Mwanahabari wa Taifa
JF-Expert Member
- May 27, 2020
- 1,588
- 956
🤣🤣Naona PhD imeanza kuonekana kivitendo, Chapa kazi Biteko,
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
🤣🤣Naona PhD imeanza kuonekana kivitendo, Chapa kazi Biteko,
Jambo usilolijua na sawa na usiku wa kiza.Lakini kuna kundi la Wajinga wachache wanasema hafai! Kiss anatokea kanda ya ziwa!
Njoo na Ushahidi mkuu wanguJambo usilolijua na sawa na usiku wa kiza.
The guy is corrupt 100%.
Huyu bwana ni mla rushwa mkubwa. Anaamini sana katika rushwa, ndiyo maana pia kwenye kupata PhD yake, na yeye katumia njia ya utoaji rushwa.hata ufanyeje ratiba ya kuondolewa wizarani ipo pale pale, kuvuja kwa taarifa ndo kumekupa muda wa ziada bt muda wowote utatimuliwa.
Sikatai, Wewe thibitisha tu mkuu, Mlarushwa hawezi kusemwa tu mpaka pamekuwa na Ushahidi,Huyu bwana ni mla rushwa mkubwa. Anaamini sana katika rushwa, ndiyo maana pia kwenye kupata PhD yake, na yeye katumia njia ya utoaji rushwa.
Yeye kuwataja waovu wengine hakufuti uovu wake.
Safi sana Waziri Dk. Biteko. Hawa wanaochafua taswira ya nchi kwa kutapeli wafanyabiashara wa nje wanapaswa kupewa adhabu kali hasa.===
Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko amemwagiza Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Mhandisi Yahya Samamba kuwasimamisha kazi Maafisa saba wa Ofisi za Madini za Mikoa mbalimbali ya Kanda ya Ziwa kutokana na kutokuwa waaminifu katika shughuli zao za usimamizi wa Sekta ya Madini katika maeneo yao.
Agizo hilo amelitoa Dkt. Biteko Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga alipokutana na Wafanyabiashara wa Madini wa Kanda ya Ziwa kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara hao.
Dkt, Doto Biteko amesema, kuna baadhi ya watumishi wa Ofisi za Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa ambao sio waaminifu na wanajihusisha na udanganyifu kwenye biashara ya madini ikiwemo kuwapunguzia wachimbaji viwango vya ubora wa madini yao ili wajipatie fedha.
“Nichukue fursa hii kuwatadharisha Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa yote nchini kuhakikisha mnawafuatilia kwa karibu Maafisa wenu wanaoshirikiana na baadhi ya wafanyabiashara ambao wamekuwa wakiwaibia wachimbaji wadogo wa madini kwa kupaka mafuta kwenye mashine ya kupimia ubora wa dhahabu na kusababisha kupata kiwango cha chini cha ubora wa madini ukilinganisha na uhalisia wa madini yenyewe,” amesema Dkt. Biteko.
Aidha, Dkt. Biteko amesema, kumeibuka kwa kundi la baadhi ya wafanyabiashara wa madini ya dhahabu wanaojihusisha na vitendo vya kuwatapeli wafanyabiashara wa nje ya nchi kwa kuwaomba fedha ili wawanunulie madini lakini wanashindwa kufanya hivyo na kujificha kwenye kisingizio kuwa wanaumwa Uviko-19 baada ya kupewa fedha.
Dkt. Biteko amesema kuwa, kundi hilo limekuwa likipokea fedha za ununuzi wa madini kutoka kwa wafanyabiashara wa nje ya nchi na kupiga picha maboksi ya madini yaliyofungwa siri za Wizara ya Madini ambazo ni feki na kuwatumia kwa njia ya mitandao kuwa mzigo uko njiani, jambo ambalo sio kweli na wanapotumiwa fedha wanazima simu zao.
“Hivi karibu amekuja mzungu ofisini kwangu analia kutapeliwa dola za Kimarekani 800,000 sawa na kiasi cha shilingi bilioni 7.2, tulipompigia simu mhusika aliyepatiwa fedha hizo alirusha maneno na kusingizia kuwa anaumwa ugonjwa wa korona jambo ambalo sio kweli," amesema Dkt, Biteko.
Pia, Dkt. amesema, hapo awali wafanyabiashara wa madini walikuwa wakituhumiwa katika shughuli ya utoroshaji wa madini na kusababisha serikali kukosa maduhuri lakini baada ya kulidhibiti jambo hilo kwa sasa wameibuka katika kuwatapeli wafanyabiasha fedha zao kwa madai ya kuwanunulia madini.
Sambamba na hayo, Dkt. Biteko amesema, kuna baadhi ya Masoko ya Madini yamekuwa yakifanya vema katika ukusanyaji wa maduhuri ya serikali ambapo Mwaka 2020/2021 Soko la Madini la Mkoa wa Geita liliongoza nchi nzima kwa kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 211.5, soko la pili ni Soko la Mkoa wa Mara ambalo lilikusanya kiasi cha shilingi bilioni 109.3 ikifuatiwa na Soko la Madini Mkoa wa Kimadini la Kahama ambalo lilikusanya kiasi cha shilingi bilioni 93.7.
Awali, Waziri Biteko alikutana na Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa Kumi na moja ya Kimadini ikiwemo Kahama, Mbogwe, Geita, Shinyanga, Mara, Simiyu, Mwanza, Singida, Kigoma, Kagera na Tabora ambapo aliwataka kuwa waaminifu katika shughuli zao baada ya kubaini mapungufu katika baadhi ya Mikoa hasa katika masuala ya usimamizi, ufuatiliaji na uaminifu.
Weka mkeka wa ushahidi hapa. Hizi mambo za kukaa nyuma ya keyboard na kurusha tu tuhuma, no!Jambo usilolijua na sawa na usiku wa kiza.
The guy is corrupt 100%.
Rushwa hutolewa mafichoni. Ushahidi wake huwa siyo rahisi sana. Lakini tunakuwa na uhakika kwa sababu ya taarifa za watoaji rushwa wenyewe. Unajua mtoaji rushwa hitoa au kwa sababu anaona asipofanya hivyo atapoteza haki yake, au anajua hana haki, anataka apate upendeleo.Sikatai, Wewe thibitisha tu mkuu, Mlarushwa hawezi kusemwa tu mpaka pamekuwa na Ushahidi,
#Rais anamifumo atamshika tu kama ni kweli,
Ushahidi wa tuhama zake, upo kwa wenye mamlaka. Angalao kwenye hilo nina uhakika wa 100%.Weka mkeka wa ushahidi hapa. Hizi mambo za kukaa nyuma ya keyboard na kurusha tu tuhuma, no!
khaaaaNaona PhD imeanza kuonekana kivitendo, Chapa kazi Biteko,
Hahaha, Dkt Biteko wewe Chapa kazi tu mkuu
😀 Siasa tamuNaona PhD imeanza kuonekana kivitendo, Chapa kazi Biteko,
Naona mnajiandaa na kuchukua fomu uchaoNaona PhD imeanza kuonekana kivitendo, Chapa kazi Biteko,
Hawezi kuzipata, hata akizipata haziwezi kufanya kazi maana jamaa dishi limeyumba vibaya sana!Na wewe tafuta akili
Toa ushahidi nyambafffYeye mwenyewe amekosa uaminifu. Na wasaidizi wake wanafuata nyayo zake.
Dr Msukuma Bado Hajaanza Kazi Nafikiria 2022 AtaanzaNaona PhD imeanza kuonekana kivitendo, Chapa kazi Biteko.