TANZIA Dkt. Faustine Ndugulile, aliyekuwa Mbunge wa Kigamboni afariki Dunia

TANZIA Dkt. Faustine Ndugulile, aliyekuwa Mbunge wa Kigamboni afariki Dunia

Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile 1969-2024

Spika wa Bunge Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb) anasikitika kutangaza kifo cha Mbunge wa Kigamboni, Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile kilichotokea usiku wa kuamkia leo tarehe 27 Novemba, 2024 nchini India alipokuwa akipatiwa matibabu.

"Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mbunge wa Kigamboni na Mkurugenzi Mteule wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika, Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile. Kwa niaba ya Wabunge natoa pole kwa familia, wakazi wa Kigamboni na Watanzania wote. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi", amesema.

Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na familia inaendelea kuratibu shughuli za mazishi na taarifa zaidi zitaendelela kutolewa.

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA, APUMZIKE KWA AMANI.

Imetolewa na: Kitengo cha Mawasiliano na Elimu kwa Umma,
Ofisi ya Bunge,
DODOMA.
27 Novemba, 2024


View attachment 3162859

Huu ni Msiba Mkubwa sana hasa kwa Wanachama wa JamiiForums kwa kumpoteza Mwenzao Dr Faustine Ndugulile.
View attachment 3162839
Hivi karibuni, Dk Faustine Ndugulile Jumanne ya Agosti 27, 2024 alishinda nafasi ya Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Ukanda wa Afrika na alipaswa kuanza majukumu hayo mapya Februari 2025.
View attachment 3162854
View attachment 3162855
View attachment 3162860
Faustine Engelbert Ndugulile, alizaliwa 31 Machi 1969) ni mwanasiasa wa chama cha CCM nchini Tanzania na ni mbunge wa jimbo la Kigamboni tangu mwaka 2010.

Mnamo 1997 alipata shahada ya udaktari wa madawa katika Chuo kikuu cha Dar es Salaam na mwaka 2001 alipata shahada ya uzamili katika mikrobiolojia na chanjo katika chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Dk Ndugulile ni nani?
DK.FAUSTINE NDUGULILEA lizaliwa March 1969 Mbulu mkoani Manyara,Akapata elimu ya msingi na ya Sekondari nchini Zimbabwe na kisha kidato cha Tano na Sita katika shule ya Tambaza jijini Dar es Salaam.

Mwaka 1997 alipata shahada ya udaktari wa madawa katika chuo kikuu Cha Dar es salaam na mwaka 2001 alipata shahada ya uzamili ya mikrobiolojia na chanjo katika chuo kikuu Cha Dar es salaam.

Mtanzania huyu ni mwanachama wa chama cha Mapunduzi( CCM ) nchini Tanzania na ni mbunge wa jimbo la kigamboni tangu mwaka 2010.

Taaluma na kazi

Dk Ndugulile ni Daktari Tiba na ana Shahada ya Uzamili ya Tiba katika Tiba Mikrobiolojia na Kinga kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Shahada ya Uzamili ya Afya ya Umma (MPH) kutoka Chuo Kikuu cha Western Cape, na Shahada ya Kwanza ya Sheria (LL.B) kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Pia aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Afya ya Bunge la Tanzania, Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Mabunge ya Kimataifa (IPU) Advisory Group Health na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Mtandao wa Kamati za Afya za Bunge la Afrika (NEAPACOH).

Dk. Ndugulile aliwahi kuwa naibu waziri wa Afya wa Tanzania kati ya 2017-2020, pia aliwahi kuwa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 2020-2021.

Pia amefanya kazi kama mkurugenzi katika Wizara ya Afya Tanzania anayeshughulikia huduma za uchunguzi na pia meneja wa programu mwanzilishi wa Huduma ya Kitaifa ya Usambazaji Damu mwaka 2006.
Kati ya 2007-2010, aliwahi kuwa Mshauri Mkazi wa Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC) nchini Afrika Kusini akitoa msaada wa kiufundi kwa nchi nyingine nyingi kama vile Angola, Msumbiji, Tanzania na Rwanda.

APUMZIKE KWA AMANI
Hiyo ni kazi ya watu wa West Africa, wale watu ni hatari sana.
 
Wasifu wa marehemu Dkt. Faustine Ndugulile, Mkurugenzi mteule wa Shirika la Afya Duniani

faustine-1-905x613.jpg


Dkt. Faustine Engelbert Ndugulile ameaga dunia usiku wa kuamkia leo Novemba 27, 2024 nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu.

Dkt. Ndugulile alikuwa mtaalamu wa afya, mwanasiasa mahiri, na kiongozi wa mfano aliyetoa mchango mkubwa katika maendeleo ya sekta za afya, mawasiliano, na usimamizi wa kimataifa. Alizaliwa tarehe 31 Machi 1969, katika wilaya ya Mbulu, mkoani Manyara, Tanzania.


Elimu na Utaalamu

Dkt. Ndugulile alipata elimu ya hali ya juu na kuwa miongoni mwa wataalamu wa kipekee waliochanganya taaluma ya tiba na sheria. Alipata shahada ya Udaktari wa Tiba (MD) mwaka 1997 na Shahada ya Uzamili ya Tiba (MMed) mwaka 2001 kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mnamo 2010, alihitimu Shahada ya Uzamili ya Afya ya Umma (MPH) kutoka Chuo Kikuu cha Western Cape, Afrika Kusini, na mnamo 2022 alikamilisha Shahada ya Sheria (LL.B) kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.
Safari ya kisiasa na uongozi

Dkt. Ndugulile alijiunga na siasa mwaka 2010 alipochaguliwa kuwa Mbunge wa Kigamboni kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM). Aliongoza jimbo lake kwa kujituma, akitekeleza miradi ya kuboresha miundombinu, afya, na huduma za kijamii.

Kati ya mwaka 2007 hadi 2010, aliwahi kuwa Mshauri Mkazi wa Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC) nchini Afrika Kusini akitoa msaada wa kiutaalam kwa nchi nyingine nyingi kama vile Angola, Msumbiji, Tanzania na Rwanda.

Mnamo Oktoba 2017, Rais wa Tanzania wa wakati huo, Dkt. John Magufuli, alimteua kuwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee, na Watoto, akisimamia mipango muhimu ya kuboresha huduma za afya, hususan afya ya mama na mtoto.

Baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2020, aliteuliwa kuwa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari akiongoza kwa ubunifu, na kusisitiza matumizi ya teknolojia kuboresha maisha ya wananchi na kuimarisha uchumi wa kidijitali.

Mnamo Agosti 27, 2024, Dkt. Ndugulile alichaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, nafasi iliyompa heshima kubwa na Tanzania kwa ujumla kwani, ilimuweka mstari wa mbele katika kusimamia na kuimarisha mifumo ya afya barani Afrika, huku akitarajia kuanza kutumikia wadhifa huo mwezi Februari, 2025.
Pia alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Afya ya Bunge la Tanzania, Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Mabunge ya Kimataifa (IPU) Advisory Group Health na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Mtandao wa Kamati za Afya za Bunge la Afrika (NEAPACOH).

Dkt. Ndugulile ameacha watoto wawili, Martha na Melvin Ndugulile.

Dkt. Faustine Ndugulile atakumbukwa kama kiongozi shupavu aliyewakilisha Tanzania kwa heshima katika majukwaa ya kitaifa na kimataifa, akiwa mfano wa kuigwa kwa uadilifu na bidii. Mchango wake katika sekta ya afya, mawasiliano, na usimamizi utaendelea kuishi milele.
 
P
Kaka Faustine jamani, yaani huu msiba mwenzenu umenivuruga. Ni family friend. Nashindwa nampigia simu dada yake kumpa pole au naenda uwiii.
Hii familia wana roho nzuri, pamoja kuwa na pesa ila wana upendo sana. Vizuri havidumu 😭
Ulale mahala pema, peponi Kaka Faustine. Dah hee!!!
Poleni sana
Mungu awatie nguvu
 
Back
Top Bottom