Dkt Mvungi: Muungano Ulishavunjika!

Dkt Mvungi: Muungano Ulishavunjika!

Hivyi ninyi mnamlalamikia nani?
hakuna kiongozi wa nchi hii ambaye anajali masuala ya muungano.
Dawa ni kwenda mahakamani kuishtaki jamhuri na serikali ya zanzibar kwa kutishia uhai wa UWEPO WA TANZANIA

Uhai wa uwepo wa Tanzania kwa masilahi gani iwapo hakuna anayeujali?
 
Wanaonyanyaswa ni Tanganyika ambao hawana serikali yao katika muungano. Na bado mambo yanageuzwa eti Zanzibar inanyanyaswa! Aidha serikali tatu au hakuna muungano. Ni hivyo tu.
 
Wanaonyanyaswa ni Tanganyika ambao hawana serikali yao katika muungano. Na bado mambo yanageuzwa eti Zanzibar inanyanyaswa! Aidha serikali tatu au hakuna muungano. Ni hivyo tu.

Serikali tatu zitaondoaje umaskini wetu?Au tunachukuliwa na upepo wa kisiasa tunasahau faida ya tunachokitaka?
 
mIMI KWA MAWAZO YANGU TURUDI KULE KULE KWA mWANZA SERIKALI TATU TANGANYIKA,ZANZIBAR NA MUUNGANO Sasa hapa ndo tujadili kwani Anayosema DK. Mvungi all is wright!! but Sisi ambao hatukusoma walalaloi tukipewa Khanga na T shirt basi CHochote anachotaka Mwenyekiti Ruksaa :mad2:
 
mIMI KWA MAWAZO YANGU TURUDI KULE KULE KWA mWANZA SERIKALI TATU TANGANYIKA,ZANZIBAR NA MUUNGANO Sasa hapa ndo tujadili kwani Anayosema DK. Mvungi all is wright!! but Sisi ambao hatukusoma walalaloi tukipewa Khanga na T shirt basi CHochote anachotaka Mwenyekiti Ruksaa :mad2:

Kisha tutafaidika nini na serikali tatu? Jamani wanaodai serikali tatu msiishie tu kwamba "tunataka serikali tatu." Hizo Serikali tatu mzi-link na maendeleo, ndio mtaeleweka!
 
Jumanne , 7 Septemba 2010 kuna mjadala iliyopangwa kufanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee iliyotayarishwa Kituo cha sheria na haki za Binadamu kwa kushirikiana Kituo cha Huduma za Sheria cha Zanzibar.

Mada kuu:
* mapungufu yaliyoko katika katiba ya Jamhuri wa Muungano Tanzania ya Mwaka 1977
*Mabadiliko ya Kumi ya Katiba za Zanzibar.

Mjadala utaongozwa na mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuuu cha Dar Es Salaam na mada zitatolewa na mabingwa wa sheria na katiba.

SEE: Advert on Mwananchi, september 5, 2010, Page 5
 
Jumanne , 7 Septemba 2010 kuna mjadala iliyopangwa kufanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee iliyotayarishwa Kituo cha sheria na haki za Binadamu kwa kushirikiana Kituo cha Huduma za Sheria cha Zanzibar.

Mada kuu:
* mapungufu yaliyoko katika katiba ya Jamhuri wa Muungano Tanzania ya Mwaka 1977
*Mabadiliko ya Kumi ya Katiba za Zanzibar.

Mjadala utaongozwa na mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuuu cha Dar Es Salaam na mada zitatolewa na mabingwa wa sheria na katiba.

SEE: Advert on Mwananchi, september 5, 2010, Page 5

Kwa nini "mapungufu" katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 na sio "mapungufu" katika Katiba ya Zanzibar, 1984? Hapa naona Wazanzibari wanataka kutuingiza mkenge katika mjadala huo bila kujijua!
 
nani kasema zanzibar si nchi? hebu tafuteni vizuri hizo kumbukumbu zenu ili mujue kuwa ni nchi au siyo. Hivi kama huyo Sengodo Mvungi anayewatia ujinga watanzania kwa kusema Zanzibar si nchi anajua vizuri Historia ya Zanzibar na Tanganyika na jinsi huo muungano ulivoanzishwa au anpiga kelele tu kwa vile kazizowea? Aliulizwa dola inatakiwa iwe na nini akasema mambo manne; 1:watu, 2:Uongozi wenye maamuzi, 3:Ardhi yenye mipaka, 4:kutambulika kimataifa. Swali linakuja hapa, je Zanzibar haina vitu vyote hivo? Kuna watu, viongozi, ardhi ambayo mipaka yake si ya kuwekwa na mtu(mzungu) bali ni mipaka iliyowekwa na mungu (bahari)na hilo la mwisho kama hajui historia ya zanzibar arudi asome tena, Zanzibar ilikuwa nchi ya kwanza kuwa na uwakilishi katika Umoja wa Mataifa, kabla hata ya Tanganyika kufikiria suala hilo. Sasa kama wanzanzibari wanadai nchi yao kisha wanaambiwa si nchi kwa misingi ambayo haipo kabisa, ni jambo la kushangaza sana. Sisemi kama muungano usiwepo, la ila wapeni wazanzibari kile wanachokidai bila kupiga makelele. Naamini watu wenye akili na wasomi kama hao kina Sengodo Mvungi wakikaa pamoja na kujadili na kukubaliana juu ya matakwa ya wazanzibari bac hayo ni mambo madogo na rahisi sana kutekelezeka, kama vile ilivokuwa rahic kwa baba yenu wa taifa kuunda muungano........!!!!
 
nani kasema zanzibar si nchi? hebu tafuteni vizuri hizo kumbukumbu zenu ili mujue kuwa ni nchi au siyo. Hivi kama huyo Sengodo Mvungi anayewatia ujinga watanzania kwa kusema Zanzibar si nchi anajua vizuri Historia ya Zanzibar na Tanganyika na jinsi huo muungano ulivoanzishwa au anpiga kelele tu kwa vile kazizowea? Aliulizwa dola inatakiwa iwe na nini akasema mambo manne; 1:watu, 2:Uongozi wenye maamuzi, 3:Ardhi yenye mipaka, 4:kutambulika kimataifa. Swali linakuja hapa, je Zanzibar haina vitu vyote hivo? Kuna watu, viongozi, ardhi ambayo mipaka yake si ya kuwekwa na mtu(mzungu) bali ni mipaka iliyowekwa na mungu (bahari)na hilo la mwisho kama hajui historia ya zanzibar arudi asome tena, Zanzibar ilikuwa nchi ya kwanza kuwa na uwakilishi katika Umoja wa Mataifa, kabla hata ya Tanganyika kufikiria suala hilo. Sasa kama wanzanzibari wanadai nchi yao kisha wanaambiwa si nchi kwa misingi ambayo haipo kabisa, ni jambo la kushangaza sana. Sisemi kama muungano usiwepo, la ila wapeni wazanzibari kile wanachokidai bila kupiga makelele. Naamini watu wenye akili na wasomi kama hao kina Sengodo Mvungi wakikaa pamoja na kujadili na kukubaliana juu ya matakwa ya wazanzibari bac hayo ni mambo madogo na rahisi sana kutekelezeka, kama vile ilivokuwa rahic kwa baba yenu wa taifa kuunda muungano........!!!!

Hapa ndugu rayyaan ujue kuwa Dkt Sengodo Mvungi alikuwa anatoa maoni ya kisheria na wewe umetoa maoni yako. Sasa usifanye maoni yako kuwa ni "marking scheme" mpaka tukubaliane na wewe kwa kila kitu unachosema. Unapodai kuwa Zanzibar ina uongozi wenye maamuzi sijui unamaanisha "maamuzi yote" yaani sovereinty au unamaanisha nini? Na kama Zanzibar ina maamuzi yote unafikiri inaweza kupigana vita peke yake? Inaweza kujiunga na jumuiya ya kimataifa peke yake?
Na unapodai kuwa Zanzibar inajulikana kimataifa unamaanisha lipi hapo? Zanzibar ilikuwa mwanachama wa UN lakini si sasa! Kwa hiyo UN inajua kwamba kuna visiwa vinaitwa Zanzibar vilivyoko nchini Tanzania lakini vyenyewe sio nchi!
Na huko kuwa na mipaka, hata Kigoma ina mipaka na watu pia, lakini sio nchi!
 
Hakuna Effect yoyote ile ukitangaza Nchi moja iungane na Nchi nyingine ili mradi yawepo Makubaliano kati ya hizo nchi mbili zinazo ungana.

Kwani Wazenj walipotangaza Zanzibar kuwa nchi walikubaliana na nani?
 
Mimi nakuwa mgumu kukubaliana na DR MVUNGI kwamba muungano unavunjwa kwa marekebisho ya Katiba ya Zanzibar. Muungano ni zao la Hati ya Muungano ambayo iliafikiwa na pande mbili za muungano na hatimaye kuwa sehemu ya msingi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Pamoja na kuwepo serikali ya Muungano chini ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano, bado Zanzibar ilibaki kuwa na Katiba yake. Katiba ya Zanzibar ni zao la wananchi wa Zanzibar kwa kupitia Baraza lao la Kutunga Sheria. Hamna sehemu yoyote katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano inayoitiisha Katiba ya Zanzibar kwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Kwa maoni yangu Raisi Kikwete hapaswi kulaumiwa kwa marekebisho ya Katiba ya Zanzibar kwakuwa Raisi wa Jamhuri sio ofisi inayoundwa chini ya Katiba ya Zanzibar wala haiwajibiki kwa Katiba ya Zanzibar. Raisi wa Jamhuri hana mamlaka yoyote halali katika Katiba ya Zanzibar. Hana ubavu kuwazuia Baraza la Wawakilishi kurekebisha Katiiba ya Zanzibar. Ni kwa maana hiyo nakubaliana na Mgongolwa kwamba suala hili ni la kisiasa zaidi kuliko kishearia.

Hata Katiba ya Jamhuri ambayo kimsingi chimbuko lake kuhusiana na muungano ni Hati ya Muungano imeshakiuka makubaliano ya msingi yaliyomo katika Hati ya Muungano lakini muungano bado upo. Mambo chingu nzima ambayo awali hayakuwa ya muungano yamefanywa kuwa ya muungano kwa marekebisho ya Katiba. Bahati mbaya wakati katiba inarekebishwa kugeuza mambo yasiyo ya muungano kuwa ya muungano vifungu vya Hati ya Muungano kuhusiana na masuala hayo vimebaki hivyo hivyo.

Hayo ni baadhi ya masuala ambayo yanaweza kijadiliwa na Mahakama ya Katiba inayotamkwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Kwamba
GEORGE JINASA
 
Jamani hivi kwa nini Zanzibar isiwe dissolved na kuwa assimilated ktk Jamhuri ya Muungano?
Mi sielewi Muungano wa nchi mbili halafu moja inabaki kuwa nchi. Hebu assume nchi ya USA na ndani yake kuna nchi ya Washington DC.
I don't get it!
 
Back
Top Bottom