Dkt. Mwigulu L.N, (Phd) Pitia haya utapata jambo fulani muhimu

Taratibu zilizopo ni za hovyo, ndio mana nimeegemea kwenye upotevu wa fedha katika ufuatiliaji.

Nimetoa mfano flan wa mradi wa 45 M.

unavyosema hizi taratibu, basi ni haki kwa watendaji kufanye yale yaliyoko kwenye taratibu, ikiwemo kulipana posho hata kwenye kazi ambazo hazifai kulipwa posho.
 
Nimekuelewa vizuri..

Mimi.sio Mwigulu na Wala siko hapa kumjibia ila miongoni mwa uliyopendekeza ndio serikali inataka ifanye hivyo..

Mfano kwenye taasisi ambazo kuna wakaguzi wa ndani huwa wanafuatilia utekelezaji wa mradi from scratch tena hawaishii kufanya ukaguzi bali kufanya monitoring pia..

Shida ilikuwa inakuja ni kwamba unaemkagua ndio anatakiwa akuwezeshe pia taarifa ya ukaguzi huwa inajadiliwa na hao maafisa masuuli huwataka wakaguzi kuondoa baadhi ya hoja..

Pendekezo la serikali Kwa sasa litaziba hiyo ombwe..Kuhusu wakaguzi wa Nje kuvizia nadhani ndio maana wameamua kuajiri watumishi wengin Ili wasisubirie mwisho wa mradi..

Na jambo la mwisho wakubwa wanazingua.sana hasa wakiwa na maslahi na mradi husika.
 
Kenya, baada ya kufanya mabadiliko ya Elimu yao ambayo imekuwa CBC kwa sasa(competency based curriculum), sasa Benki ya Dunia imeitambua Kenya Kuwa na elimu bora katika Bara​
Mleta mada akili huna sio kazi ya benki yeyote duniani kutambua kiwango cha elimu kuwa ipi bora .Hivi kwa akili yako unsiona hiyo ni kazi ya benki ? Hata kama akili huna?
 
Hapana.

Inawezekana kabisa taratibu zilizopo huzielewi.

Ninachoweza kukubaliana nawe ni kama watu wanajifanya wanafuata taratibu kumbe wanatumia mwanya huo kuvuruga taratibu zenyewe.

Sikubaliani nawe kabisa kwamba taratibu zilizopo ni mbovu. Sema hazitimizwi ipasavyo.

Ninaelewa wazi kabisa katika nchi yetu tulivyo na tabia ya kulaumu tu kila kitu huku hatutimizi yale tunayoyalalamikia sisi wenyewe.

Kwa bahati nzuri nimesoma hadi hapo ulipoelezea udhaifu wa hao watu katika ngazi hizo. Hukueleza chochote kinachoonyesha kuwa taratibu zilizopo hazifanyi kazi, bali kinachoonekana ni kuvunja taratibu kwa wahusika, tena kwa maksudi kabisa!

Na mbaya zaidi hawawajibishwi na yeyeyote. Je, hili nalo utasema taratibu haziruhusu?

Andiko lako, 'at least,' hadi nilipokomea na kushindwa kuendelea kusoma, lina udhaifu. Umeliwasilisha kama una maslahi ndani ya hayo unayoyazungumzia na kuyapendekeza yafanyike.
 
Mleta mada akili huna sio kazi ya benki yeyote duniani kutambua kiwango cha elimu kuwa ipi bora .Hivi kwa akili yako unsiona hiyo ni kazi ya benki ? Hata kama akili huna?
Taratibu mkuu YEHODAYA, haya ni majadiliano tu, mkuu wangu, hakuna sababu ya kuitana majina.

Kenya wameweka mfumo mzuri sana wa elimu yao sasa hivi kama kweli watatimiza wanayonuia kuyapata katika elimu hiyo.
Benki hiyo inayosifu, ni wadau wakubwa katika elimu katika nchi mbalimbali, hata hapa kwetu. Umesahau wale mabinti wa Magufuli waliopata uja uzito; na ile hela, (ngapi vile? Najua kilikuwa ni kitita cha kutosha).

Kwenye mambo kama haya tuwe na subira mkuu, kwa sababu ni mambo muhimu sana katika nchi yetu.

Ninasubiri kusikia/kuona kazi za Profesa (nonsense)- Mkenda, kwa kazi atakayoifanya akiwa hapo. Nina matarajio mazuri naye, kama nilivyokuwa nayo na yule mama wa Kigoma, ambaye kwa kweli sijui kwa nini alivurunda kwenye wizara ile!
 
Mleta mada akili huna sio kazi ya benki yeyote duniani kutambua kiwango cha elimu kuwa ipi bora .Hivi kwa akili yako unsiona hiyo ni kazi ya benki ? Hata kama akili huna?
Nilisema humu, sasa ivi Afya ya akili imekuwa tatizo sugu! Unadharau Benki ya Dunia ambayo imekuwa ikitoa misaada lukuki ya Elimu hapa Tanzania??

Unatatizo la Afya ya Akili!
 
Mkuu Kalamu, kama ningewasilisha hoja kulingana na mjadala flani tuliofanya, hakika ningefahamika kirahisi!

Hii nafaham kuna ambao wanajua A-Z ya hiki kilichoandikwa, ingawa ni kama nimechanganya changanya ujumbe, na tayari kuna wanao nihisi, wamenijia inbox.

Kuna jambo liko ndani ya mada, ndio core issue, na inawaumiza sana.

Asante
 
Watu wanawaza kuongeza mabasi we unazungumza mambo ya ufuatiliaji matumizi.
 
Hayo yote umeandika ya nini hapa bongo?

Mwigulu aache kulamba Asali Je aumize kichwa chake hapa?
Mkuu tunaandika kwakuwa nafsi zinatusuta sana, kuna mambo yanaendelea aisee, unabaki kuinamisha kichwa chini.
 
Mimi siyo mtaalam wa mambo haya, lakini najua hakuna 'rocket science' katika mambo haya ya kumfanya asiyekuwa mtaalam kuyaelewa, akijitahidi kuyaelewa.

Haya unayozungumzia hapa, ni sehemu moja tu, katika mambo ya sehemu zingine serikalini yasiyofanyika kama yalivyolengwa. Ukiangalia, kila sehemu kuna upungufu na malalamiko katika utendaji.

Sasa basi, katika sehemu yenu hii ya matumizi ya fedha za waTanzania, kila mwaka, ndiyo nimesema kila mwaka karibu malalamiko ni yale yale; na hasa kila baada ya Mkaguzi Mkuu wa serikali anapowasilisha ripoti yake, kuna kelele nyingi sana husikika toka kila sehemu. Baada ya kelele hizo, kila kitu huwa kimya, kana kwamba hakuna chochote kilichotokea, na watu huendelea na shughuli zao kama kawaida, hadi msimu mwingine wa ripoti na kelele kupigwa!

Hivi kwa nini huwa hatujiulizi mambo yanakuwa hivi, na kuamua kuchukua hatua?

Watu na taasisi zote ulizozitaja humo kwenye andiko lako, wanarudia yale yale, mwaka hadi mwaka!

Sasa kama siyo ukichaa wa nchi yetu huu, sijui tuuite kitu gani!

Kila mara nasema humu, kwenye jukwaa hili hili la JF, kwamba wataalam sasa, nchi yetu haina uhaba nao katika nyanja mbalimbali; bali tatizo hawa wataalam hatujui kuwatumia, na mara nyingi tunawageuza kuwa ndio wanakuwa kikwazo kikubwa katika ufanisi wa nchi yetu.

Taratibu zipo, lakini hazifuatwi au zinageuzwa kuwa uchochoro wa kupitishia uchafu.

Nini Kifanyike kubadili hali?
Ngoja niache hili swali likielea. Lakini naamini bila wasiwasi kabisa kwamba inawezekana sana kukomesha upuuzi huu mwingi uliomo ndani ya serikali.
 
Ukifuatilia bajeti ya ufuatiliaji wa fedha za umma, hakika utalia mkuu!

Matumizi ni makubwa sana yanayoingia mifukoni mwa watu! sijui tatizo ni nini hasaa! Je mamlaka hazioni au ni makusudi??
Kiila mmoja anakula kwa urefu wa kamba yake..
 
Kiukweli, tunasafari ndefu sana, jambo hili ni kama masihara lakini usemacho ni kweli kabisa.
Bado Sana, uongozi ni ajira binafsi kwa maslai binafsi na sio wito wa kutumikia umma
 
Nchi masikin lkn imejawa milolongo miingi ya ufuatiriaji wa miradi, huu ni upumbavu.

Nchi masikin lkn imejawa ngazi nyingi za viongoz wasio na tija, binafsi huwa sioni umuhimu wa kuwa na wakurugenzi ktk wilaya kama kuna mkuu wa wilaya.

Binafsi sioni umuhimu wa mradi mdogo kufuatiliwa na rundo la viongoz, na bado mradi unakwama ama kuzingua.

As my wish kwa wenye nchi, Mfumuko wa muundo wa serikali ni muhimu sana kwa hii nchi, tunaweza kuwa tunazunguka sana kumbe tatizo ni sisi wenyewe,

Ondoa/futa kabisa baadhi ya levels za watumishi kama hao wakurugenzi, sjui madiwani, wenye viti wa mitaa, na hao waitwao mameya wa jiji maana hawana maana zaidi ya kuongeza upigaji.

Inauma lkn ndio ukweli, hiyo pesa inapotea kwa kuendekeza milolongo mingi ya ufujaji pesa wakat nchi yenyewe masikini.

Mabadiriko ni ngumu kutokea bila kumpata kiongozi sahihi, na tusije tegemea mabadiriko kutoka kwa hizo aina za wanasiasa wakina mwigulu&Sa[emoji817].

Hii nchi upigaji upo kwanzia ngazi ya mkuu wa nchi mpka kwa mtendaji wa mtaa, so kila mtu anapiga kwa nafasi yake.

Mabadiriko ni rahis sana kuyafikiria ukiwa nje ya system, lkn ukishaingizwa na kuanza kulambishwa asali ambayo ni jasho la watanzania, hakika unasahau mpaka majukumu yako ktk taifa.

Tuombe tu aje atokee kiongozi makini nje ya haya majambazi ya c+c+m
 
Haya ni matokeo ya kufanya kazi kwa kuviziana ili kuonekana taasis flan inafanya kazi.

Kungekuwa na mfumo wa utendaji kazi wa pamoja, hayo yasingekuwepo.

Ndio mana nasema, tusione aibu kubadilisha mifumo yetu, hasa inayotusababishia gharama katika mipango ya miradi ya maendeleo
 
Mkuu umeonge kwa uchungu sana, nikweli kabisa upigaji umekithiri , na sioni dalili za kujinasua hapa tulipo.

Kila mtu anamawazo ya upigaji tu! Mungu atusamehe kwakweli!
 
Nimeandika bila kufuata mtiririko, hoja na mpangilio malumu, hii ni kwa sababu za kimsing na usalama.
Mbona hatuna shida ya usalama wasiwasi wako wa nini Tena?
===
Asante kwa kutetea hoja zako vyema. Hasa hili la fedha nyingi kusimamia fedha kidogo! Mwisho wa siku mradi haukidhi thamani ya hela. Bila kubana na kudhibiti matumizi ya serikali kwa kujikita kuimarisha na kukamilisha miradi ya maendeleo, hata tukiwatoza kodi na tozo sisimizi wadudu wote wanaopatikana Tanzania kamwe hatutakuja kujitegemea kiuchumi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…