Dkt. Mataragio: Tunaimarisha mazingira ya uwekezaji na miundombinu ya nishati ili kufikisha huduma kwa wote

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio amesema Serikali inaendelea kuimarisha mazingira ya uwekezaji na miundombinu ya Sekta ya Nishati nchini ili kuwezesha wananchi kufikiwa na huduma stahiki bila kujali umbali na vipato vyao.

Dkt. Mataragio ameyaeleza hayo jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya utoaji Tuzo kwa Mawakala na Wadau wa Kampuni ya Puma Energy Tanzania ambayo inaunga mkono juhudi za Serikali za kuelimisha jamii kuhusu matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kupitia bidhaa za Puma Gas.

Dkt. Mataragio amesema moja ya majukumu ya Wizara ya Nishati ni kukutana na wadau mbalimbali wakiwemo watoa huduma na watumiaji ili kuimarisha ushirikiano kati ya sekta binafsi na Serikali utakaopelekea utoaji wa huduma bora kwa wananchi ikiwa ni moja ya vipaumbele vya Serikali.

Katika hafla hiyo, Dkt.Mataragio ameipongeza kampuni ya Puma kwa jitihada zinazounga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali katika kuhamasisha jamii ili itumie Nishati Safi ya Kupikia na hivyo kutimiza lengo la asilimia 80 ya Watanzania kutumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034.

Amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa Balozi na kinara katika kuhamasisha matumizi ya Nshati Safi ya Kupikia nchini na Duniani ili kuhakikisha Watu wanaondokana na matumizi ya kuni na mkaa ambao una madhara kwa afya na kusababisha uharibifu wa mazingira.

Kuhusu Tuzo hizo zilizotolewa na Puma Energy Tanzania kwa Mawakala na Wadau mbalimbali nchini, Dkt.Mataragio ameelekeza kuwa ziwe chachu ya kuendelea kufanya kazi kwa weledi na ufanisi kulingana na vigezo na mashariti ya Kampuni kwa maslahi ya jamii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…