DKT. Nchimbi amuagiza Bashungwa, ujenzi wa Barabara ya Kyerwa – Karagwe uanze

DKT. Nchimbi amuagiza Bashungwa, ujenzi wa Barabara ya Kyerwa – Karagwe uanze

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Emmanuel Nchimbi amemuelekeza Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa kuhakikisha utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya Kyerwa - Omurushaka Karagwe (km 62.5) kwa kiwango cha lami unaanza mara moja ili kuondoa adha wanazozipata wananchi wa Wilaya ya Kyerwa na Karagwe.

Dkt. Nchimbi ametoa agizo hilo leo tarehe 08 Agosti, 2024 wakati akizungumza na wananchi wa Kyerwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Stendi ya Mabasi ya Nkwenda, Wilaya ya Kyerwa Mkoani Kagera.

Dkt. Nchimbi ameeleza kuwa lengo la ziara yake ni pamoja na kusikiliza kero mbalimbali za wananchi, kuangalia Utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na kuimarisha Chama cha Mapinduzi.
WhatsApp Image 2024-08-08 at 15.03.32_e5631cba.jpg

WhatsApp Image 2024-08-08 at 15.03.35_b6ef69dc.jpg
“Huu ni Mkoa wa 15 tukiendelea kusikiliza kero za wananchi na kakagua utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na hapa changamoto yenu kubwa ni barabara ya kyerwa hadi Omurushaka”,amesema Dkt. Nchimbi.

Dkt. Nchimbi ameeleza kuwa katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongzwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan Mkoa wa Kagera imepokea fedha kutoka Serikali Kuu jumla ya Shilingi Trilioni 12 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya Miundombinu, Afya, Elimu na Umeme ili kuhakikisha maisha ya wana Kagera yanabadilika.
WhatsApp Image 2024-08-08 at 15.03.33_685aaccf.jpg

WhatsApp Image 2024-08-08 at 15.03.32_b34d5f00.jpg
Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amemuahidi Katibu Mkuu Dkt. Nchimbi kumleta na kumkabidhi kwa wananchi Mkandarasi aliyepatikana kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya Kyerwa - Omurushaka (km 62.5) kwa kiwango cha lami.

Bashungwa ameeleza kuwa tayari Mkandarasi ameshaoneshwa eneo la kujenga Kambi na eneo la kuweka mitambo ili kuanza ujenzi wa barabara hiyo
 
Bora aisee, nilikuwa nateseka mno kutoka Karagwe kufika Nkwenda.
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Emmanuel Nchimbi amemuelekeza Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa kuhakikisha utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya Kyerwa - Omurushaka Karagwe (km 62.5) kwa kiwango cha lami unaanza mara moja ili kuondoa adha wanazozipata wananchi wa Wilaya ya Kyerwa na Karagwe.

Dkt. Nchimbi ametoa agizo hilo leo tarehe 08 Agosti, 2024 wakati akizungumza na wananchi wa Kyerwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Stendi ya Mabasi ya Nkwenda, Wilaya ya Kyerwa Mkoani Kagera.

Dkt. Nchimbi ameeleza kuwa lengo la ziara yake ni pamoja na kusikiliza kero mbalimbali za wananchi, kuangalia Utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na kuimarisha Chama cha Mapinduzi.
“Huu ni Mkoa wa 15 tukiendelea kusikiliza kero za wananchi na kakagua utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na hapa changamoto yenu kubwa ni barabara ya kyerwa hadi Omurushaka”,amesema Dkt. Nchimbi.

Dkt. Nchimbi ameeleza kuwa katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongzwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan Mkoa wa Kagera imepokea fedha kutoka Serikali Kuu jumla ya Shilingi Trilioni 12 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya Miundombinu, Afya, Elimu na Umeme ili kuhakikisha maisha ya wana Kagera yanabadilika.
Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amemuahidi Katibu Mkuu Dkt. Nchimbi kumleta na kumkabidhi kwa wananchi Mkandarasi aliyepatikana kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya Kyerwa - Omurushaka (km 62.5) kwa kiwango cha lami.

Bashungwa ameeleza kuwa tayari Mkandarasi ameshaoneshwa eneo la kujenga Kambi na eneo la kuweka mitambo ili kuanza ujenzi wa barabara hiyo
Kweli siasa mchezo mchafu.
Kauli hizi zimepitwa na wakati.
 
Back
Top Bottom