#COVID19 Dkt.Mollel: Msiogope maneno ya Mtandaoni kuhusu Chanjo. Wataondoka na goli 0

#COVID19 Dkt.Mollel: Msiogope maneno ya Mtandaoni kuhusu Chanjo. Wataondoka na goli 0

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Godwin Mollel amewataka wananchi kutokuogopa maneno yanayoendelea mitandaoni kuhusu chanjo ya Uviko-19 kwani chanjo hiyo ni salama.

Dk Mollel amesema hayo katika mkutano mkuu wa wadau wa huduma za elimu ya afya kwa umma uliofanyika jijini hapa.
Amesema Tanzania ni Taifa la Mungu hivyo hatma yake iko mikononi kwa Mungu huku akiwataka kuchapa kazi na kuwasihi waandishi kuzingatia maudhui yanayofaa kurusha kwenye vyombo vya habari.

"Msiogope yanayoendelea mitandaoni na kwenye vyombo vya habari ni kawaida tu, mambo yatakaa vizuri…Mkachape kazi hayo mengine mtuachie sisi maronaldo wenu wao watakuja na wataondoka wakiwa wamefunga goli 0…Hali ya chanjo inaenda vizuri tunaweza kuwaacha wapumbavu na wajinga tukaenda nao,"amesema.

Katika kutoa elimu kwa umma aliwataka wadau hao kuwashirikisha watu maarufu, wasanii na viongozi wa dini ili kufikisha elimu kwa umma kuhusu umuhimu a chanjo ya Uviko 19 hasa sehemu za vijijini.

Aliwataka wadau kutokujielekeza katika kufanya semina na makongamano na badala yake bajeti iliyowekwa itumike kuwawezesha wadau kuwafikia wananchi ili kutoa elimu ya afya kwa umma na chanjo ya Uviko-19.


Mwananchi
 
"Tunaweza kuwaacha wapumbavu na wajinga tukaenda nao" Dk. Mollel.

Wapumbavu hawabadiliki hata wakichezewa ngoma, lakini wajinga hubadilika.

Sijui yule jamaa anaeogopa kukalia kiti cha kamati na kutumia "mic" ya kamati huku kila siku akituaminisha analindwa na damu ya Yesu atakuwa kundi gani kati ya hayo mawili.
 
Mbona ni kama amehamaki? Kwani kalazimishwa azungumzie hali iliyko mitandaoni?

Kama hawezi kazi si ajiondoe
 
Ni aibu nyingine, kwanini waziri asitoe elimu na si kutumia lugha za matusi?

Inashangaza sana mtaalamu kushindwa kutoa majawabu ya kisayansi kulingana na utaalamu wake lakini wanaishia kutoa maneno ya udaku na yasiyofaa!!

Hii inaprove WEAKNESSES kwa viongozi wetu, na tena kama Waziri Mollel akumbuke Watanzania walimsikia alipokuwa ana challenge suala la chanjo leo amefunika macho bila haya ndio maana anaishia kutoa matusi!!

Tuelimisheni, acheni kutumia mabavu bali jibuni hoja na Kama hakuna namna ya kujibu it's better mkanyamaza!!
 
YUKO SAWA💯%💪🇹🇿👍
"Only Stupid People Don't Change Their Minds"..😷😷.. Boutros Boutros-Ghali
Former Secretary-General of the United Nations
 
Nani anawapa jeuri hawa viongozi wa umma kuwatukana wananchi walio wachagua? Naibu Waziri ajue serikali ni watu na cheo ni dhamana. Siku wananchi wakiamua ataondoka yeye na anaye mpa kiburi kutukana wananchi. Cheo chenyewe cha kisiasa kinakupa kiburi. Bakhresa siangekuwa anatembea juu ya vichwa vya watu.
 
Huyu N/waziri huwa namuona kama ana upungufu fulani kichwani mwake (taahira). Ongea yake inathibitisha ninachokisema. "Mungu anisaidie kama dhana yangu siyo sahihi.
 
Sisi wapimbavu hatuchanji ndio msimamo wetu...
 
Tatizo lilianzia kule kuhusu chanjo eti siyo salama,, eti pigeni nyungu, kuleni malimao, chemsheni tangawizi na vitunguu swaumu hawa Mungu anawaona, leo hii wamebadilika kabisa tena kabisa aki ya Mungu nyie CCM Mungu anawaona mnatufanya vinyago ss..
 
Huyu naibu Waziri anguko lake limekaribia.Alipoongea maneno ya shombo kuhusu Askofu Kitime nilimwona ni bonge la bogus.
 
Back
Top Bottom