Dkt. Mpango: 26.4% ya Watanzania wanaishi chini ya kiwango cha umasikini wa kipato

Dkt. Mpango: 26.4% ya Watanzania wanaishi chini ya kiwango cha umasikini wa kipato

Maisha bora kwa kila Mtanzania?
Mbona hatukuyaona kwa Jakaya ambaye ndiye mwanzilishi wa kaulimbiu hiyo katika kipindi cha utawala wake?
 
W
Watanzania wameathiriwa kisaikolojia. Wamefanywa kuamini kwamba kupambania haki zao ni kuvunja sheria hivyo wamechagua kuwa wapole ili wasivunje sheria.

Otherwise demokrasia ni ya makaratasi tu.
Mtanzania hutakiwi muonea huruma,
Kama watu wamepiga Bilioni 480 kisa wamechelewesha kulipa wakandarasi wategemea nini?

Hizo pesa zilikuwa zinaweza jenga
Madarasa 24,000, ambayo yangetoa shule 1200

Hapo tumechukulia kila Darasa lijengwe kwa 20Mil, kila shule iwe na Madarasa 20
Hapo hayo Madarasa Mapya yangetosha wanafunzi Milioni 1, kama kila darasa litabeba wanafunzi 45 kama sera ya elimu esamavyo.

Ingejenga Vituo ya Afya 1200, hivi vituo vya Afya vingewekwa 6 kwenye kila wilaya.

Ingejenga Vituo vya Afya 3200, kwamba kila wilaya ingepata vituo 16

Ingejenga nyumba za walimu 16,000

Hizo pesa zingetosha kujenga barabara za lami KM 200-400, maana yake Barabara kutoka Igawa hadi Tunduma ingewezekana kabisa

Sasa angalia hayo yote afu watu wametulia tu hawahoji, wala hawaoni mtu aliyewajibika, waziri wa fedha yupo, wa ujenzi yupo
 
MCHAKATO WA MAANDALIZI YA DIRA YA MAENDELEO YA TAIFA WAZINDULIWA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. dr_mpango ametoa maagizo sita ya kuzingatiwa katika Maandalizi ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, ikiwemo kuimarisha uwezo wa uchumi uliopo na kulinda mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025.

Alitoa maagizo hayo jijini Dodoma wakati wa akizundua Mchakato wa Maandalizi ya dira mpya ya Maendeleo ya Taifa 2050.

Alisema maandalizi hayo pia yazingatie matumizi ya fursa ambazo hazijatumiwa ipasavyo hadi sasa na kuzikamata fursa zinazochipukia huku akitolea mfano kilimo, mifugo na uvuvi, mazao ya misitu, uongezaji thamani ya mazao pamoja na uvunaji wa rasilimali za kimkakati na kujenga viwanda.

“Katika kilimo Tanzania inafursa ya kuwa ghala la chakula katika Bara la Afrika na hata mashariki ya kati na duniani kama tukilenga uzalishaji mkubwa wa mahindi, ngano, shayiri, maharage ya soya, sukari, mafuta ya kupikia, korosho, matunda, mbogamboga na viungo ”, alibainisha Mhe. Dkt. Mpango.

Mhe. Dkt. Mpango alisema maamdalizi pia yazingatie suala la elimu, hususani elimu ya sayansi, elimu ya ufundi na ufundi stadi, utafiti na maendeleo na ubunifu ili kukuza ujuzi na uwezo wa nguvu kazi ya Taifa.

“Jambo la nne ni namna gani tutavutia na kuasili teknolojia ili kukuza tija katika sekta zote za uzalishaji na kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi ikiwa ni pamoja na kuingia ubia wa kimkakati ili kuiwezesha Tanzania kuwapita washindani wetu katika kipindi kifupi” , aliongeza Mhe. Dkt. Mpango.

Alisema kubaini uhalisia wa rasilimali zote zitakazo hitajika kuwezesha utekelezaji makini wa Dira mpya na utekelezaji wa mipango, pamoja na kubainisha mfumo thabiti wa ufuatiliaji na tathimini kwa kuangalia vigezo mahsusi vilivyowekwa.

Mhe. Dkt. Mpango alisema ni vema timu zilizoundwa zikajifunza kutoka katika nchi zilizoendelea kwa kasi kuanzia miaka ya 1960 hususan zile za Bara la Asia pamoja na kuangalia namna nchi nyingine zilivyoweza kujikwamua kutoka katika uchumi wa kati.

Alisema ni matumaini ya Serikali kuwa wananchi wote watapata nafasi ya kutoa maoni yao katika mchakato wa maandalizi ya Dira mpya ambayo inayotarajiwa kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi na kijamii.

“Vile vile makundi mahsusi kama vile Bunge, Mahakama, Sekta Binafsi, Idara za Seriali, Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Taasisi za Elimu, Asasi za Kiraia na Watanzania waishio ughaibuni na washirika wetu wa maendeleo watapatiwa muda wa kutosha kushiriki mchakato huu muhimu”, alibainisha Mhe. Makamu wa Rais.

Aidha, aliagiza Wizara zote, Taasisi za Umma, wakala wa Serikali, Idara zinazojitegemea, Sekretarieti za mikoa na Serikali za Mitaa, Sekta Binafsi, Wanadiaspora na Wadau wa Maendeleo kutoa ushirikiano kwa timu ya maandalizi ya Dira mpya ya Maendeleo 2050 pale watakapohitajika kufanya hiyo.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb) alisema utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 umefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika nyanja za uchumi, elimu, afya, miundombinu, umeme, mawasiliano na michezo.

Alisema kabla ya utekelezaji wa Dira iliyopo sasa makusanyo ya kodi kwa mwezi yalikuwa Sh. bilioni 30, lakini baada ya utekelezaji wa Dira hiyo makusanyo kwa mwezi yamefikia zaidi ya Sh. trilioni 2.

“Kabla ya Dira umeme ulikuwa unakutanao makao makuu ya mikoa na makao makuu ya wilaya chache, sasa tunaongelea idadi ndogo ya vijiji na vitongoji ambavyo havijapata umeme baada ya utekelezaji wa Dira”, alibainisha Mhe. Dkt. Nchemba.

Kuhusu suala la elimu Mhe. Dkt. Nchemba alisema kabla ya utekelezaji wa Dira ilikuwa ni jambo la kawaida wanafunzi waliomaliza elimu ya msingi kutochaguliwa kujiunga na elimu ya Sekondari lakini sasa wanafunzi wanaomaliza wanajiunga na elimu ya Sekondari.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba alisema utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 umewezesha nchi kufikia mafanikio mbalimbali ikiwemo kuingia katika uchumi wa kati wa hadhi ya chini ambapo Taifa lilifanikiwa kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi kwa wastani wa asilimia sita na kupungua kwa kiwango cha umaskini kwa zaidi ya asilimia tisa kutoka asilimia 35.7 mwaka 2000/01 hadi asilimia 24.6 mwaka 2017/18.

Alisema vifo vya mama na watoto nchini vimepungua kutoka vifo 854 kwa vizazi 100,000 na vifo 99 kwa vizazi 1,000 mtawalia mwaka 2000 hadi vifo 524 kwa vizazi 100,000 na vifo 36 kwa vizazi 1,000 mtawalia mwaka 2020.

“Kiwango cha udahili wa wanafunzi wa elimu ya msingi kimeongezeka kutoka asilimia 58.8 mwaka 2000 hadi 95.7 mwaka 2020; upatikanaji wa maji umeongezeka kutoka asilimia 50 mwaka 2000 hadi asilimia 86.7 mwaka 2020 kwa mijini na asilimia 55 mwaka 2000 hadi asilimia 72.3 mwaka 2020 kwa vijijini; na upatikanaji umeme vijijini umeongezeka na kufikia asilimia 69.8 mwaka 2020”, alibainisha Dkt. Mwamba.

Kuhusu maandalizi ya Dira 2050, Dkt. Mwamba alisema maandalizi hayo yametokana na mambo manne ikiwemo kuelekea ukomo wa utekelezaji wa Dira 2025, kuendeleza mafanikio yaliyofikiwa kutokana na utekelezaji wa Dira 2025, uhitaji wa mkakati utakaowezesha nchi kunufaika na maendeleo ya kiuchumi na kiteknolojia yanayoendelea kuibuka duniani.

“Masuala kama vile uchumi wa buluu, matumizi ya roboti, biashara ya hewa ukaa) pamoja na uhitaji wa Mkakati utakaoanisha Agenda ya Maendeleo ya nchi na mikakati mingine ya Kikanda na Kimataifa ambapo Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 itahakikisha kuwa Tanzania inaendelea kuoainisha Agenda yake ya Maendeleo na Agenda na Mikakati ya Kimataifa”alisema Dkt. Mwamba

Alisema maandalizi ya Dira hiyo yanajumuisha tathmini ya utekelezaji wa Dira 2025 kwa kuwa tathmini hiyo ni muhimu katika kuainisha mafanikio, hatua za utekelezaji na changamoto zilizojitokeza kipindi cha utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025.
 
Lakini kwa Muumba wataenda kusemaje yaani kiongozi anaoga Maji ya juu na swimming pools Maji yake yatibiwa kwa gharama kubwa huu watu wake au ndugu zao wanakunywa Maji ya dimbwii na kulala Nyumba za tembe hata choo Hana lakini huyo kiongozi akisafiri analala huko abrodi mahotel za royal na kula mabaga wakati waliompigia kura wanakunywa Maji ya madimbwi na vipeyuu
Mungu wako si mungu wao. Wanachofanya ndio haswa wanatekeleza malengo na matakwa ya mungu wao.

Siku yao haiko mbali sana, wacha waendelee kututesa.
Yaani nimekaa iramba nduguti
 
kuchoshana tu. Dira kibao zimepita. Tupate kwanza tathmini ya utekelezaji wa hizo zilizopita.
 
Mtanzania hutakiwi muonea huruma,
Kama watu wamepiga Bilioni 480 kisa wamechelewesha kulipa wakandarasi wategemea nini?

Hizo pesa zilikuwa zinaweza jenga
Madarasa 24,000, ambayo yangetoa shule 1200

Hapo tumechukulia kila Darasa lijengwe kwa 20Mil, kila shule iwe na Madarasa 20
Hapo hayo Madarasa Mapya yangetosha wanafunzi Milioni 1, kama kila darasa litabeba wanafunzi 45 kama sera ya elimu esamavyo.


Ingejenga Vituo ya Afya 1200, hivi vituo vya Afya vingewekwa 6 kwenye kila wilaya.

Ingejenga Vituo vya Afya 3200, kwamba kila wilaya ingepata vituo 16

Ingejenga nyumba za walimu 16,000

Hizo pesa zingetosha kujenga barabara za lami KM 200-400, maana yake Barabara kutoka Igawa hadi Tunduma ingewezekana kabisa



Sasa angalia hayo yote afu watu wametulia tu hawahoji, wala hawaoni mtu aliyewajibika, waziri wa fedha yupo, wa ujenzi yupo
Inatia Hasira sana yani.
 
Eti Serikali inazindua mchakato wa maandalizi ya Dira 2050 badala izindue Dira Kamili.

Sasa hapo ndio nini hasa? Kwa nini tusifanye kazi zingine za maana ?
20230404_083548.jpg
 


Dkt. Philip Mpango, Makamu wa Rais wa Tanzania amesema “Malengo makuu ya dira ya Mwaka 2025, Maisha bora kwa kila Mtanzania, Kudumisha amani, usalama na umoja katika Nchi, Utawala bora, Jamii iliyoelimika vyema na inayojifunza, tano ni uchumi imara na shindani.”

Pamoja na hatua kubwa ambayo Nchi imepiga bado kuna changamoto mbalimbali zilizosababisha malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2000-2025 kutofikiwa kikamilifu mfano:

“Changamoto ya umasikini wa kipato na lishe duni, kwa mujibu wa utafiti wa Mapato na Kaya, takribani 26.4% ya Watanzania wanaishi chini ya kiwango cha umasikini wa kipato, ambayo ni zaidi ya Robo na Wananchi masikini zaidi wanaishi vijijini 31.3%.

Kuna mikoa, nitataja michache Kagera, Kigoma, Singida, Tabora na Dodoma ambayo kiwango cha umasikini ni kikubwa zaidi kwa sababu mbalimbali kutokana ikiwemo matatizo ya Kihistoria na miundombinu duni.

Aidha, tofauti ya kipato miongoni mwa Watanzania imeendelea kuongezeka licha ya kufanya vizuri katika kigezo cha kufanya vizuri uchumi jumla.

Kiwango cha tofauti ya kipato kwa kutumia kipimo cha uwiano kiliongezeka kutoka 0.34 Mwaka 2011/12 mpaka 0.38 Mwaka 2017/18.

Katika kipindi kama hicho, kipimo hicho cha tofauti ya kipato kwa maeneo ya Mijini nacho kiliongezeka kutoka 0.37 hadi 0.41.

30% ya Watoto chini ya miaka mitano wana udumavu Nchini
Akizungumza katika uzinduzi wa Mchakato wa Maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango amesema takwimu hizo ni kwa mujibu wa utafiti wa Mapato na Kaya.

Amesema “Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na viashiria vya Malaria kwa Mwaka 2022 unaonesha kuwa 30% ya Watoto wenye Umri chini ya miaka mitano wana udumavu na 9% ya Watoto wana udumavu mkali.”


Dkt. Mpango: Elimu yetu haikidhi mahitaji ya soko la ajira
Kwa upande wa kuwa na jamii iliyoelimika na inayojifunza, tumepata mafanikio ya kuridhisha ikiwemo kuongezeka kwa Wanafunzi katika ngazi zote za elimu.

Viwango vya ufaulu vimeongezeka, uwezo wa kusoma na kuandika Nchini unakadiriwa kuwa 92%.

Pamoja na mafanikio hayo bado vijana wengi wanaomaliza masomo hawapati fursa za ajira, pia elimu yetu haikidhi mahitaji ya soko la ajira wala kuwezesha wahitimu kujiajiri.

Jitihada za kurekebisha hali hiyo zinaendelea ikiwemo kupitia sera ya elimu na mitaala.

Ni wachache sana hao.
 
Kwa mujibu wa utafiti wa Kipato Cha Kaya Mikoa mingine ni

Kigoma,
Singida,
Dodoma,
Tabora
Kagera.

 
Kiwango cha chini ya umaskini, it means kaya ama familia moja hata wangepewa wiki mbili hadi tatu kulipa deni la buku, wataishia jela tu.

Actually, siyo umaskini tena, bali ni UFUKARA - abject poverty. Hii ni hali ambayo mtu hawezi tena kujihudumia mwenyewe. Anakuwa tegemezi left, right, and centre. Mercy!
 
VP Mpango, mtu mnyenyekevu, mcha Mungu, msema kweli na nguli wa uchumi.

I really hope kati ya Mpango au Majaliwa mmoja wao akwee pale juu baada ya mama kumaliza kazi yake.

Unawezaje kumtofautisha Mpango na Jiwe? Unafahamu kuwa ile report ya matumizi ya fedha Wakati Jiwe yuko mahututi ilimtaja Mpango kuwa mhusika mkuu na ndio maana Samia akapata kigugumizi hajaiweka hadharani mpaka leo!!
 
Back
Top Bottom