Dkt. Eliezer Feleshi awataka mawakili wa Serikali kujitathimini

Dkt. Eliezer Feleshi awataka mawakili wa Serikali kujitathimini

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Tanzania (AG), Dk Eliezer Feleshi amewataka mawakili wa Serikali kujitathimini kama wanaendana na dhima na kujitosheleza kwa nafasi walizopewa. Dk Felishi amesema hayo leo Jumatano, Septemba 28, 2022 wakati akifungua mkutano wa mawakili wa Serikali ulioandaliwa na ofisi yake.

“Jitathimini mwenyewe, kuna wagumu wa kujitathimini kwa sababu ni mabwana wasio na makosa, basi waambie wengine wakutathimini. Huwezi wewe kujitathimini weka mifumo ya wewe kupata mrejesho,” amesema.

Amesema kwa kuweka mifumo ya kujitathimini kiongozi atajua udhaifu wake upo wapi na kuchukua hatua ili aweze kwenda mbele. Pia, amewataka viongozi hao kuweka mikakati ya kujengeana uwezo kwa warsha, kuwasimamia, semina na mikutano.

“Kuna watu wa ajabu kabisa Mungu amekujalia umesoma, halafu hutaki wenzako waendelee, ni sawa na ibilisi kabisa. Kwasababu siku ya mwisho Mungu atakuhoji wangapi ulichangia wakaelewa kazi,” amesema.
 
Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Tanzania (AG), Dk Eliezer Feleshi amewataka mawakili wa Serikali kujitathimini kama wanaendana na dhima na kujitosheleza kwa nafasi walizopewa. Dk Felishi amesema hayo leo Jumatano, Septemba 28, 2022 wakati akifungua mkutano wa mawakili wa Serikali ulioandaliwa na ofisi yake.

“Jitathimini mwenyewe, kuna wagumu wa kujitathimini kwa sababu ni mabwana wasio na makosa, basi waambie wengine wakutathimini. Huwezi wewe kujitathimini weka mifumo ya wewe kupata mrejesho,” amesema.

Amesema kwa kuweka mifumo ya kujitathimini kiongozi atajua udhaifu wake upo wapi na kuchukua hatua ili aweze kwenda mbele. Pia, amewataka viongozi hao kuweka mikakati ya kujengeana uwezo kwa warsha, kuwasimamia, semina na mikutano.

“Kuna watu wa ajabu kabisa Mungu amekujalia umesoma, halafu hutaki wenzako waendelee, ni sawa na ibilisi kabisa. Kwasababu siku ya mwisho Mungu atakuhoji wangapi ulichangia wakaelewa kazi,” amesema.
Kwanza angeanza yeye kujitathmini.mahakama zenyewe zinaendeshwa na wanasiasa wa ccm,iwe mawakili.ukikutana na hao mawakili wana njaa ya kufa mtu, mishahara kiduchu unategemea watatoa haki.hata yeye anaishi kwa rushwa iwe mawakili ambao hawana mbele!hapa kinachotakiwa ni katiba tu hivyo lkn vinginevyo tunatwanga maji kwenye kinu
 
Kwanza angeanza yeye kujitathmini.mahakama zenyewe zinaendeshwa na wanasiasa wa ccm,iwe mawakili.ukikutana na hao mawakili wana njaa ya kufa mtu, mishahara kiduchu unategemea watatoa haki.hata yeye anaishi kwa rushwa iwe mawakili ambao hawana mbele!hapa kinachotakiwa ni katiba tu hivyo lkn vinginevyo tunatwanga maji kwenye kinu
Hehe... sidhani kama unamfahamu vizuri Jaji Feleshi wewe.
 
Kwanza angeanza yeye kujitathmini.mahakama zenyewe zinaendeshwa na wanasiasa wa ccm,iwe mawakili.ukikutana na hao mawakili wana njaa ya kufa mtu, mishahara kiduchu unategemea watatoa haki.hata yeye anaishi kwa rushwa iwe mawakili ambao hawana mbele!hapa kinachotakiwa ni katiba tu hivyo lkn vinginevyo tunatwanga maji kwenye kinu
Hio katiba itakomesha rushwa au? Kenya wanakatiba nzuri rushwa ikkoje?? Katiba bila usimamiz madhubuti wa kiuongoz hkna chochote, rushwa itaendlea kuwepo siku zote
 
Back
Top Bottom