MAAJABU YA KALUNGUYEYE KWENYE TIBA ZA KIASILI NA KUFICHUA UCHAWI, KUWEKA KINGA
✡️HUONDOA MIKOSI NA VIFUNGO MWILINI (saga miba na ngozi ya kalunguyeye Kisha changanya Kwa pamoja na dawa inaitwa HABATI NUKSI YA UNGA Kisha utakuwa unaoga na kujifukiza kutwa mara 2 Kwa siku 14.
⚛️KUITA WATEJA KWENYE BIASHARA(saga miba na ngozi ya kalunguyeye na manyoya ya ndege anaitwa nyangenyange Kisha changanya na dawa inaitwa KASERA halafu utakuwa unaoga na kuchoma kwenye biashara yako kutwa mara 2 Kwa mda wa siku 10 Kwa manuizi.
☸️KULETA MVUTO KWA WATU NA KUKUFANYA UKUMBUKWE KAMA ULIKUWAGA UMESAHAULIKA NA KUDHARAULIKA(saga miba na ngozi ya kalunguyeye pamoja na shiroto na gamba la kakakuona na ngweshi Kisha utachanganya na dawa zinaitwa MPAPATIKO na MKUMBI halafu utakuwa unaoga na kujifukiza na kuchoma Kwa manuizi Yako kutwa mara 2 Kwa siku 14.
✡️ZINDIKO LA MJI MCHAWI AKIJA ACHOMWE NA MIBA(unguza miba na ngozi ya kalunguyeye pamoja na mzizi wa muwa na mzizi wa mpingo Kisha saga pamoja upate unga wake.
JINSI YA KUANDAA MCHANGANYIKO WAKO
utachukuwa chupa Tano zile ndogo Kisha utaweka hiyo dawa Yako kwenye chupa hizo halafu ukishaweka hiyo dawa weka tena na sindano Moja Kila chupa na kipande Cha wembe Kila chupa na bangi Kila chupa hapo dawa Yako imekamilika kwahiyo utafukia Kona nne na katikati ya mji wako wakati wa usiku Kwa manuizi ambayo umenuwia.