao wanashangilia mauaji na uonevu Rais samia aliona hawawezi kumsaidia.
Pia Rais Samia anaamini katika uongozi wa vijana.Slaa ana zaidi miaka 78.
Baada ya Slaa kukiridhisha kuwa utawala wa Rais Samia hauna mpango wa kumtumia, ndipo akaamua kuungana na Dr.Charles Kitima kuishambukia serikali
Kama Slaa angepewa cheo, muda huu angekuwa anatetea Mkataba wa DP World.
Huu ni uthibitisho kuwa Kitima na Slaa ni wadini sana ambao Kuingia kwa Rais Samia madarakani kwao waliona ni suprise.
Hawakujiadaa kuongozwa na Rais Samia ndio maana Wamekuwa mbogo sio kwenye mkataba wa bandari tu bali kwenye utawala wa Rais Samia kwa ujumla.
Rejea mahojiano ya Slaa na star tv baada ya Rais samia kuapishwa, Slaa aliishambulia serikali na kuituhumu kuhusu kifo cha Rais Magufuli, Slaa akamalizia kwa kusema kama wanataka wanikamate,siogopi kukamatwa, alionekana ni mtu mwwnye hasira ya kukosa cheo.
Kwa msingi huo, huu ni uthibitisho kuwa Tamko lililoitwa la TEC lina msukumo wa kidini kuliko msukumo wa kisheria na kisiasa.
Nchi yetu ina dini kubwa Mbili, Wakristo na waislaam, tujaalie hilo ni tamko la wakatoliki.
Je na waislaam nao wakitoa tamko lao linalopingana na tamko la TEC?
Vipi walokole nao wakiunga mkono uwekezaji, serikali itafuata msimamo wa dini gani?
Ndio msingi uliosababisha serikali kutamka kuwa haina dini,lengo nikuepuka misuguano inayoweza kuliingiza taifa kwenye machafuko.
Tumeshatoa maoni,serikali imeyasikia na ndani ya serikali kuna watu wa dini zote na wasiokuwa na dini, kuna wanasheria kuna vyombo mbalimbali vya dola.
Ni imani yangu kuwa Swala la uwekezaji wa Bandari watalifanyia kazi kwa kulinda maslahi ya taifa.
Viongozi wa dini wasiingile utendaji wa serikali ambayo kila mmoja anatambua haina dini.
Tuwapuuze Slaa na kitima, wanataka kutuingiza kwwnye vita yao ya maslahi binafsi kwa Kisingizio cha kulinda rasilimali , tuulinde umoja wetu uliodumu kwa zaidi ya miaka 50.
Tujifunze Burundi na Rwanda, mauaji ya kimbali yalihamasishwa na viongozi wa dini.
Kwanza tamko limesomwa na mtu mmoja bila kuwepo na askofu mwingine yeyote.
Aliyesoma na kuandika tamko amekuwa miongoni mwa watu wanaopinga mkataba wa bandari kwa nyakati tofauti hata kabla ya tamko la leo. TEC imetumika kama Jukwaa lilisaidia Slaa na Kitima kufikisha hoja zao.
Rejea mjadala mdaharo uliowashirikisha Rostam, Kitila Mkumbo, Zitto, Lema, Shekh Ponda, Balile na Dkt. Kitima mwenyewe.
Kwenye madahalo watu wote walikubaliana kuhusu umuhimu wa uwekezaji, Kitima pekee ndie alikuwa na hoja tofauti, akasema haoni sababu ya kukabidhi uhuru wetu kwa waarabu, akapinga uwekezaji na kutaka mkataba tuachane nao, tuwaachie vijana wa kitanzania waendeshe, akaongeza kuwa hata wakiiba watatumia pesa hizo humuhumu nchini(ingia youtube andika mdaharo wa bandari utaona ninachokisema)
Leo ameibuka kama katibu wa TEC nafasi iliyowahi kushikwa na Dkt. Slaa.
Anatoa tamko kwamba TEC inapinga uwekezaji na wanamuamuru Rais Ufute mkataba.
Kwenye andiko lake ametoa hoja kubwa tatu.
1. Kwenye andiko lake anadai Mihimili iheshimiane, isiingiliwe hapa alimaanisha Kesi ya Mwabukusi ambayo kwa vyovyote Kitima alihusika kuifungua.
Kushindwa kwa Mwabukusi ni sawa na kushindwa kwa Kitima, lazima Kitima atafute plan B.
Kitima kwenye andiko lake anasema mihimili isiingiliane, kila muhimili uwe huru.
Kwake anaamini walishindwa kesi kwakuwa mahakama haikuwa na uhuru wa kufanya maamuzi, Kitima ni kama anasema mahakama ilishinikizwa kutoa yale maamuzi.
Halafu anafanya makosa kwenye andiko hilohilo kuhusu hoja hiyo kwa mushinikiza Rais Samia kutengua maamuzi ya bunge ambao ni muhimili mwingine wa dola ambao awali amesema mihimili isiingiliwe.
Hapa anahalalisha kuingiliwa kwa munimili wa Bunge ili kufanikisha malengo yake.
Rais akiingilia bunge atakuwa naendelea kuvunja katiba, kukosea kwa kufanya kile ambacho Kitima anapinga kwenye Tamko lake.
2. Kuhusu hoja ya kutaka Bandari iendeshwe na wazawa, kwamba haijawahi kuendeshwa na wageni, amesahau kuwa Bandari imeendeshwa na TICS kwa miaka 22 hakulisema hili kwa makusudi, huenda anatamani TICS ndio iendelee badala ya DP-World ili kulinda maslahi binafsi aliyonayo bandarini.
Hapa Kitima ni kama ana msalahi binafsi anayoyapigania kwa kutumia mwamvuli wa TEC, hoja yake inamashaka. Kumbukeni sakata la ESCROW kuna hadi viongozi wa dini ambao walinufaika na wizi wa ESCROW sio wasafi kwa kiwango hicho.
3. Kitima na Dkt. Slaa ni watu wenye Itikadi kali ya ukristo(Udini)
Kuna Wakristo wasiokuwa na ubaguzi halafu kuna Slaa na Kitima waliopea kwenye Udini.
Sio utamaduni wetu Watanzania kunadiliana habari za udini ma Ukabila, lakini kwa muktadha huu nitalisemea ili muwajue vizuri.
Kwa nyakati tofauti Kitima ameonesha ni mtu mwenye chuki ya kidini na mdini sana tangu akiwa Makamu mkuu wa chuo cha St Augustine Mwanza.
Nakumbuka wakati wa utawala wa Rais Kikwete kwenye kipindi cha star TV chini ya Dotto Bulendu kitima aliilaumu serikali ya Rais Kikwete kwa kuruhusu waarabu wenye ndevu hadi kifuani kuzagaa Kariakoo, alisema kwamba wale wenye ndevu ndio magaidi kwamba serikali inawatazama haiwachukulii hatua.
Yaani kwenye ule mjadala, kitima akaona ndevu ni tishio kwake.
Ndiyo maana Tangu utawala uchukuliwe na Rais Magufuli, Mkatoliki mwenzake Kitima hajawahi kujitokeza hadharani kuipinga serikalinya magufulipamoja na chamgamoto zote za Utawala wa Magufuli.
Kadhalika Dkt. Slaa, kwenye utawala wa Magufuli hakuwahi kuishambulia serikali kwa lolote hata pale palipokuwa na makosa ya wazi, baadae Slaa alipewa zawadi ya cheo kuwa balozi wa tanzania kwa kazi nzuri ya Kuhujumu demokrasia yetu.
Baadae alirudishwa nyumbani baada ya kumaliza muda wake wakati wa utawala wa Rais samia, hadi hivi karibuni kwenye sakata la mbowe, Slaa alisema mbowe anaweza kuwa gaidi kwamba mashtaka aliyoshtakiwa nayo yalikuwa halali, hapa alitoa kauli ya kumfurahisha Rais samia kwa lengo la kuwinda zawadi ya cheo kipya.
Rais Samia amejipambanua kuwa hataki wapambe ni kiongozi anaetembea kwenye 4R, msisitizo ukiwa mwafaka wa kitaifa.
Watu kama slaa ambao wanashangilia mauaji na uonevu Rais samia aliona hawawezi kumsaidia.
Pia Rais Samia anaamini katika uongozi wa vijana.Slaa ana zaidi miaka 78.
Baada ya Slaa kukiridhisha kuwa utawala wa Rais Samia hauna mpango wa kumtumia, ndipo akaamua kuungana na Dr.Charles Kitima kuishambukia serikali
Kama Slaa angepewa cheo, muda huu angekuwa anatetea Mkataba wa DP World.
Huu ni uthibitisho kuwa Kitima na Slaa ni wadini sana ambao Kuingia kwa Rais Samia madarakani kwao waliona ni suprise.
Hawakujiadaa kuongozwa na Rais Samia ndio maana Wamekuwa mbogo sio kwenye mkataba wa bandari tu bali kwenye utawala wa Rais Samia kwa ujumla.
Rejea mahojiano ya Slaa na star tv baada ya Rais samia kuapishwa, Slaa aliishambulia serikali na kuituhumu kuhusu kifo cha Rais Magufuli, Slaa akamalizia kwa kusema kama wanataka wanikamate,siogopi kukamatwa, alionekana ni mtu mwwnye hasira ya kukosa cheo.
Kwa msingi huo, huu ni uthibitisho kuwa Tamko lililoitwa la TEC lina msukumo wa kidini kuliko msukumo wa kisheria na kisiasa.
Nchi yetu ina dini kubwa Mbili, Wakristo na waislaam, tujaalie hilo ni tamko la wakatoliki.
Je na waislaam nao wakitoa tamko lao linalopingana na tamko la TEC?
Vipi walokole nao wakiunga mkono uwekezaji, serikali itafuata msimamo wa dini gani?
Ndio msingi uliosababisha serikali kutamka kuwa haina dini,lengo nikuepuka misuguano inayoweza kuliingiza taifa kwenye machafuko.
Tumeshatoa maoni,serikali imeyasikia na ndani ya serikali kuna watu wa dini zote na wasiokuwa na dini, kuna wanasheria kuna vyombo mbalimbali vya dola.
Ni imani yangu kuwa Swala la uwekezaji wa Bandari watalifanyia kazi kwa kulinda maslahi ya taifa.
Viongozi wa dini wasiingile utendaji wa serikali ambayo kila mmoja anatambua haina dini.
Tuwapuuze Slaa na kitima, wanataka kutuingiza kwwnye vita yao ya maslahi binafsi kwa Kisingizio cha kulinda rasilimali , tuulinde umoja wetu uliodumu kwa zaidi ya miaka 50.
Tujifunze Burundi na Rwanda, mauaji ya kimbali yalihamasishwa na viongozi wa dini.