Dkt. Conrad Masabo: Tulikosea tulipokabidhi umiliki wa demokrasia kwa vyama vya siasa badala ya umiliki huo kubaki kwa raia

Dkt. Conrad Masabo: Tulikosea tulipokabidhi umiliki wa demokrasia kwa vyama vya siasa badala ya umiliki huo kubaki kwa raia

DR Mambo Jambo

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2012
Posts
11,622
Reaction score
26,005
Mhadhiri wa sayansi ya siasa wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Dk Conrad Masabo anasema demokrasia ya Tanzania iliharibiwa tangu mwaka 2016 kutokana na uamuzi uliofanywa na Watanzania kuamini mtu na sio utaratibu.

“Tunachokipitia ni matokeo ya huo uamuzi wetu. Demokrasia kama haki nyingine hudaiwa na sio kuombwa, pia inapaswa kulindwa ili walioitoa wasiipokonye tena,” anasema.

Katika kipindi hicho, Dk Masabo anasema Watanzania wote waliamini Hayati John Magufuli ni mkombozi na 2021 waliamini Rais Samia Suluhu Hassan atawakomboa, hadi kupigiwa chapuo na vyama vya upinzani.

Kwa mtazamo wa mwanazuoni huyo, kwa hali ilivyo hadhani kama maboresho yanawezekana.

Hata hivyo, anaeleza uwezekano upo katika mambo mawili ambayo ni kuja kwa kiongozi mwenye hisani aijenge demokrasia licha ya kuwa jambo hilo ni gumu kwa mfumo wa demokrasia ya vyama uliopo.

Jambo la pili, anasema wananchi wajiunge kuidai, kitu ambacho ni kigumu kwa vile raia wameamua kuwaachia wanasiasa jukumu hilo.

“Kuna uwezekano mkubwa wa kulipa thamani kubwa ili kurejea tulipokuwa mwaka 2015, swali ni nani wa kulipa gharama hii?” anahoji.

Dk Masabo anasema kinachoitesa Tanzania ni kwa sababu demokrasia yake ni ya vyama na sio ya raia, hivyo raia au wananchi wanaamini hawana wajibu wa kudai na kuilinda.

“Mafanikio ya Reject Financial Bill (kuondolewa kwa muswada wa fedha) ya Kenya ni kwa vile ilikuwa inaongozwa na kusimamiwa na raia na ndio maana baada ya vyama kuingia, malengo na mafanikio yamepotea,” anafafanua.

Credit: JamboTv
Screenshot_20240919_080222_X.jpg
 
Mna uhakika na hiyo phd yake?
Kwa hiyo vyama vya siasa vinamilikiwa na Mbuzi?
 
Mna uhakika na hiyo phd yake?
Kwa hiyo vyama vya siasa vinamilikiwa na Mbuzi?
Kuna Tofauti kubwa sana Kati ya Vyama vya Siasa na Demokrasia ndugu..
Unaweza ukawa na vyama vya Siasa lakini hauna Demokrasia..

Wewe unavyohisi Kipindi cha Hilter hakukuwa na Chama cha Siasa?? Kipindi cha Mugabe hakukuwa na Chama cha Siasa?? Kipindi cha Idd amini hakukuwa na Chama cha siasa??

Kuwa na akiba ya Maneno na Ujifunze kwa maswali
 
Kuna Tofauti kubwa sana Kati ya Vyama vya Siasa na Demokrasia ndugu..
Unaweza ukawa na vyama vya Siasa lakini hauna Demokrasia..

Wewe unavyohisi Kipindi cha Hilter hakukuwa na Chama cha Siasa?? Kipindi cha Mugabe hakukuwa na Chama cha Siasa?? Kipindi cha Idd amini hakukuwa na Chama cha siasa??

Kuwa na akiba ya Maneno na Ujifunze kwa maswali
Basi leteni demokrasia yenu au ndio hii hii ya kutekana?
 
Mhadhiri wa sayansi ya siasa wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Dk Conrad Masabo anasema demokrasia ya Tanzania iliharibiwa tangu mwaka 2016 kutokana na uamuzi uliofanywa na Watanzania kuamini mtu na sio utaratibu.

“Tunachokipitia ni matokeo ya huo uamuzi wetu. Demokrasia kama haki nyingine hudaiwa na sio kuombwa, pia inapaswa kulindwa ili walioitoa wasiipokonye tena,” anasema.

Katika kipindi hicho, Dk Masabo anasema Watanzania wote waliamini Hayati John Magufuli ni mkombozi na 2021 waliamini Rais Samia Suluhu Hassan atawakomboa, hadi kupigiwa chapuo na vyama vya upinzani.

Kwa mtazamo wa mwanazuoni huyo, kwa hali ilivyo hadhani kama maboresho yanawezekana.

Hata hivyo, anaeleza uwezekano upo katika mambo mawili ambayo ni kuja kwa kiongozi mwenye hisani aijenge demokrasia licha ya kuwa jambo hilo ni gumu kwa mfumo wa demokrasia ya vyama uliopo.

Jambo la pili, anasema wananchi wajiunge kuidai, kitu ambacho ni kigumu kwa vile raia wameamua kuwaachia wanasiasa jukumu hilo.

“Kuna uwezekano mkubwa wa kulipa thamani kubwa ili kurejea tulipokuwa mwaka 2015, swali ni nani wa kulipa gharama hii?” anahoji.

Dk Masabo anasema kinachoitesa Tanzania ni kwa sababu demokrasia yake ni ya vyama na sio ya raia, hivyo raia au wananchi wanaamini hawana wajibu wa kudai na kuilinda.

“Mafanikio ya Reject Financial Bill (kuondolewa kwa muswada wa fedha) ya Kenya ni kwa vile ilikuwa inaongozwa na kusimamiwa na raia na ndio maana baada ya vyama kuingia, malengo na mafanikio yamepotea,” anafafanua.

Credit: JamboTvView attachment 3100112
Alipokosea ni kusema ilianzia 2016 , wakati huyo WA 2016 alikuwa ana rekebisha mapungufu yaliokuwepo kabla yake.
Matatizo yetu yata suluhishwa Kwa kuwa na Katiba Mpya, hii ya sasa inategemeana na Busara na IQ ya Kiongozi.
 
Basi leteni demokrasia yenu au ndio hii hii ya kutekana?
Samahani!
Unaposema Neno "Leteni" ni ipi hasa Tafsiri yako?

Sipo katika Jukwaa au Kundi lolote la Kimaamuzi kisiasa pengine Ungetaja watu uliotaka wasikie Your Concern..
Thanks
 
Back
Top Bottom