Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli, Oktoba atavuna alichopanda

Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli, Oktoba atavuna alichopanda

Kipi usichoelewa kwenye mada.

"Atavuna alichopanda." Ulitaka avune bangi alipopanda mchicha?

Buku 7 tu hizo hadi akili mnashikiwa?

Kwamba yeye hajui atakachovuna? Majuha wa wapi nyie?

Au ulitaka tumhakikishie kuwa hatavuna alivyopanda?
Tatizo la NYUMBU ndio hilo tu. Umejaa povu hovyo kabisa
 
Nakutakia mafanikio mema

Unanitakia mimi mafanikio? Utakuwa mburula kweli kweli.

Kujitoa ufahamu kwa sababu ya njaa zenu siyo applicable kwa kila mtu.

Barabara hii mwenye maslahi nayo ni miye? Ya nyani bwege kuchekelea miti ikiungua kumbe ni ya kweli.

Fungeni kabisa na bandari ya Dar mtakuwa mmenikomoa kweli kweli!
 
Yeye alivyokuwa anawafanyia ujeuri wananchi alijua hatutakutana, ndio tumekutana atakula jeuri yake
 
Unanitakua mimi mafanikio? Utakuwa mburula kweli kweli.

Barabara hii mwenye maslahi nayo ni miye? Ya nyani kuchekelea miti ikiungua kumbe ni ya kweli.

Fungeni kabisa na bandari ya Dar mtakuwa mmenikomoa kweli kweli!
We dogo, acha mihemko ya uchadema! Hapo ndipo unaharibu. Nyie na Mwendawazimu wenu Tundu Lissu hamtaki kila kitu alichokifanya JPM? Hiyo barabara nakuhakikishieni itatengenezwa tu
 
Yeye alivyokuwa anawafanyia ujeuri wananchi alijua hatutakutana, ndio tumekutana atakula jeuri yake

Ajabu kuwa yeye na wapambe wake wanadhani tumeshasahau hata tu kuwa wapo waliopotea, waliojeruhiwa kinyama na hata kukutwa kwenye viroba.

Achilia mengi mengine aliyopanda yeye na wapambe wake.

Sasa wanataka au wanategemea wavune nini kama walichopanda ni mbaazi?
 
We dogo, acha mihemko ya uchadema! Hapo ndipo unaharibu. Nyie na Mwendawazimu wenu Tundu Lissu hamtaki kila kitu alichokifanya JPM? Hiyo barabara nakuhakikishieni itatengenezwa tu

Dogo nikiwa miye, wewe utakuwa kibaka miezi wa kuku.

Kumbe hii barabara itatengenezwa? Si mmekuwa mnawahimiza wengine wajikite kwenye waliyoifanyia jamii si watakayofanya?

Tayari mmeshasahau? Bendera fuata upepo?

Mnaleta mikakati ya kushinda mechi iliyokwisha chezwa? Mnataka kujifunika shuka sasa wakati kumekwisha kucha?

Jidanganyeni pamoja naye Ila uhalisia utabakia ukiwa mweusi na mweupe:

Ataadhibiwa vilivyo kwani pamoja na kuitelekeza barabara hii kwa kipindi chote hali akiwekeza kwao miradi isiyokuwa na vipaumbele yapo mengi ambayo anawajibika moja kwa moja. Ndiyo maana atavuna kila alichopanda!

Hiyo ndiyo habari yenyewe.
 
Back
Top Bottom