Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli: Mimi sikuzaliwa Rais, Urais mlinipa ninyi

Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli: Mimi sikuzaliwa Rais, Urais mlinipa ninyi

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Mgombea Urais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Dkt John Magufuli ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano anayemaliza muhula wake wa kwanza amesema hakuzaliwa Rais.

Amesema Urais amepewa na wananchi ambao amesema kwa nguvu zao wameweza kufanikisha kukamilika miradi mbalimbali ya kitaifa na iliyofanyika Kilimanjaro.

Aidha amewaomba radhi kwa watu wa Mwanga, Same na Korogwe kutokana na kutokamilika kwa mradi wa maji unaohusisha Mwanga, Same na Korogwe ambao ilibidi uwe umekamilika mwaka 2017.

Kutokana na kuchelewesha kwa mradi huo, Magufuli ameahidi kusimamia mradi huo yeye mwenyewe. Kwa kuwa amesema alikuwa Waziri wa Ujenzi hivyo anajua kuwashughulisha makandarasi.
 
Kwanza alisema alikua anaujaribu tu urais na hakuna aliemlazimisha kuchukua form, Asa asitufokee hapa, aliingia kwa kura na atatoka kwa kura hizo hizo.... Hatutaki wanaojaribu cheo kikubwa namna hii afu wanaishia kutesa wananchi maskini!

......Meko Must Go in Burigi To Rest!
 
Si alituambia tusubiri kwanza aendeleze sehemu walizo mpa kura?
Sasa ana tuomba radhi kwa lipi?

Kura zetu bado hatuto mpa. Tunae ambae ata fanya kazi Tanzania yote kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania. Na kwa mujibu wa kiapo chake kwamba ata wahudumia Watanzania wote bila upendeleo.. Pole Magu, huwajui watu wa huo ukanda. Mkwara wako wa jana Same umekosea. Ungeenda kupiga mkwara kwenu Chato sio Kilimanjaro..
 
Nimeshapokea elf kumi kutoka CCM eti niwachague nami moyoni nasema ivi tar 28 namtandika Lissu livema likuuubwa (LLL)
Elfu kumi huku kwetu ni kura za watu kumi. Nipo Moto safarini Dodoma.
 
Urais alipewa na akina Modest Kapilimba, Januari Makamba, Abdulrahman Kinana na Nape. Hao ndiyo wana siri ni kura ngapi mwaka 2015 walizichota kwa Lowassa nakumhamishia yeye. Watanzania walimkataa kuanzia mwaka 2015.

Asitusingizie Watanzania, HATUKUMCHAGUA wala hatutamchagua tarehe 28/ 10/ 2020. Tunamtaka Tundu Lissu, na mwaka huu hatuibiwi kura
 
Africa's problems are not the people, but the leaders. Why are Africa countries not blessed with good leadership?.
Wewe mtoto umeandika Nini hiki?
"The people" "The leaders" (not all plural words start with The")

What is "Africa countries"?!!!

"Watanzania walio wengi hawajui kingereza" TL.
 
Back
Top Bottom