Dkt. Kigwangalla: Wananchi wana haki ya kuikosoa Serikali, na hiyo iko kikatiba

Dkt. Kigwangalla: Wananchi wana haki ya kuikosoa Serikali, na hiyo iko kikatiba

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Waziri wa utalii Dkt. Kigwangalla amesema wananchi wana haki ya kikatiba ya kuisema na kuikosoa serikali iliyopo madarakani. Dkt Kigwangalla amesema yeye haoni tabu kukosolewa au kutukanwa mitandaoni kwa sababu hiyo ndio siasa yenyewe.

"Wizara hii hata nilipokuwa mbunge kabla sijateuliwa niliifahamu kuwa na matukio mbalimbali ya kutisha, ikifika wakati wake wa bajeti walikuwa wakiisubiria kwa hamu kuchangia na kulipua mabomu na kuwashambulia mawaziri na mawaziri walikuwa hawadumu muda mrefu"

“Hata nilipoteuliwa niliambiwa sidhani kama nitafika mbali, wakati nilipoteuliwa niliulizwa nitafanya nini ili nisitumbuliwe kama wengine, niliwaambia waniache nifanye kazi tutakutana mwaka 2020 ndio hii sasa nakwenda miaka miwili hadi mitatu sasa"

"Rais Dkt John Magufuli akikupenda sana atakutoa kwa heshima atakusemea mambo mengine hayo mengine hayasemi na ukiona upo kwenye wizara muda mrefu ujue yeye na vyombo vyake wanakufuatilia hadi wanajiridhisha huyu mtu hapigi pesa"

Dr Kigwangalla alikuwa akihojiwa katika studio za Clouds na watangazaji Babie Kabae na Sam Sasali.
Ametia nia ya kutetea jimbo la Nzega vijijini

Chanzo: Clouds 369

Eb0fR2CWkAEwW4R.jpg
 
Amepata baraka za jiwe kuongea hayo? Hiyo katiba ya wapi anayosema? Mbona hasemi pia katiba inaruhusu vyama vyote vya siasa kufanya siasa sio km ilivyo sasa ambapo chama chake cha kishetani kinatumia kila hila kuharibu amani ya nchi?
Kwanini kila siku wanabambika watu kesi?
 
Mzee anajitetea na kujipendekeza,kuna something anajificha nacho

Scare crow!
 
Waziri wa utalii Dkt. Kigwangalla amesema wananchi wana haki ya kikatiba ya kuisema na kuikosoa serikali iliyopo madarakani. Dkt Kigwangalla amesema yeye haoni tabu kukosolewa au kutukanwa mitandaoni kwa sababu hiyo ndio siasa yenyewe.

"Wizara hii hata nilipokuwa mbunge kabla sijateuliwa niliifahamu kuwa na matukio mbalimbali ya kutisha, ikifika wakati wake wa bajeti walikuwa wakiisubiria kwa hamu kuchangia na kulipua mabomu na kuwashambulia mawaziri na mawaziri walikuwa hawadumu muda mrefu"

“Hata nilipoteuliwa niliambiwa sidhani kama nitafika mbali, wakati nilipoteuliwa niliulizwa nitafanya nini ili nisitumbuliwe kama wengine, niliwaambia waniache nifanye kazi tutakutana mwaka 2020 ndio hii sasa nakwenda miaka miwili hadi mitatu sasa"

"Rais Dkt John Magufuli akikupenda sana atakutoa kwa heshima atakusemea mambo mengine hayo mengine hayasemi na ukiona upo kwenye wizara muda mrefu ujue yeye na vyombo vyake wanakufuatilia hadi wanajiridhisha huyu mtu hapigi pesa"

Dr Kigwangalla alikuwa akihojiwa katika studio za Clouds na watangazaji Babie Kabae na Sam Sasali.
Ametia nia ya kutetea jimbo la Nzega vijijini

Chanzo: Clouds 369

Kingwangala hataki tena ubunge na uwaziri? Manake siku hizi huwezi kumpinga yule boss ukaachwa.
 
Back
Top Bottom