Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli: Natamani kufika kila eneo kufanya kampeni lakini siwezi

Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli: Natamani kufika kila eneo kufanya kampeni lakini siwezi

Anaogopa atakosa la kusema kuhusu bei ya korosho kwa sasa kwavile huu ndo wakati mwafaka wa msimu wa mauzo na wananchi wa mikoa hiyo wangependa kuona ahadi inayotekelezeka kuanzia sasa na si ahadi. Kiufupi Magufuli hana sera mpya juu ya maslahi kwa zao hilo na watu wakusini.
Ajabu Dr Magufuli akose la kusema kwa mambo mazuri aliyoyafanya kuhusu korosho ikiwemo kupandisha bei na kurudisha utaratibu wa zamani. Not possible
 
Dkt. Bashiru: Tumegusia maeneo ya uchaguzi, yeye alitaka kuzungumza na wagombea wetu wa Zanzibar na Muungano lakini nikamueleza nimetumwa mimi kuzumza nae kwa niaba yao kwa sababu wao wana kazi nyingi. Dkt Mwinyi anaendelea na kampeni na wameanza wamechelewa tarehe 12 mwezi wa tisa na Rais Magufuli ratiba yake nae pia ni nzito na ina kazi nyingi za uongozi nchi pamoja na kampeni.

Na nikamueleza ndio maana hakuweza kwenda katika baadhi ya mikoa ikiwemo Pemba, Ruvuma, Katavi, Rukwa, Lindi Mtwara na Morogoro.

===========

Akitoa taarifa kupitia vyombo vya habari Dr Bashiru katibu mkuu wa CCM ametangaza kua Dr Magufuli hatoweza kufika mikoa ya lindi,Mtwara na Ruvuma.

Sababu alizotoa ni kua mgombea mwenza alishafika huko (Mama Samia Suluhu)

Akimaliza ratiba ya DSM ataelekea Pwani, Tanga, Kilimanjaro, Manyara na kumalizia Dodoma.

Swali ninalojiuliza Dr Magufuli ana mpango gani na mikoa ya kusini?mbona sio kawaida kwa mgombea Urais kutokufika kabisa kanda fulani wakati wa kampeni.

Je, hii ni fursa kwa Tindu Lissu kwenda kuvunja kabisa ngome za CCM mikoa ya kusini ?Kama kumbukumbu ziko sawa Dr Magufuli ziara zake mikoa ya kusini alirudi na uchovu mara ya mwisho alipoenda na pia ni eneo muhimu sana kimkakati kwa sababu kuna ngome za CUF ambazo zimehamia mikononi mwa ACT, tatu Membe anatoka mikoa ya huko na la mwisho ambalo ni muhimu sana Kuna suala la siasa ya zao la korosho bila kusahau gesi ambayo wananchi walipigwa ipasavyo miaka ya 2012 huko.

Ni mimi mpenda haki, Uhuru na maendeleo, nikiripoti kutoka kichakani.
 
Labda kama anataka kisafisha mazingira ya Kazi na kupitisha mikataba yaki-Mangungo dakika za Mwisho Mwisho Ili akichomolewa awe ameshajiwekea mazingira vzr.

Haiingii akilini kipindi hiki Kampeni zimepamba Moto yeye akatulie ofisini, what a confidence??

Anamtegemea Waziri Mkuu, ni Illegal Waziri Mkuu kufanya Kampeni. Na Anafanya Kampeni Kwa Ratiba ipi wakati Tume haimtambui?
 
Itoshe kusema upinzani this time mtaanguka vibaya kaskazini, msijipe matumaini yasiyokuwepo kwa kuangalia historia ya kaskazini
Brother Siasa ni Science kabisa, ndio kuan ile inaitwa Political Science; Ishu ya Kaskazini hasa sehemu za mijini sio mtu, ishu ni Chama, ishu ni CCM, lakini pia Kuna kauli zimekuwa zikitolewa kwamba ukichagua Upinzani Maendeleo hayatakuja; Hizi kauli kwa upande wa kaskazini hazifanyi kazi; Kwani miundombinu michache iliyowekwa inawafanya wananchi waanzie hapo hapo, pasi na kusubiri maendeleo mengine.

Moshi mjini na Karatu ni moja wapo ya Majimbo ambayo tangu Mfumo wa Vyama vingi uanzishwe, hayajawahi kuwa chini ya CCM na maendelea yapo; Hivyo kwa watu wenye uelewa mzuri kauli kama izi hawatazikubali; Kwani kinachosemwa na experience walionao haiingii Akilini.

Kama CCM ile chini ya Mdogo wangu Kinana mastermind, ilishindwa kutoboa 2010, 2015. Kwa Arusha hata mimi simkubali Lema kwenye Ishu ya Perfomance Lema hamwingii Gambo, lakini pia Hamwingii Mgombea aliyepita; CCM imekuwa ikisimamisha Potential Candidates lakini ishu ni Chama; Inabidi wakishachukua nchi, wahakikishe wanaendelea kuonyesha upendo kwa wananchi ijapokuwa jimbo lipo upinzani, hapo wataweza ku-win; Maana Hiyo Wakionyeshe chama kwamba bado wako nao pamoja kichama, sio kiserikali;
Political Science inahitajika iwe Applied huko Kaskazini, kuliko mabavu.
 
Akihutubia jimbo la Kawe, Rais Magufuli amesema yeye ni Binadamu hataweza kwenda lindi na Mtwara hivyo atamtuma Kassim Majaliwa Kassim

Mimi kama mwana CCM naunga mkono kumtumia Mama Salma Kikwete na Jakaya Kikwete mikoa ya lindi na Mtwara na tayari hilo limefanyika....
Anaogopa ya Kagera yasimkute tena.Amepora watu korosho hajawalipa angeenda kuwaambia nini. Si mseme tu ukweli?
 
Ccm oyeee

Wakuu nimeshangazwa na hatua ya mwenyekiti wetu wa ccm taifa kuamua kutokwenda kuomba kura katika mikoa ya lindi mtwara na ruvuma .hivi kati ya katoro na mkoa wa mtwara ni wapi palikuwa na umuhimu wa kwenda.

Haya sasa isitoshe anasema yeye ni mwenyekiti wa ccm taifa lakini tunashangaa huku Zanzibar na pemba hatofika.sisi wanaccm ndio tunaoteseka huku mitaani hawatuelewi kabisa...
 
Haijawahi tokea mgombea wa ccm tangu nchi hii iumbwe kuacha kwenda kusini kuomba kura sasa atashindaje sasa
 
Rais Magufuli angepumzika ofisini

Sisi Watanzania tunampenda sana kura zote kwake
 
Gari ya Njaa ukianza tatizo kipindi kile siku 2 kampeni, siku 10 mapunziko.
 
Back
Top Bottom